Muuguzi adaiwa kumpiga mgonjwa wakati akimuhudumia jijini Mbeya

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,899
Mama mmoja amedai kupigwa na muuguzi wakati akijifungua katika hospitali ya Rufaa Meta ya jijini Mbeya na baada ya kujifungua muuguzi huyo akamchukua mwanae mchanga na kumtupia kifuani jambo ambalo amesema lilihatarisha uhai wa mwanae.

Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Amos Makalla amefanya ziara ya kustukiza katika hospitali ya Rufaa ya wazazi Meta ya jijini Mbeya na kushuhudia msongamano mkubwa wa akina mama wajawazito hospitalini hapo, na alipofika katika chumba cha akina mama ambao wanasubiri watoto wao ambao wamewekwa katika chumba maalum cha joto, ndipo akakutanana na malalamiko ya mama Salome Waya ambaye amedai kupigwa na muuguzi wakati akijifungua.

Kufuatia madai hayo, mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makalla akalazimika kupitia nyaraka za mama huyo ili kumtambua muuguzi aliyemfanyia ukatili huo na akafanikiwa kumbaini kuwa anaitwa Beatrice Sanga ndipo akatoa agizo kwa mkurugenzi wa hospitali ya rufaa ya kanda ya nyanda za juu kusini, Dk. Goodlove Mbwanji kufanya uchunguzi na kuchukua hatua dhidi ya muuguzi huyo ndani ya siku saba.

Mkurugenzi wa hospitali hiyo, Dk. Goodlove Mbwaji amesema kuwa katika mazingira hayo hawezi kujitetea na badala yake atazingatia maelekezo ambayo amepewa na mkuu wa mkoa.
 
Wewe!!! Tumezaa kwa kuelekezwa vizuri na sio mikofi na kutupiwa mtt. Manesi acheni tabia za kishetan..pam**aaaaff
 
Kujifungua si mchezo kabisa kipigo ni cha muhimu sana so long mama na mtoto wako hai. watoe zawadi kwa midwife na sio kumletea politics hata makala haijui kazi ya kuzalisha!

Wamelazmishwa??hujui ukunga na kz yyte ya yakitabibu ni wito na uwe na moyo wa huruma!!umpge anayejifungua???we utakuwa me ndo maana unaongea upupu!ukiona kz ngumu haikulipi unawaachia wnye wito na kz!km ni kwli adhabu ya kutosha inamuhusu mgumba hyo!!!!!
 
Mama mmoja amedai kupigwa na muuguzi wakati akijifungua katika hospitali ya Rufaa Meta ya jijini Mbeya na baada ya kujifungua muuguzi huyo akamchukua mwanae mchanga na kumtupia kifuani jambo ambalo amesema lilihatarisha uhai wa mwanae.

Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Amos Makalla amefanya ziara ya kustukiza katika hospitali ya Rufaa ya wazazi Meta ya jijini Mbeya na kushuhudia msongamano mkubwa wa akina mama wajawazito hospitalini hapo, na alipofika katika chumba cha akina mama ambao wanasubiri watoto wao ambao wamewekwa katika chumba maalum cha joto, ndipo akakutanana na malalamiko ya mama Salome Waya ambaye amedai kupigwa na muuguzi wakati akijifungua.

Kufuatia madai hayo, mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makalla akalazimika kupitia nyaraka za mama huyo ili kumtambua muuguzi aliyemfanyia ukatili huo na akafanikiwa kumbaini kuwa anaitwa Beatrice Sanga ndipo akatoa agizo kwa mkurugenzi wa hospitali ya rufaa ya kanda ya nyanda za juu kusini, Dk. Goodlove Mbwanji kufanya uchunguzi na kuchukua hatua dhidi ya muuguzi huyo ndani ya siku saba.

Mkurugenzi wa hospitali hiyo, Dk. Goodlove Mbwaji amesema kuwa katika mazingira hayo hawezi kujitetea na badala yake atazingatia maelekezo ambayo amepewa na mkuu wa mkoa.
Kama kuna mashahidi itakuwa vizuri kupata ukweli.
 
Mama mmoja amedai kupigwa na muuguzi wakati akijifungua katika hospitali ya Rufaa Meta ya jijini Mbeya na baada ya kujifungua muuguzi huyo akamchukua mwanae mchanga na kumtupia kifuani jambo ambalo amesema lilihatarisha uhai wa mwanae.

Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Amos Makalla amefanya ziara ya kustukiza katika hospitali ya Rufaa ya wazazi Meta ya jijini Mbeya na kushuhudia msongamano mkubwa wa akina mama wajawazito hospitalini hapo, na alipofika katika chumba cha akina mama ambao wanasubiri watoto wao ambao wamewekwa katika chumba maalum cha joto, ndipo akakutanana na malalamiko ya mama Salome Waya ambaye amedai kupigwa na muuguzi wakati akijifungua.

Kufuatia madai hayo, mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makalla akalazimika kupitia nyaraka za mama huyo ili kumtambua muuguzi aliyemfanyia ukatili huo na akafanikiwa kumbaini kuwa anaitwa Beatrice Sanga ndipo akatoa agizo kwa mkurugenzi wa hospitali ya rufaa ya kanda ya nyanda za juu kusini, Dk. Goodlove Mbwanji kufanya uchunguzi na kuchukua hatua dhidi ya muuguzi huyo ndani ya siku saba.

