hamis77
JF-Expert Member
- Aug 20, 2013
- 11,643
- 19,018
Mungu kupitia Nabii Musa alitoa maelekezo kuhusu uchanganyaji wa mbengu ili kupata kiumbe kimoja.
Kizazi kiovu baadae walichanganya mbegu za wanyama tofauti wakatoa viumbe wa ajabu kina Godzila ,Mungu kupitia Gharika akawaharibu, Kuna watu leo walikuwa wanabisha haiwezekani kuchanganya mbegu ya kiumbe tofauti na Mwingine ukatoa kiumbe tofauti, Lakini Zamani walifanya, na leo wanadamu wamefikia huko
Tusome Hapa, pia usipoelewa pitia Tafsiri mbalimbali , Humo makanisani hao wanaojiita manabii na wachungaji wakisoma hi mistari wanatafsiri kana kwamba Mungu alizuia kupanda shamba moja mahindi na maharage , Lakini maana halisi Ni kuchukua Mbegu ya kiumbe A ukafanya kuunganisha na mbegu B, Kisha upate KIUMBE MMOJA.
Tusome ...
KENYA WAMERUHUSU GMO, Sasa wanazalisha Maparachichi yasiyo na mbegu Kama haya
Tanzania isionje sumu ya GMO kwa kukijaribu kilimo hiki. India walifanya hili kosa na matokeo yalikuwa ni wakulima wadogo laki tatu (300,000) kujiua wenyewe katika muhula wa miaka 20. Hatima kama hii tuiepuke hapo nyumbani kwa udi na uvumba.
# Vinasaba vya epicyte ambavyo vipo kwenye baadhi ya mazao ya vyakula vya GMO (Genetically Modified Organism) kupitia mbegu zake vitazuia ongezeko la watu duniani, kwa sababu kazi ya hiki kinsaba ni kuwafanya wanaume na wanawake wasizae milele -ingawa tendo la ndoa litafanyika kama kawaida. Na kwa kutumia teknolojia inayoitwa “RNA crop interference technology” wame – “fine-tune” huo uhanithi na ugumba uliowekwa kwenye hiki kinsaba cha epicyte uwaathiri Watu Weusi peke yao. Yes, “…GMO food crops have now been fine-tuned to cause irreversible infertility in black people alone.”
# Kupitia lobbyists waliowekwa kwenye idara zao ziitwazo “Political Action Committees (PACs) makampuni mara nyingi huwa yanaweka mifukoni wasomi pamoja na baadhi ya viongozi wa kitaifa ili kuthibiti, hata kupotosha mataifa lengwa. Nchi yetu iwe macho sana na njama za sampuli hii.
Siku ya Alhamisi ya tarehe 6/10/2022 Dr. Ally, kwenye mtandao wa “Uwanja wa Diplomasia” alichapisha andiko lenye kichwa cha habari kifuatacho: ‘GMO, NDIO AU HAPANA KWA TANZANIA’.
GMO
Kwa mujibu wa matokeo ya tafiti za kitaifa na kimataifa, pamoja na uzoefu (real life experiences) ya watu wanaoishi na kilimo hiki ni vema: “GMO iwe Hapana kwa Tanzania.”
Hili andiko la Dr. Ally nimelisoma kwa kina. Katika kutoa tafsiri za GMO na misamiati mingine ya bayolojia andiko lake limekaa vizuri; lilipopwaya ni katika kujibu hofu za watu kuhusu faida na hasara za kilimo cha uhandisi jeni.
Swali la msingi ni hili: Kwa nini taasisi zetu za taifa za utafiti za Tanzania, Kenya na Uganda zinapoteza fedha na wakati kutafiti jambo ambalo limekwisha fanyiwa utafiti “exhaustively” na Umoja wa Mataifa na matokeo yake yapo wazi? Hii, si sawa na kusema baada ya huu utafiti wa Umoja wa Mataifa watu wasitishe tafiti katika fani ya kilimo. La hasha. “Public crop-breeding programmes” ambazo hazirudishi mataifa kwenye utumwa-mamboleo ziendelee, tumekuwa nazo tangu kilimo kiwepo duniani miaka zaidi ya 10,000 iliyopita. Lakini kwa nini tunang’ang’ania GMO ambayo imethibitika: (i) Ina kila aina ya madhara na (ii) Hizo tafiti zetu zenyewe wala hazijitegemei?
(i) Madhara: “In 2009 the American Academy of Environmental Medicine called for a moratorium of GM foods, safety testing and labelling. Their review of the available literature at the time noted that animal studies show serious health risks associated with GMO food consumption including infertility, immune dysregulation, accelerated aging, dysregulation of genes associated with cholesterol synthesis, cell signalling and protein formation, and changes in the liver, kidney, spleen and gastro-intestinal system.” Na madhara haya yamejitokeza katika kila tafiti yenye kujitegemea kutoka kila kona ya ulimwengu.
(ii) Tafiti zetu Hazijitegemei kivipi?
