Muziki wa dansi Ulipokuwa Muziki!!!

mcmzungu

Member
Jul 11, 2015
48
65
Nakumbuka kipindi hicho muziki wa dansi ulipokuwa muziki Twanga wakitamba na nyimbo 'jirani' utunzi wa Ally Choki, TOT Band na wimbo 'Masimango' utunzi wa Waziri Sonyo, African revolution na 'Tunda special' utunzi wa Muumuni Mwinjuma, FM academia 'Dunia Kigeugeu' na Stono Musica wimbo 'Binadamu' utunzi wa marehemu Ndanda Kosovo ilikuwa ni Raja.

Nakumbuka Muumini Mwinjuma alikuwa anarap 'Wazimu Wangu Ukinipanda hata nguo Nitavua' na kweli mashabiki walikuwa wanavua kutokana uhondo wa muziki wa dansi. Au Ally Chocky alipoingia ukumbini na Farasi mpaka kuitwa 'Mzee wa Farasi'. Nakumbuka vijembe kati ya Ally Chocky, Banza,Muumin au Ndanda Kosovo na Totoo ze Bingwa ilikuwa ni burudani sana.

Najiuliza kwanini muziki wetu wa dansi la kizazi kipya limechuja wakati Ally Choki, Muumin, Totoo ze Bingwa, Badi Bakule, Lwiza Mbutu, Kalala Junior, Ferguson, Nyoshi el Sadaat, Patcho Mwamba, Mule mule FBI, Charles Baba, Chokoraa bado mpo mmeacha mzigo wote kwa Christian Bella ambacho ilibidi Mgawane riziki .

Mbaya zaidi hakuna Mwanamuziki wa dansi Mtanzania hata mmoja anayekimbizana na wasanii wa bongo flavour. Unaweza kusema tatizo ni Promo lakini zipo njia nyingi mno kuwafikia Mashabiki kama magazeti, TV, Youtube, Instagram, Blogs nk.

Tunaomba sana Mturudishie muziki Wetu kama zamani ulizeni hata bongo flavour Wanatumia mbinu gani.Nawatakia heri na fanaka Wasanii wa dansi katika mwaka huu mpya na Natamani ujumbe uwafikie popote walipo.Nakaribisha maoni ya Wadau mbalimbali.
 
Uzi huu uendelee ikibidi Moderator uiweke stick kama special thread. Muziki wa dansi ulitisha sana mwishoni mwa miaka ya 90 na mwanzoni mwa miaka ya 2000 baada ya wabongo kuchoshwa na muziki wa Congo.

Watu kama Ally Choki, Banza Stone, Mwinjuma Muumin, na Ndanda Cossovo walifanya makubwa kuuweka juu huu muziki kabla haujaja kupokewa kijiti na Bongofleva. Enzi hizo uzinduzi wa Album ilikuwa gumzo, nikikumbuka zinduzi za album za Twanga Pepeta full mbwembwe, Mara Ally Choki atinge ukumbini na Farasi, Mara Kijiko, Mara aingilie juu ya ukumbi, alikuwa akiacha gumzo kila uzinduzi.

Muumin naye alitisha sana na wimbo wake Tunda akiwa Tamtam, huku Banza Stone akitisha na Mtaji wa Maskini bila kumsahau Ndanda Kosovo 'kichaa' na wajelajela wenzake. Makundi yaliyotisha ni mengi, ikiwa ni pamoja na wazee wa miduara kina Chuchu Sound ambapo unakutana na vichwa kama Chuchu Yusuph, Omary Mkali na Mao Santiago
 
Inasemekana tatizo lilikuwa wanalogana sana.

Kuna mzee Bagamoyo huko kila Muumini anapotoa wimbo mpya anachofanya yeye ni kwenda kusafisha kaburi lake.

Kisa Muumini alienda kwa Mtaalamu amfanyie mambo...Mambo yalipokubali Muumini akaingia mitini hapo ndio bwana mganga alipoizika nyota ya Muumini.

Hizi siri za Muumini zilitoka hatujui na hao wengine walificha mangapi.
 
Hebu tujiulize, mbona Kongo mziki wa dansi una mafanikio makubwa wakati sisi mambo ni vuluvulu? Bendi zimechoka na wanamuziki wako choka mbaya.
 
Wengi wanaumwa..na ukiwa na mawazo ya ugonjwa utawezaje ku concentrate na utunzi?..R.I.P banza na ndanda...wengine poleni kwa kuumwa....wale wazee kule msondo wote wamepukutika na chanzo kimesababishw na kiumbe mmoja ...gombania goli hazifai basi tu
 
Wengi wanaumwa..na ukiwa na mawazo ya ugonjwa utawezaje ku concentrate na utunzi?..R.I.P banza na ndanda...wengine poleni kwa kuumwa....wale wazee kule msondo wote wamepukutika na chanzo kimesababishw na kiumbe mmoja ...gombania goli hazifai basi tu
Nani huyo mkuu?
 
