Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,744
- 25,446
Mlipuko wa bomu unatokea katika sherehe ya kumpongeza Kamishina wa Jeshi la Polisi, Ibrahim Miraji baada ya kuteuliwa na rais kuchukua nafasi hiyo.
Hapo nyumbani kwake kwenye sherehe hiyo kuna viongozi wengi wa polisi akiwemo IGP Godlove. Mlipuko huo unammaliza Miraji na mkewe tu.
Ukiachana na vifo vya wawili hao, kuna watu wengi wakijeruhiwa na hivyo kukimbizwa hospitalini. Miongoni mwa majuruhi hao alikuwepo mke wa Dilunga, Aisha.
Dilunga alikuwa Naibu Kamishina wa Jeshi la Polisi, yaani akitoka Miraji kwa cheo anafuata yeye. Mwanaume huyo anachanganyikiwa, anamchukua mke wake na kumpeleka hospitali huku akiwa na majeraha makubwa mwilini mwake.
Baada ya kukaa kwa siku mbili, anaambiwa kwamba mkewe alimeuawa hospitalini kwa kuchomwa sindano iliyokuwa na sumu.
Hilo linamuuma na kwa maelezo ya mlinzi aliyewekwa hapo, anasema muuaji alivalia shati jeupe, tai nyekundu na koti la kidaktari.
Dilunga hakubali, anaamua kumtafuta muuaji kwa nguvu zote. Huku akiendelea kusisitiza lazima muuaji apatikane, anapokea taarifa na kuambiwa mkubwa wa polisi mwingine, Dikwe ameuawa nyumbani kwake huko Kibaha, na muuaji alivalia shati jeupe na tai nyekundu, yaani ni muuaji yuleyule ambaye alimuua mkewe kitandani.
Hapo ndipo msako rasmi unaanza, Muuaji Mwenye Tai Nyekundu anaanza kusakwa kila kona pasipo kugundua kwamba angeendelea kuwamaliza viongozi wa jeshi la polisi kila alipojisikia kufanya hivyo.
Kitabu kinapatikana kwa sh. 10000 kwa wakazi wa Dar na 15,000 kwa watu wa mikoani. Kumbuka kwamba hiyo 5000 ni gharama ya kusafirisha kitabu kikufikie.
Mawasiliano: 0718069269.
@chilojr