Kwa taarifa, Co-ordinator au Mratibu wa utafiti unaofanywa huko Makutopora ni taasisi moja inayojulika kwa jina la AATF – African Agricultural Technology Foundation – makao makuu yake yapo Nairobi, nchini Kenya. Nani wanafadhili hii “Foundation”? Ni hawa hapa: Bill & Belinda Gates Foundation, Howard G. Buffet Foundation, The Rockefeller Foundation, UKAID, USAID, Feed: Future, Syngenta Foundation & PEPSICO.
Hawa wote wana maslahi makubwa kwenye ‘Bi0-tech Industry’; ushauri wao au misimamo yao haiwezi kujitegemea wala kuwa ya kujitolea kwenye suala la GMO; ushauri na misimamo yao itakuwa inatetea maslahi yao binafsi.
Na kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknoloji ya Tanzania (COSTECH) ya tarehe 06/11/2018, huu mradi wa ,Water Efficient Maize for Africa’ (WEMA) wa huko Makutopora, Dodoma, unafadhiliwa na wafuatao: Bill and Belinda Gates Foundation, Howard G.Buffet Foundation na Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Marekani (USAID) kupitia African Agricultural Technology Foundation (AATF).
Hivi, katika manzili (circumstances) kama hizi kweli tunawategemea hao wafanyakazi wa huko Makutopora waseme ukweli wa kuwa hiki kilimo cha GMO hakitufai?
Hii ‘scenario’, kwa maoni yangu, haina tofauti na ile ya mtu kujitungia mtihani mwenyewe, kujisimamia mwenyewe, kusahihisha mwenyewe na mwishoni kujitangazia matokeo. Inahuzunisha.
(b) Nadharia na Kweli ya Kilimo cha GMO.
Nadharia.
Dr. Ally kwenye andiko lake amerudia nadharia (theory) zinazotumiwa na “spin doctors” wanaonadi kilimo cha GMO. Mathalani, ameandika:
“… Idadi kubwa ya watu (ambayo inakadiriwa kufika bilioni 9.8 ifikapo mwaka 2050), inamaanisha maeneo ya kilimo yanapungua wakati uhitaji wa kuzalisha zaidi ili kulisha watu unaongezeka; hivyo unahitaji mbegu zinaweza kukupa mazao mengi kwenye eneo dogo.”
Ukweli ni Huu.
Ripoti ya Umoja wa Mataifa inayoitwa “Agriculture at a Crossroads” iliyochapishwa mwaka 2008 chini ya mwavuli (auspicies) wa International Assessment of Agricultural Knowledge, Science and Technology for Development (IAASTD) inajibu hiyo hoja ya Dr. Ally kwa undani.
Utafiti wa hii Ripoti ulichukua miaka minne na washiriki walikuwa ni wataalamu 900 kati yao wakiwepo wanasayansi wabobezi 400 kutoka nchi 110. Na wafadhili walikuwa ni Umoja wa Mataifa kupitia taasisi zake zifuatazo: Benki ya Dunia, UNDP, UNESCO, WHO, UNEP, Global Environmental Facility (GEF), Food & Agricultural Organization (FAO) na wengineo. Aidha makampuni ya Biotech yafuatayo nayo yalifadhili huo utafiti: Monsanto, Syngenta, BASF, Unilever, Crop Life International and Association of Global Agrichemical Companies.
Watafiti walipewa hadimu rejea ifuatayo:
“How can we reduce hunger and poverty, improve rural livelihoods and facilitate equitable, environmentally, socially, and economically sustainable development through the generation of, access to, and use of agricultural knowledge, science and technology? And crucially what role if any the controversial technique of genetic engineering should play in feeding the world’s hungry.”
Matokeo ya utafiti yanasema hivi:
“… Kilimo cha GMO hakina mchango wowote kwenye malengo ya kupunguza njaa na umaskini duniani, kuleta lishe bora, afya kwa wanavijiji au maendeleo endelevu ya jamii na mazingira. … Na mfumo unaopiga marufuku wakulima kuhifadhi mbegu utaua uhuru wa chakula wa mataifa.” Ripoti hiyo inaendelea kuuhimiza ulimwengu kujikita katika kilimo cha kikaboni (organic farming) na kuachana na kilimo hiki cha GMO.
Aidha, Dkt. H. Harren, Mwenyekiti Mwenza (Co-chair) wa hiyo Ripoti ya Umoja wa Mataifa – “Agriculture at a Crossroads” akijibu Waandishi wa Habari hoja iliyokaririwa na Dr. Ally hapo juu, alikuwa na haya ya kusema:
“… Kwa kweli sioni matumizi yoyote ya maana ya GMOs, hivi sasa au siku za usoni. Tunazalisha chakula cha kuweza kulisha kikamilifu watu bilioni 14, na hiyo ni zaidi ya chakula kitakachohitajika kulisha watu bilioni 9 ambao wanatarajiwa duniani ifikapo mwaka 2050.”
