Muungano ukivunjika, Zanzibar kuwa 'Dubai ndogo'

Nakubalia na wewe Mia kwa Mia ! Leaved there too, nataka owe kesho ili mbatata zetu, nyama, maharagwe etc etc tuwauzie kwa dola sasa!!. Na Hao wa Inge na Waziri waliopo bars sijui watawapa post gani huko!. Infact Kama wao wakipata mafuta obviously hata sisi tutakuwa nayo. Mungu Ibariki Tanganyikawildernesscamps .
Nimekaa Zanzibar kwa miaka saba sasa, nakuhakikishia inawezekana kukatokea machafuko Zanzibar baada ya muungano. Wazanzibari ni watu ambao ni rahisi kudanganywa na wanasiasa. Na kwa sababu ya wazanzibari wengi kukosa kazi, wana muda mwingi wa kusikiliza uwongo bila kufanya utafiti wa maana.
Tuanze na OIC. Kati ya waisilamu wenye matatizo makubwa ya kimaisha hapa ulimwengini ni Wapalestina. Lakini OIC haiwasaidii Wapalestina badala yake Wapalestina wanaishi kwa msaada kutoka EU. Sasa niwaulize, kulikoni OIC (Jumuia ya nchi za Kiisilamu) zishindwe kuwasaidia waislamu wenzao wa Palesintina ila wawasaidie wazanzibari? Pili nchi gani ulimwenguni humu imeendelea kwa misaada?
Uchimbaji wa mafuta. Huenda ni kweli kuna mafuta Zanzibar. lakini nawashauri Wazanibari walichukulie suala la mafuta kwa makini sana. Kuna nchi zilikuwa na amani sana hapa Afrika, lakini siku tu mafuta yalipoanza kuchimbwa ndio siku walipigana na maelufu wakafa kwa sababu ya mafuta.
Uvuvi. Uvuvi haujawahi kutajirisha nchi hata moja. Norway ambayo ni tajiri sana, huenda tajiri kuliko nchi zote ulimwenguni hawakutajirika kwa uvuvi pekee. Kwanza utajiri wa Norway umekuwa mkubwa pale walipogundua mafuta na kuanza kuyachimba tena wakakataa kujiunga na OPEC kwa hiyo wanachimba bila mashariti ya OPEC.
Utalii. Utalii wa Zanzibar unaendeshwa kiholela na in fact, hakuna cha kuwavutia watalii Zanzibar. watalii wanaokwenda Zanzibar ni wale masikini, wanawaita vishuka. Alafu, hawana skills za kuendeleza utalii. Mahoteli yaliopo yanaendeshwa na Wakenya na Watanzania bara.
Kuna tatizo kubwa la ufisadi ninaloliona Zanzibar japo watu wengi hawalioni. Viongozi ni matajiri sana ukilinganisha na vipato vyao, yaani mshahara. Miaka ya 2006 niliambiwa na mchumi mmoja kuwa kipato cha ZRB kipindi kile kilikuwa 3 Bil kwa mwezi lakini matumizi halali ya serekali yanayolipwa na mapato kutoka ZRB yalikuwa 1.8 Bil. Kwa hiyo kila mwezi 1.2 Bil ambayo ni sawa na 40% ilikuwa inapotea.
Tatizo jingine ni siasa za uhasama. Siasa za Zanzibar ni za uhasama. In fact, alichokisema Nyerere kuwa wazanzibari wanajiita wazanzibari ndani ya muungano ni kweli. Kuna kipindi watu walikuwa hawasali hata msikiti mmoja, kisa yule ni mpemba na huyu ni muunguja. Mbaya zaidi ni kuwa wanafahamiana na itikadi za kichama zinarithishwa kwa watoto. Sio kama Tanzania bara unamkuta Vicent Nyerere ni CHADEMA lakini Makongoro Nyerere ni CCM na wote wanagombea ubunge. Niliona kipindi Vicent Nyerere akifanya kampeni kule Musoma, Madaraka nyerere, japo ni CCM yule, lakini alikuwa anampa support.
Last, nadhani zaidi ya theluthi ya Wazanzibari wanaishi bara. Na mbaya zaidi ni kuwa wale wenye uwezo kielimu na kifedha in terms of mitaji, ndio wako bara. Nimeenda pemba na kuilinganisha na matajiri wa kipemba walioko daa, kwa kweli havifanani.
Muungani japo si upendi kabisa kwa sababu naamini Zanzibar inapendelewa sana, kwa mfano wabunge wanaotoka Zanzibar ambao ni zaidi ya 60 katika bunge la jamhuri ya muungano wakati in terms of resource contribution Zanzibar inachangia kidogo zaidi chini ya mkoa wangu wa Kilimanjaro, naona kama si halali. Wangetakiwa walete wabunge chini ya 10 kama mkoa wangu wa Kilimanjaro.
 
Na Bakhresa akirudi Zanzibar, soko la unga litakuwa kwa wazanzibar tu ambao population yao haifiki hata milion nne. Itabidi auze semi-trailer zake zote zinazosambaza unga kwenda Zambia, Congo na Malawi, kwani akirudi Zanzibar itabidi anunue ndege za kusafirisha bidhaa zake kupeleka huko Zambia na Congo kwani kamwe Tanganyika haitaruhusu bidhaa yoyote kutoka Zanzibar kuingia au kupitia ardhi yake

usisahau mahindi na bidhaa nyingine atapata wapi?
 
Zanzibar is a jigger in a toe, an irksome sweetheart. It is high time Tanganyka helped her look for a new partner... Urika! Arabs are trustworthy suitors.

Moja yamambo ambayo zenji wanadhani kwamba yanakwamisha maendelo yao ni muungano. Wengi hutamba kuifanya zanzibar ikaribiane na dubai kwa maendeleo, kwa kutumia bandari, misaada ya oic, uchimbaji wa mafuta, uvuvi, na utalii iwapo muungano utavunjika.