Wengi wanaumwa..na ukiwa na mawazo ya ugonjwa utawezaje ku concentrate na utunzi?..R.I.P banza na ndanda...wengine poleni kwa kuumwa....wale wazee kule msondo wote wamepukutika na chanzo kimesababishw na kiumbe mmoja ...gombania goli hazifai basi tu
hawa wazee wa bendi walikula bata sana enzi hizo... heshima kwa hassan bitchuka na shaban dede kwa kujitunza..pale msondo, wengi wamepotezwa na huyu mgeni wa kisasa na bado wengi ni wagonjwa kazi za mziki ni kazi za hatari sana kama hauko makini..mziki ni kazi ya kuchungulia kaburi ina anasa na starehe nyingi sana, kama hujaingi kwenye mziki inahitajika semina kubwa sana..
 
hawa wazee wa bendi walikula bata sana enzi hizo... heshima kwa hassan bitchuka na shaban dede kwa kujitunza..pale msondo, wengi wamepotezwa na huyu mgeni wa kisasa na bado wengi ni wagonjwa kazi za mziki ni kazi za hatari sana kama hauko makini..mziki ni kazi ya kuchungulia kaburi ina anasa na starehe nyingi sana, kama hujaingi kwenye mziki inahitajika semina kubwa sana..
Umeandika kwa hisia sana!
 
hawa wazee wa bendi walikula bata sana enzi hizo... heshima kwa hassan bitchuka na shaban dede kwa kujitunza..pale msondo, wengi wamepotezwa na huyu mgeni wa kisasa na bado wengi ni wagonjwa kazi za mziki ni kazi za hatari sana kama hauko makini..mziki ni kazi ya kuchungulia kaburi ina anasa na starehe nyingi sana, kama hujaingi kwenye mziki inahitajika semina kubwa sana..

Shaban Dede amefariki tarehe 06.07.2017, RIP
 
Nimemiss sauti ya badi bakule,yupo pande zipi jaman yule binadam.

Uno la Aisha madinda liliwachanganya wengi sana,nahisi litakua liliondoka na watu wengi sana.
 
Chozi la munyonge malipo Kwa Mungu Babaaeee hata waseme sisi ni kaazi mamaaa ee... FM academia ooh bana na Nzambe,×2 eeeh....RAPA wamekula ya mbuziii...wameota pembee (weka kibezi hapo ya mbuzi)....Jeeelaa jela ni ni mbaaya...jeela jela ni mateso...¶π
 
Huwa najiuliza kuhusu umakini wa hawa watu wa sanaa kwenye mahusiano sipati majibu.
Sina hakika kama elimu ya ukimwi na STI's wamefundwa vizuri. Wengi utasikia kazaa na flani.
Anyway nao ni wana jamii tu!
 
Chozi la munyonge malipo Kwa Mungu Babaaeee hata waseme sisi ni kaazi mamaaa ee... FM academia ooh bana na Nzambe,×2 eeeh....RAPA wamekula ya mbuziii...wameota pembee (weka kibezi hapo ya mbuzi)....Jeeelaa jela ni ni mbaaya...jeela jela ni mateso...¶π
Uko vizuri mkuu
 
Huu ulikuwa muziki safi sijui kwann umepotea...mimi naamini....kumekosekana wawekezaji serious
Ni kweli mkuu tutaumiss sana huu mziki. Kwa sasa tuusikilize tu kama Zilipendwa manake soko la mziki limeshatekwa na vijana wa kisasa na Bongo flavour zao.
Na kiukweli mziki unawalipa kuliko enzi za mziki wetu pendwa.
Vijana wa sasa wamesaidiwa sana na uwepo wa mitandao ya kijamii na namna mpya ya kujitangaza so wanaweza kuulinda mziki wao pia.
Binafsi nimewamiss sana kina Ally Choki, Mwinjuma Muumini, Banza stone (R.I.P), F.M. Academia etc hawa ningependa niendelee kuona Live show zao
Lakini pia napenda kusikiliza mziki wa wakongwe Marijani Rajab, Mbaraka Mwinshehe, Tx Moshi, Rehan Bitchuka, Maalim Gurumo, kwa ujumla mziki wa Dansi wa Tanzania ambao kiukweli ndio unaotambulisha Tanzania.
Tumeshindwa kuulinda kama taifa na kiukweli utakuja kusahaulika na tutabaki na ladha hizi za kimagharibi tu.
So sad!
 
Back
Top Bottom