Huu ndio ukweli wa kilimo hiki cha GMO – hakina tija, si muhimu na hakihitajiki; siyo tu hapo nyumbani, bali Afrika na dunia nzima. Tafiti zote za kitaifa na kimataifa zilizokwishafanywa zenye kujitegemea (kwa maana ya kutofadhiliwa na makampuni ya bio-teknolojia) zote zinasema kama hii ripoti inavyosema.
Baada ya ripoti yenye hadhi ya upeo huu kutolewa, katika ulimwengu wa kawaida kilichotakiwa kufanyika ni Umoja wa Mataifa kupiga marufuku kabisa hiki kilimo duniani kote. Kwani haiswihi Umoja wa Mataifa kuwa na “Article” nambari 1 ya “Charter” yake inayohimiza suala liitwalo ‘self-determination of nations’ halafu iunge mkono kilimo ambacho utafiti wake yenyewe unasema kinaua uhuru wa mataifa, yaani inaua hiyo, “self-determination of nations.”
Mgawanyiko wa wadau kwenye Ripoti ya Umoja wa Mataifa.
Baada Ripoti ya Umoja wa Mataifa, Agriculture at a Crossroads kuchapishwa mwezi Aprili 2008 huko Johannesburg, Afrika ya Kusini, wadau waligawanyika katika makundi matatu.
Kundi la kwanza, lilikuwa ni la mataifa 58 ambayo yaliunga mkono na ku – “ratify” hii ripoti, ikiwa ni pamoja na Tanzania, Kenya na Uganda.
Kundi la pili, lilikuwa ni la yale makampuni ya bioteknolojia ambayo yalichangia huu utafiti. Hili kundi lilikataa kusaini au ku – “ratify” ripoti kwa sababu matokeo yalipiga vita maslahi yake.
Kundi la tatu, lilikuwa ni la mataifa mama ya haya makampuni ya GMO, yakiongozwa na Marekani, Kanada na Australia. Kundi hili nalo lilikataa kuunga mkono ripoti; lakini haya mataifa yalikiri kuwa pamoja na kutokusaini kwetu ripoti ni kuntu.
Maswali yanayolilia majibu kwa Afrika ya Mashariki ni haya: Baada ya kusaini hii “comprehensive Report” ya Umoja wa Mataifa dhidi ya kilimo cha GMO, kwa nini hizi nchi bado zinakumbatia hiki kilimo? Je, walikuwa hawajui nini wanasaini? Je, wamenunuliwa na makampuni ya GMO? Au je, wametiswa na mataifa mama ya makampuni haya?
Fauka ya hayo, je, viongozi wa Tanzania na Afrika Mashariki, wanafahamu kuwa: “Genetic Engineering Approval Committee (GEAC)” ya India, iliitahadharisha Serikali yake kuwa: “Bt cotton is not recommended for small farmers” Na GEAC ikapuuzwa? Viongozi wetu wanalifahamu hili?
Sasa hebu tuangalie uzoefu “experience” wa wakulima wadogo walioshurutiswa na serikali yao kukumbatia hiki kilimo cha uhandisi jeni huko India.
India: Maswali karibu hayo hayo ambayo yanaulizwa na wananchi wa Afrika Mashariki yanaweza kuulizwa na wananchi wa India. Mwaka 1970, India iliweka katika Katiba yake katazo la ku – “patent” mimea au “life form.” Lakini miaka ya 1990s Monsanto waliingia India na kuleta hizo sera zilizokatazwa kwenye Katiba ya nchi. Baada ya Monsanto kukamata soko la Bt Cotton kwa asilimia 90, wakulima walipandishiwa bei ya mbegu za hiyo pamba kwa asilimia alfu nane (8,000%).
Wakulima waliposhindwa kununua mbegu, wakawa wanakopeshwa kwa makubaliano ya kulipa baada ya mavuno. Lakini mchanganyiko wa uzorotaji wa ubora wa pamba ya GMO, uliosababisha kushuka kwa bei, pamoja na kuporomoka kwa mavuno kulikotokana na ardhi kuchujuka kwa sababu ya matumizi makubwa ya madawa ya kilimo yanayoendana na mbegu za GMO – kuliwafanya wakulima wadogo wa India washindwe kulipa madeni yao.
Uamuzi wa makampuni ya GMO ulikuwa ni kuwanyang’anya wakulima hao mashamba yao pamoja na mali zingine walizokuwa nazo. Baada ya kujikuta wamepoteza kila kitu ndipo kipupwe cha wakulima wadogo wa pamba za GMO kujiua wenyewe kilipopamba moto. Wakulima wadogo 300,000 walijiua wenyewe katika muhula wa miaka 20. Hivi sasa wakulima wadogo wa pamba walio wengi wameachana na kilimo cha Bt cotton kwa sababu hakina faida.
Mwaka 2018 ndipo Mahakama Kuu ya India ilipoingilia kati na kupiga marufuku ku – ‘patent’ mimea ikinukuu katazo lililopo kwenye Katiba yao tangu 1970. Aidha Mahakama ilifutilia mbali mfumo wa tozo za “royalty or technology surcharges” ambazo Monsanto ilikuwa inawatoza wakulima.
