simplemind
JF-Expert Member
- Apr 10, 2009
- 16,409
- 9,183
Wakazi wa Zanzibar,Mombasa Tanga wanasema mvua inakunya. Bara wanasema inanyesha. Yupi sahihi?
Wakazi wa Zanzibar,Mombasa Tanga wanasema mvua inakunya. Bara wanasema inanyesha. Yupi sahihi?
Bw. Simplemind ninajitosa kujadili hoja uliyoileta jamvini. Kwa ueledi (soma weledi) wangu mi ninaona asemaye 'mvua imenyesha' na yule asemaye 'mvua imekunya' wote wako sahihi ila tu wametumia kauli tofauti katika kitenzi cha tungo hiyo. Ukijadili mofolojia ya neno 'kunyesha' na 'kunya' yote yana asili ya mzizi mmoja yaani -ny-. Ni kutokana na mzizi huo mnyambuliko unatuletea maneno mzo mzo kutegemea maana ya msemaji. Tazama mifano hapa chini:
Kauli Neno nyambuo
Kutenda Ku-ny-a
Kutendea Ku-ny-e-a
Kuntendwa Ku-ny-ew-a
Kutendesha Ku-ny-e-sh-a
Kutendeshea Ku-ny-e-sh-e-a
Lakini matumizi ya kimuktadha tunasema kwamba pale ambapo mtu anasema 'mvua imemnyea' inamaanisha kuwa mvua iliyomtendea ilikuwa kubwa sana na pasipo shaka anakuwa ametota si haba.
Nawasilisha!!!
Bw. Simplemind ninajitosa kujadili hoja uliyoileta jamvini. Kwa ueledi (soma weledi) wangu mi ninaona asemaye 'mvua imenyesha' na yule asemaye 'mvua imekunya' wote wako sahihi ila tu wametumia kauli tofauti katika kitenzi cha tungo hiyo. Ukijadili mofolojia ya neno 'kunyesha' na 'kunya' yote yana asili ya mzizi mmoja yaani -ny-. Ni kutokana na mzizi huo mnyambuliko unatuletea maneno mzo mzo kutegemea maana ya msemaji. Tazama mifano hapa chini:
Kauli Neno nyambuo
Kutenda Ku-ny-a
Kutendea Ku-ny-e-a
Kuntendwa Ku-ny-ew-a
Kutendesha Ku-ny-e-sh-a
Kutendeshea Ku-ny-e-sh-e-a
Lakini matumizi ya kimuktadha tunasema kwamba pale ambapo mtu anasema 'mvua imemnyea' inamaanisha kuwa mvua iliyomtendea ilikuwa kubwa sana na pasipo shaka anakuwa ametota si haba.
Nawasilisha!!!