Muumini auawa na mchungaji

Status
Not open for further replies.

ShyaRuwa

JF-Expert Member
Joined
May 30, 2015
Posts
8,252
Reaction score
14,793




Muchungaji mmoja nchini Afrika ya kusini kwa jina la Lethebo Rabalango wa kanisa la Mount Zion general assembly amemua muumini wake ambaye ni mwanamke kwa kumwekea spika nzito juu yake.

Mchungaji Lethebo alimwalika mwanamama huyo mbele ya kanisa ili aweze kuonesha miujiza ya Mwenyezi Mungu, ndipo alipomwamuru mwanamke huyo alale chini na kuwaambia watumishi wa kanisa wamwekee spika juu yake yenye uzito wa 113.4k na mchungaji kukaa juu yake kwa nia ya kumkandamiza.

Mchungaji huyo alisema kwa uwezo wa Mungu mwanamke huyo hatahisi maumivu, ila cha kushangaza mwanamke alibakia kimya baada ya kukosa pumzi,na kusemekana kuwa amepoteza fahamu.

Juhudi za kumwamsha ziligonga mwamba ndipo ikabainika kuwa mwanamama huyo amepoteza uhai. Hata hivyo mchungaji amemlaumu marehemu kwa kusema kwamba hakuwa na imani ya kutosha.
 
Hapa mwenye kutakiwa kuwa na imani ya kutosha ni nani? Hebu ndugu zanguni wenye uelewa wa kutosha njooni mtupe Darasa. Nitafurahi sana kama hii mada itachangiwa sana na watu wenye kuujua ulimwengu wa roho.

Wengi wa Elimu ya kawaida watampiga vita huyu mchungaji, Lakini ningependa kusikia wenzetu wanaoujua ulimwengu wa roho wanasemaje?
 
Ni mchungaji kwakweli.
 
Hahahaha haya ni masihara hakuna na imani ya kutosha????
 
Dah ila picha hazifunguki
Hahahaha haya ni masihara hakuna na imani ya kutosha????
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…