Maswali ambayo Wahindi nao wanajiuliza ni haya: Je, wakati Monsanto wanaingiza hiki kilimo cha kiharamia nchini, hii Katiba ya 1970 ilikuwa wapi? Kwa nini hiyo Mahakama Kuu, ilichelewa kuingilia kati kwa kiasi hiki? Je, Viongozi walinunuliwa, walilaghaiwa au walitishwa?
Kwa wananchi wa Afrika Mashariki swali linguine la kujiuliza ni hili: Iwapo Monsanto walipandisha bei ya Bt cotton kwa asilimia 8,000 huko India, kuna sababu gani ya kuamini kuwa Monsanto hawatatupandishia bei kwa asilimia hizo hapo Afrika Mashariki? Jamani, ndiyo, ubepari ni unyama, lakini unyama ulio kwenye kilimo cha GMO upo katika daraja la peke yake.
Nadharia.
Aidha Dr. Ally anaendelea kusema: “Kuna hoja kwamba GMO si salama kiafya, si sahihi kusema hivyo, maana GMO ni neno la pamoja, hivyo hatuwezi kuhukumu GMOs zote kwa kauli moja.”
Ukweli ni Huu.
Hii kauli ya kuwa hiki kilimo si salama haikutokea kijiweni. Imesemwa na wataalamu baada ya kujiridhisha kwa utafiti. Kwa mfano tafiti za kitaifa za nchi zifuatazo zilithibitisha kuwa GMO si salama: Uingereza, Ufaransa, Austria na Urusi. Na hiyo Ripoti ya Umoja wa Mataifa yenye kurejewa hapo juu, inasema hivyo hivyo.
Pia kutokuwa na usalama kwa GMO kumejitokeza kwenye ‘documents’ 44,000 za siri za Food and Drug Administration (FDA) ambazo zilifunguliwa baada ya hukumu ya Mahakama huko Marekani. Kwenye hizo ‘documents’, wanasayansi wa FDA, yaani wanasayansi wa serikali wanaongelea ukosefu wa usalama wa GMO. Sasa Dr. Ally anaikana hii kauli kwa utafiti upi?
‘Public interest lawyer’, Steven M. Druker, aliyekabidhiwa hizo ‘documents’ 44,000 na Mahakama, baada ya kuzisoma ameandika kitabu kiitwacho:
Altered Genes, Twisted Truth – (How the Venture to Genetically Engineer Our Foods Has Subverted Science, Corrupted Government, and Systematically Deceived the Public).
Na Jeffrey M. Smith, mwandishi wa kitabu cha (Seeds of Deception & Genetic Roulette) kwenye “review” yake ya Altered Genes, Twisted Truth, aliandika hivi:
Nadharia.
Andiko la Dr. Ally linaendelea kusema:
“Utafiti uliofanywa na watafiti kutoka Shule Kuu Ya Biashara (UDBS) hapa Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam na wadau wengine kama COSTECH (2011), unaonesha kwamba, kama Tanzania ingeanza kulima mahindi ya GMO yanayostahimili ukame na wadudu kuanzia 2016 na miaka sita baadae, basi ingeongeza thamani ya uzalishaji wa zao hilo kwa zaidi ya shilingi za kitanzania trilioni 1.7.”
Ukweli ni Huu.
Utafiti huo si sahihi. Hayo mahindi “yanayostahimili” ukame yamelimwa Afrika ya Kusini kwa muda wa miaka 15, yalisababisha mlipuko wa “super weeds na super bugs” uliofanya kilimo kisiwe na faida na hatimaye kampuni ya Monsanto iliyopeleka hizo mbegu huko, kulipa fidia wakulima wa nchi hiyo kimya kimya. Hivyo basi, matokeo ya hizi tafiti zetu ni za kuzipokea kwa tahadhari kubwa sana.
Jambo la kushangaza ni kwamba kwa mara ya kwanza, Monsanto imejitolea kulipa faida waathirika wake bila kwenda mahakamani. Lakini haishangazi sana; kwa sababu hayo mahindi yenye kuleta hasara Afrika Kusini ndio yaliyosukumiwa Tanzania, Kenya, Uganda na Msumbiji, kwa ahadi ya kutozitoza hizo nchi “royalty”. Sasa kama kungalikuwa na “full-blown court case” juu ya hasara na madhara ya hizo mbegu, hizi nchi zisingeliingia mkenge wa kuzipokea. Marejeo yafanywe kwenye Makala haya: “Failed Monsanto GMO corn Pushed on African Countries with Help of Bill Gates.”
Dr. Ally pia anahoji kauli inayohusu utegemezi ya Waziri wa Kilimo, Mheshimiwa Hussein Bashe, kauli ambayo yamkini haina utata wowote.
Utegemezi unaoongelewa haupo kwenye hizo mbegu zinatoka wapi (nje au ndani ya nchi) utegemezi upo kwenye tabia (characteristic) ya mbegu zenyewe.