Je ni kweli tanganyika inawakwamisha kutimiza azma yao?

Kama jibu ni ndio, vipi visiwa vya sheli sheli, na vinginevyo, navyo vimeungana na tanganyika?

Kama jibu ni hapana, je ni nini ambacho zanzibar wanacho, ila sheli sheli hawana?

Kama hakuna jibu la msingi, muungano na utadumu milele, kelele za mlango.......
 
Muungano ukivunjika Tanganyika tujiadae kupokea wakimbizi wengi wa kisiasa, kibaguzi na kidini!

Huu ndio ukweli! Waunguja watapigana na wapemba; wenye asili ya kiarabu watapigana na wenye asili ya kinyamwezi;
waislamu watawapiga wakristo na kuanzisha sharia! Ilimradi kutakuwa kama Somalia kwa muda hadi tutakapopeleka majeshi yetu kuweka amani kama tulivyofanya Usheli Sheli!

kweli mkuu. hata wale wabunge wa chadema wapigwa mapnga na waislam. Duh hata igunga Tindikali kamwagiwa na waislam. hata yule raia alieuliwa uchaguzi wa Igunga kapigwa na waislam. kumbe hata wakiristo wanakuwa wauaji? ndio maana sasa bara vurugu tupu. hadi mbunge anapigwa mapanga? aliepigwa mkiristo, mpigaji mkiristo, polisi aliesimamia mkiristo.
 
Kiongozi pekee aliyefanya cha maana kwa ZNZ ni Marehemu Karume.
Jumbe alianzisha miradi mipya kibao (michepuo, mashamba ya mpira na hiliki, viwanda vidogo vidogo n.k.) lakini miradi ilikuwa kama nyumba za karata, hakuna mmoja uliofanikiwa isipokuwa kiwanda cha sukari/pombe.

Mwinyi alipokaa uraisi aliwaahidi Wazanzibari watakula tende mbichi, wakaishia kula mbura na fuu.

Marehemu Mzee Wakili, mbiu yake ilikuwa "Serikali haina fedhwa".

Salmini aliahidi ZNZ itakuwa kama Singapore, wananchi wakaishia kubaguana hadi mazikoni badala ya kuleta maendeleo. Lile jengo la Free Duty pale bandarini lililokula mabilioni ya pesa. linaoza.

Karume mwana, alishirikiana na Mkapa kufanya Mauaji.

Hawa waliopo sasa, sijui niwalezeje.

Kwa ufupi, adui wa ZNZ ni Wazanzibari na viongozi wao wenyewe, wasitafute mchawi.

Bora wewe umesema...kikulacho ki nguoni mwako. Tuache hizi hadithi if we want to become seroius about going forward successful
 
^ akili finyu. Zanzibar hakuna ubaguzi wa dini, wala kabila wala uunguja ja upemba! Hamuijui history ya visiwa vya zanzibar. Historia ya zanzibar ukiisoma ndo utajua jinsi gani unguja na pemba walivo ndugu, na hawatogombana, hizo ni fitna za babaenu Nyenyere, akitaka unguja na pemba watengane na wagombane wasiwe wamoja! Lakini hilo halitatokea!
Mimi naona kama ubaguzi utakuja kwenu tanganyika, mmoja kashasema apo juu, tujiandae kuwapokea wapemba wa tmk. Effect kubwa itaonekana kwa tanganyika, MAKABILA 120 hii ni hatari, kumejaa ubaguzi lakini tumewafundisha ustaarabu kidogo mkaelimika lakini tukiondoka mtabaguana sana na mtapigana. Tanganyika ni obstacle kwa maendeleo ya visiwani hili ni kweli. Kama sasa ivi, kuna ishu ya mafuta, sasa mimi nashangaa kwanini mnang'ang'ania mafuta ya watu? Kwanini mnaizuia znz kujiunga na OIC, watu wake ndo wanaotaka kwanini mnawazuia?

ujinga mwingine kweli ni mzigo kweli kweli. haya tueleze kwani kuna watu wanaitwa WAZANZIBAR na WAPEMBA?
 
kweli mkuu. hata wale wabunge wa chadema wapigwa mapnga na waislam. Duh hata igunga Tindikali kamwagiwa na waislam. hata yule raia alieuliwa uchaguzi wa Igunga kapigwa na waislam. kumbe hata wakiristo wanakuwa wauaji? ndio maana sasa bara vurugu tupu. hadi mbunge anapigwa mapanga? aliepigwa mkiristo, mpigaji mkiristo, polisi aliesimamia mkiristo.

Kuwa na heshima wewe. umeamriwa
-kuwaheshim wakristo
-kula chakula ya wakristo
-kuiga maisha ya wakristo ( quruan 5:3, kama sio quruan 3:5) nimechanganya vifungu tu.
 
Asilimia 99.99 ya Wazanzibari ni Waislamu anyway, wakitaka kuanzisha sharia nje ya Muungano rukhsa!

Si wanakubaliana? Na nchi si ni yao? Hii itakuwa pilipili ya shamba kwa Tanganyika, kwa nini ituwashe?

Sasa, na hawa wakristo wawili asilimia 0.001 hawa wanaoishi Zanzibar itawabidi wavumilie, wasilimu au wahame. Wakihama kuja Bara tunaweza kuwa absorb, kwanza sasa hivi nusu ya Wazanzibari wanaishi Tanganyika anyway, pamoja na marais wao wote waliostaafu.[/FONT][/SIZE]

Wote hao rudisha kwao au walipie kuishi ughaibuni kama wenzao wanaotoka Kenya, Uganda nk.
 
Back
Top Bottom