Mkurugenzi wa hospitali hiyo, Dk. Goodlove Mbwaji amesema kuwa katika mazingira hayo hawezi kujitetea na badala yake atazingatia maelekezo ambayo amepewa na mkuu wa mkoa.
Huyo mama anayedaiwa kupigwa atakuwa mnafiki tu....wasipigwe wote apigwe yeye tu?? Migonjwa mingine bila kuitandika makwenzi hutaweza kusaida
 
Hizi ni tabia ambazo haziwezi kuelezeka katika mazingira ya kawaida ya kibinaadamu. Nesi alipaswa awe mwanajeshi.
Stori ya upande mmoja, umemuuliza huyo nesi upate maelezo yake? Wagonjwa wote wasilalamike kupigwa na huyo nesi alalamike huyo mdada aliyekosa nidhamu?
 
Kujifungua si mchezo kabisa kipigo ni cha muhimu sana so long mama na mtoto wako hai. watoe zawadi kwa midwife na sio kumletea politics hata makala haijui kazi ya kuzalisha!
Huna akili timamu wewe, ukiendelea na tabia yako haitokuchukua muda mrefu, tupo njiani tunakuja, mpuuzi kabisa
 
Wamelazmishwa??hujui ukunga na kz yyte ya yakitabibu ni wito na uwe na moyo wa huruma!!umpge anayejifungua???we utakuwa me ndo maana unaongea upupu!ukiona kz ngumu haikulipi unawaachia wnye wito na kz!km ni kwli adhabu ya kutosha inamuhusu mgumba hyo!!!!!
Msome huyu mkuu hapa chini...
Yapo mazingira umkimchekea mjamzito tu basi tegemea kifo cha mama au mtoto,wakati mwingine wote huyo muuguzi kwa nini ampige yeye tu! Kati ya wote waliojifungua tafadhali umakini na ukomavu wa maamuzi unahitajika hawa wauguzi ni msaada mkubwa sana tuwahurumie sana.
 
manesi wanakuwaga na hasira nadhani kaz wanyofanya ni ngumu ikiwa ktk mazingira magumu na malipo hayasadifu kazi kubwa wanzofanya,lakn sitetei ujinga wa kunyanyasa wagonjwa wakiona kaz imewshinda waache kazi tuu,
Uzazi ni uhai wa watu, kama kazi ngumu si unaacha tu ukafanye iliyo rahisi, tunapitia nchi nzima tukikubaini haina huruma
 
Yapo mazingira umkimchekea mjamzito tu basi tegemea kifo cha mama au mtoto,wakati mwingine wote huyo muuguzi kwa nini ampige yeye tu! Kati ya wote waliojifungua tafadhali umakini na ukomavu wa maamuzi unahitajika hawa wauguzi ni msaada mkubwa sana tuwahurumie sana.
Sio lazima upost, huna hoja ya maana kaa kimya, umeshawahi kuingia chumba cha kujifungulia? au unapost tu pumba zako? Vipi kama mzazi wako angepigwa na kutupiwa mtoto? Au mkeo, au dada yako? Tena mbele yako ukiwa unaona kwa macho yako mwenyewe!! Tutakaowabaini hatutawaonea huruma, kama kazi ngumu acha katafute iliyo rahisi sio kuchezea uhai wa watu, huyo mtoto alierushiwa mama mzazi fikiria kama angeanguka chini angepona? Tatizo kuvamia taaluma za watu, wito hakuna, uwezo wa kufikiri ni hafifu, tunakuja......tukikubaini ni sheria tu watachukuliwa
 
Niliona huyu mama akiwa anasimulia. Aliongea kwa uchungu aiisee . Ila kuna wauguzi ambao si waadilifu kabisa
Badilikeni
 
Huyo mama hana shukrani ...ni kawaida na muhimu mtoto kuwekwa kifuani kwa mama baada ya kujifungua.

Pia sioni umbali wa kutoka kwenye K hadi kwenye kifua utakaomwezesha muuguzi kumrusha mtoto!

Kama alikuwa anabana mapaja sana lazima makofi yamtembelee....

All in all uchunguzi wa wataalamu wa afya ndio utagundua ukweli....

Kama huyo muuguzi ni mzoefu wa kupiga makofi atakuwa na tatizo lakini kama ni mara ya kwanza most likely huyo mama ni shidaa...

Pia kuna haja ya wataalamu wa ukunga Tanzania kuintroduce protocal ya kuzuia maumivu wakati wa kujifungua kwani leo kapigwa mama kesho atapigwa au kupakazwa kinyesi na damu muuguzi simply sababu ni heka heka za uchungu.
 
Pande zote mbili wasikilizwe kwa umakini sana,

Swala la kusukuma mtoto kabla ya muda muafaka linaweza kusababisha kifo cha mtoto,

Na swala la kulabua mjamzito kofi la uso nalo linaweza kumchanganya mjamzito network ikakata,

Hapa wasikilizwe wote kwa umakini mkubwa
 
Back
Top Bottom