Mbegu za asili popote zitakapotoka, ukipanda, mavuno yake unaweza kutumia kama mbegu za kupanda msimu au mwaka unaofuata. Lakini mbegu za GMO popote zitakapotoka, mavuno yake hayawezi kutumiwa kama mbegu, msimu unaokuja – ukipanda mavuno ya GMO hayaoti; ndiyo kusema wakulima wanategemezwa kwa wauza mbegu milele; yaani kunafutwa kujitegemea kwa wakulima. Hilo si suala jepesi.
Utafiti uliofanywa kwa muhula wa miaka 14 wa Chuo Kikuu cha Wisconsin-Madison, uliolenga wakulima wa mahindi wa Wisconsin, Minnesota, Illinois, Iowa na Nebraska ulionyesha kuwa kilimo ambacho siyo cha GMO kina tija zaidi, na ile hali ya kuwa wakulima wasio wa uhandisi jeni hawakulazimika kununua mbegu kila msimu ndio uliofanya faida ipatikane.
Mwaka 2008 Ripoti ya utafiti wa “Organic Agriculture and Food Security in Africa ambayo ilifadhiliwa na United Nations Conference on Trade and Development (UNCTAD) kwa kushirikiana na United Nations Environment Programme (UNEP) ulionyesha kuwa miradi yote ambayo ilihama kutoka kwenye kilimo cha GM na kurudi katika kilimo cha kikaboni “Organic farming” iliongeza mavuno yao. Pia, Ripoti hiyo ilisisitiza kuwa kilimo cha kikaboni (organic) kinaleta lishe (nutrition) bora katika jamii. Hapa napo kutokuwepo kwa utegemezi katika kupata mbegu nako kulichangia kuleta haya matokeo.
Hivyo basi, kauli ya Mh. Bashe kwenye hili, haina dosari, ni kweli tupu.
“Confined field trials” ni kiini macho.
Dhana ya ‘confined field trials’ ni kiini macho, kwani mmea ukishipandwa sehemu ya wazi shambani, hakuna njia ya kuu – “confine” huo mmea; kwa sababu “cross pollination” kupitia upepo, ndege na wadudu haijapata kuwa “confined.”
Na hii “cross pollination” ndio inayofanya uthibiti wa uhakika wa madhara ya kilimo cha GMO ni kukipiga marufuku kabisa, kwani aina hii mbili ya kilimo (GMO and Non-GMO) haviwezi kudumu bega kwa bega – (cannot co-exist).
Mwisho wa andiko lake, Dr. Ally ameandika hivi:
“Hivyo maamuzi haya yanapaswa kufanywa na wataalamu kutoka wizara husika (mfano afya, uvuvi na kilimo) wataalamu hao ndio wanajua zaidi ni wapi wanahitaji nguvu/teknolojia ya ziada (GMOs) kwa maana zile njia za kitaalamu za asili zimeshindwa kutatua changamoto husika.”
HITIMISHO.
Kurejesha kilimo cha uhandisi jeni (GMO) nchini Tanzania ni kuteleza kwa upeo wa juu. Faida nyingi zinazoelezwa za kilimo hiki hazina uhalisia lakini hatari zake zote ni za kweli. Kila walikokijaribu kilimo hiki matokeo yamekuwa si murua – ni vilio: India, Afrika ya Kusini, Burkina Faso, Mexico, United States of America. Na 2018 Burkina Faso imepiga marufuku hiki kilimo kilichokumbatiwa kwa mbwembwe zote 2003.
Watu wanaopigia chapuo kilimo cha uhandisi jeni, wawe ni wanasiasa, watumishi wa serikali (civil servants) au wasomi kwenye vyuo na taasisi mbalimbali -waangaliwe kwa macho mawili: watakuwa aidha hajui wanachokishabikia au wanafanya makusudi. Watatuponza hawa.
Marufuku iliyopitishwa Tanzania tarehe 22/11/2018 dhidi ya kilimo cha uhandisi jeni ni ya kuzingazitiwakwa juhudi zote. Inalinda maslahi mapana ya Tanzania na Watanzania. Ni marufuku ya kishujaa na kizalendo. Idumishwe.
Kufuta hilo katazo, ni kufuta uhuru wetu wa chakula na kuvuruga afya zetu pamoja na za mazingira yetu. Watu waliolambishwa asali hawataweza kuyasema haya ingawa wanayaona.
Hapa chini ni documentary iliyoelezea madhara ya kilimo cha GMO kwa kina:
“Seeds of Death: Unveiling The Lies of GMO’s Full Documentary HD
Kizazi kiovu baadae walichanganya mbegu za wanyama tofauti wakatoa viumbe wa ajabu kina Godzila ,Mungu kupitia Gharika akawaharibu, Kuna watu leo walikuwa wanabisha haiwezekani kuchanganya mbegu ya kiumbe tofauti na Mwingine ukatoa kiumbe tofauti, Lakini Zamani walifanya, na leo wanadamu wamefikia huko
Tusome Hapa, pia usipoelewa pitia Tafsiri mbalimbali , Humo makanisani hao wanaojiita manabii na wachungaji wakisoma hi mistari wanatafsiri kana kwamba Mungu alizuia kupanda shamba moja mahindi na maharage , Lakini maana halisi Ni kuchukua Mbegu ya kiumbe A ukafanya kuunganisha na mbegu B, Kisha upate KIUMBE MMOJA.
