Kwa kuusoma muswada huu, utagundua kuwa kuna harufu ya dhuluma kubwa mbele yetu. TUCTA, kumbukeni kila mwezi mnachukua asilimia mbili toka kwenye mishahara yetu. Waheshimiwa wabunge, chondechonde--msiupitishe muswada huu kwa sababu hauna sehemu unasema kuhusu watu waliopoteza ajira kwa kufukuzwa ama wanaopoteza ajira kwa redundancy. TUCTA msipopigania hili maana yake mmesaliti wafanyakazi, na hakutakuwa na maana ya wafanyakazi kuendelea kuwa wanachama wakati mnashindwa kuwatetea. Walisema kutakuwa na FAO LA KUKOSA AJIRA, ila haioneshi kama lipo. Enyi mliotunga haya, hivi mna roho gani nyie, mna dini kweli?