Tusome ...
Kumbukumbu la Torati 22:9 SRUV
Usipande shamba lako la mizabibu aina mbili za mbegu; yasije yakaondolewa matunda yote, mbegu ulizopanda na mavuno ya mizabibu yako.Mambo ya Walawi 19:19 SRUV
Mtazishika amri zangu. Usiwaache wanyama wako wa mfugo wakazaana kwa namna mbalimbali; usipande shamba lako mbegu za namna mbili pamoja;KENYA WAMERUHUSU GMO, Sasa wanazalisha Maparachichi yasiyo na mbegu Kama haya
Tanzania isionje sumu ya GMO kwa kukijaribu kilimo hiki. India walifanya hili kosa na matokeo yalikuwa ni wakulima wadogo laki tatu (300,000) kujiua wenyewe katika muhula wa miaka 20. Hatima kama hii tuiepuke hapo nyumbani kwa udi na uvumba.
# Vinasaba vya epicyte ambavyo vipo kwenye baadhi ya mazao ya vyakula vya GMO (Genetically Modified Organism) kupitia mbegu zake vitazuia ongezeko la watu duniani, kwa sababu kazi ya hiki kinsaba ni kuwafanya wanaume na wanawake wasizae milele -ingawa tendo la ndoa litafanyika kama kawaida. Na kwa kutumia teknolojia inayoitwa “RNA crop interference technology” wame – “fine-tune” huo uhanithi na ugumba uliowekwa kwenye hiki kinsaba cha epicyte uwaathiri Watu Weusi peke yao. Yes, “…GMO food crops have now been fine-tuned to cause irreversible infertility in black people alone.”
# Kupitia lobbyists waliowekwa kwenye idara zao ziitwazo “Political Action Committees (PACs) makampuni mara nyingi huwa yanaweka mifukoni wasomi pamoja na baadhi ya viongozi wa kitaifa ili kuthibiti, hata kupotosha mataifa lengwa. Nchi yetu iwe macho sana na njama za sampuli hii.
Siku ya Alhamisi ya tarehe 6/10/2022 Dr. Ally, kwenye mtandao wa “Uwanja wa Diplomasia” alichapisha andiko lenye kichwa cha habari kifuatacho: ‘GMO, NDIO AU HAPANA KWA TANZANIA’.
Kwa mujibu wa matokeo ya tafiti za kitaifa na kimataifa, pamoja na uzoefu (real life experiences) ya watu wanaoishi na kilimo hiki ni vema: “GMO iwe Hapana kwa Tanzania.”
Hili andiko la Dr. Ally nimelisoma kwa kina. Katika kutoa tafsiri za GMO na misamiati mingine ya bayolojia andiko lake limekaa vizuri; lilipopwaya ni katika kujibu hofu za watu kuhusu faida na hasara za kilimo cha uhandisi jeni.
- Watu wanasema kwamba tafiti baada ya tafiti zimefanywa na taasisi kadha wa kadha zinazozijitegemea (yaani ambazo hazipokei fedha kutoka kwa ‘bio-tech industry’) na zote zimejiridhisha kuwa hiki kilimo hakifai na hatarishi kwa afya za watu na mazingira pia kinafuta uhuru wa chakula wa mataifa (national food sovereignty), hivyo basi hakihitajiki. Katika tafiti iliyokuwa kubwa kupita zote, yenye kutoa hayo matokeo ni ile ya Umoja wa Mataifa – Agriculture at a Crossroads” – ambayo nchi za Tanzania, Kenya na Uganda ziliidhinisha (ratified it).
ILI KULINDA AFYA ZA WATANZANIA NA MAZINGIRA PAMOJA NA UHURU WA TAIFA WA CHAKULA, “KILIMO CHA GMO KIWE NI MARUFUKU TANZANIA.”
Swali la msingi ni hili: Kwa nini taasisi zetu za taifa za utafiti za Tanzania, Kenya na Uganda zinapoteza fedha na wakati kutafiti jambo ambalo limekwisha fanyiwa utafiti “exhaustively” na Umoja wa Mataifa na matokeo yake yapo wazi? Hii, si sawa na kusema baada ya huu utafiti wa Umoja wa Mataifa watu wasitishe tafiti katika fani ya kilimo. La hasha. “Public crop-breeding programmes” ambazo hazirudishi mataifa kwenye utumwa-mamboleo ziendelee, tumekuwa nazo tangu kilimo kiwepo duniani miaka zaidi ya 10,000 iliyopita. Lakini kwa nini tunang’ang’ania GMO ambayo imethibitika: (i) Ina kila aina ya madhara na (ii) Hizo tafiti zetu zenyewe wala hazijitegemei?
(i) Madhara: “In 2009 the American Academy of Environmental Medicine called for a moratorium of GM foods, safety testing and labelling. Their review of the available literature at the time noted that animal studies show serious health risks associated with GMO food consumption including infertility, immune dysregulation, accelerated aging, dysregulation of genes associated with cholesterol synthesis, cell signalling and protein formation, and changes in the liver, kidney, spleen and gastro-intestinal system.” Na madhara haya yamejitokeza katika kila tafiti yenye kujitegemea kutoka kila kona ya ulimwengu.
(ii) Tafiti zetu Hazijitegemei kivipi?
Kwa taarifa, Co-ordinator au Mratibu wa utafiti unaofanywa huko Makutopora ni taasisi moja inayojulika kwa jina la AATF – African Agricultural Technology Foundation – makao makuu yake yapo Nairobi, nchini Kenya. Nani wanafadhili hii “Foundation”? Ni hawa hapa: Bill & Belinda Gates Foundation, Howard G. Buffet Foundation, The Rockefeller Foundation, UKAID, USAID, Feed: Future, Syngenta Foundation & PEPSICO.
Hawa wote wana maslahi makubwa kwenye ‘Bi0-tech Industry’; ushauri wao au misimamo yao haiwezi kujitegemea wala kuwa ya kujitolea kwenye suala la GMO; ushauri na misimamo yao itakuwa inatetea maslahi yao binafsi.
Na kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknoloji ya Tanzania (COSTECH) ya tarehe 06/11/2018, huu mradi wa ,Water Efficient Maize for Africa’ (WEMA) wa huko Makutopora, Dodoma, unafadhiliwa na wafuatao: Bill and Belinda Gates Foundation, Howard G.Buffet Foundation na Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Marekani (USAID) kupitia African Agricultural Technology Foundation (AATF).
Hivi, katika manzili (circumstances) kama hizi kweli tunawategemea hao wafanyakazi wa huko Makutopora waseme ukweli wa kuwa hiki kilimo cha GMO hakitufai?
Hii ‘scenario’, kwa maoni yangu, haina tofauti na ile ya mtu kujitungia mtihani mwenyewe, kujisimamia mwenyewe, kusahihisha mwenyewe na mwishoni kujitangazia matokeo. Inahuzunisha.
(b) Nadharia na Kweli ya Kilimo cha GMO.
Nadharia.
Dr. Ally kwenye andiko lake amerudia nadharia (theory) zinazotumiwa na “spin doctors” wanaonadi kilimo cha GMO. Mathalani, ameandika:
“… Idadi kubwa ya watu (ambayo inakadiriwa kufika bilioni 9.8 ifikapo mwaka 2050), inamaanisha maeneo ya kilimo yanapungua wakati uhitaji wa kuzalisha zaidi ili kulisha watu unaongezeka; hivyo unahitaji mbegu zinaweza kukupa mazao mengi kwenye eneo dogo.”
Ukweli ni Huu.
Ripoti ya Umoja wa Mataifa inayoitwa “Agriculture at a Crossroads” iliyochapishwa mwaka 2008 chini ya mwavuli (auspicies) wa International Assessment of Agricultural Knowledge, Science and Technology for Development (IAASTD) inajibu hiyo hoja ya Dr. Ally kwa undani.
Utafiti wa hii Ripoti ulichukua miaka minne na washiriki walikuwa ni wataalamu 900 kati yao wakiwepo wanasayansi wabobezi 400 kutoka nchi 110. Na wafadhili walikuwa ni Umoja wa Mataifa kupitia taasisi zake zifuatazo: Benki ya Dunia, UNDP, UNESCO, WHO, UNEP, Global Environmental Facility (GEF), Food & Agricultural Organization (FAO) na wengineo. Aidha makampuni ya Biotech yafuatayo nayo yalifadhili huo utafiti: Monsanto, Syngenta, BASF, Unilever, Crop Life International and Association of Global Agrichemical Companies.
Watafiti walipewa hadimu rejea ifuatayo:
“How can we reduce hunger and poverty, improve rural livelihoods and facilitate equitable, environmentally, socially, and economically sustainable development through the generation of, access to, and use of agricultural knowledge, science and technology? And crucially what role if any the controversial technique of genetic engineering should play in feeding the world’s hungry.”
Matokeo ya utafiti yanasema hivi:
“… Kilimo cha GMO hakina mchango wowote kwenye malengo ya kupunguza njaa na umaskini duniani, kuleta lishe bora, afya kwa wanavijiji au maendeleo endelevu ya jamii na mazingira. … Na mfumo unaopiga marufuku wakulima kuhifadhi mbegu utaua uhuru wa chakula wa mataifa.” Ripoti hiyo inaendelea kuuhimiza ulimwengu kujikita katika kilimo cha kikaboni (organic farming) na kuachana na kilimo hiki cha GMO.
Aidha, Dkt. H. Harren, Mwenyekiti Mwenza (Co-chair) wa hiyo Ripoti ya Umoja wa Mataifa – “Agriculture at a Crossroads” akijibu Waandishi wa Habari hoja iliyokaririwa na Dr. Ally hapo juu, alikuwa na haya ya kusema:
“… Kwa kweli sioni matumizi yoyote ya maana ya GMOs, hivi sasa au siku za usoni. Tunazalisha chakula cha kuweza kulisha kikamilifu watu bilioni 14, na hiyo ni zaidi ya chakula kitakachohitajika kulisha watu bilioni 9 ambao wanatarajiwa duniani ifikapo mwaka 2050.”
Huu ndio ukweli wa kilimo hiki cha GMO – hakina tija, si muhimu na hakihitajiki; siyo tu hapo nyumbani, bali Afrika na dunia nzima. Tafiti zote za kitaifa na kimataifa zilizokwishafanywa zenye kujitegemea (kwa maana ya kutofadhiliwa na makampuni ya bio-teknolojia) zote zinasema kama hii ripoti inavyosema.
Baada ya ripoti yenye hadhi ya upeo huu kutolewa, katika ulimwengu wa kawaida kilichotakiwa kufanyika ni Umoja wa Mataifa kupiga marufuku kabisa hiki kilimo duniani kote. Kwani haiswihi Umoja wa Mataifa kuwa na “Article” nambari 1 ya “Charter” yake inayohimiza suala liitwalo ‘self-determination of nations’ halafu iunge mkono kilimo ambacho utafiti wake yenyewe unasema kinaua uhuru wa mataifa, yaani inaua hiyo, “self-determination of nations.”
Mgawanyiko wa wadau kwenye Ripoti ya Umoja wa Mataifa.
Baada Ripoti ya Umoja wa Mataifa, Agriculture at a Crossroads kuchapishwa mwezi Aprili 2008 huko Johannesburg, Afrika ya Kusini, wadau waligawanyika katika makundi matatu.
Kundi la kwanza, lilikuwa ni la mataifa 58 ambayo yaliunga mkono na ku – “ratify” hii ripoti, ikiwa ni pamoja na Tanzania, Kenya na Uganda.
Kundi la pili, lilikuwa ni la yale makampuni ya bioteknolojia ambayo yalichangia huu utafiti. Hili kundi lilikataa kusaini au ku – “ratify” ripoti kwa sababu matokeo yalipiga vita maslahi yake.
Kundi la tatu, lilikuwa ni la mataifa mama ya haya makampuni ya GMO, yakiongozwa na Marekani, Kanada na Australia. Kundi hili nalo lilikataa kuunga mkono ripoti; lakini haya mataifa yalikiri kuwa pamoja na kutokusaini kwetu ripoti ni kuntu.
Maswali yanayolilia majibu kwa Afrika ya Mashariki ni haya: Baada ya kusaini hii “comprehensive Report” ya Umoja wa Mataifa dhidi ya kilimo cha GMO, kwa nini hizi nchi bado zinakumbatia hiki kilimo? Je, walikuwa hawajui nini wanasaini? Je, wamenunuliwa na makampuni ya GMO? Au je, wametiswa na mataifa mama ya makampuni haya?
Fauka ya hayo, je, viongozi wa Tanzania na Afrika Mashariki, wanafahamu kuwa: “Genetic Engineering Approval Committee (GEAC)” ya India, iliitahadharisha Serikali yake kuwa: “Bt cotton is not recommended for small farmers” Na GEAC ikapuuzwa? Viongozi wetu wanalifahamu hili?
Sasa hebu tuangalie uzoefu “experience” wa wakulima wadogo walioshurutiswa na serikali yao kukumbatia hiki kilimo cha uhandisi jeni huko India.
India: Maswali karibu hayo hayo ambayo yanaulizwa na wananchi wa Afrika Mashariki yanaweza kuulizwa na wananchi wa India. Mwaka 1970, India iliweka katika Katiba yake katazo la ku – “patent” mimea au “life form.” Lakini miaka ya 1990s Monsanto waliingia India na kuleta hizo sera zilizokatazwa kwenye Katiba ya nchi. Baada ya Monsanto kukamata soko la Bt Cotton kwa asilimia 90, wakulima walipandishiwa bei ya mbegu za hiyo pamba kwa asilimia alfu nane (8,000%).
Wakulima waliposhindwa kununua mbegu, wakawa wanakopeshwa kwa makubaliano ya kulipa baada ya mavuno. Lakini mchanganyiko wa uzorotaji wa ubora wa pamba ya GMO, uliosababisha kushuka kwa bei, pamoja na kuporomoka kwa mavuno kulikotokana na ardhi kuchujuka kwa sababu ya matumizi makubwa ya madawa ya kilimo yanayoendana na mbegu za GMO – kuliwafanya wakulima wadogo wa India washindwe kulipa madeni yao.
Uamuzi wa makampuni ya GMO ulikuwa ni kuwanyang’anya wakulima hao mashamba yao pamoja na mali zingine walizokuwa nazo. Baada ya kujikuta wamepoteza kila kitu ndipo kipupwe cha wakulima wadogo wa pamba za GMO kujiua wenyewe kilipopamba moto. Wakulima wadogo 300,000 walijiua wenyewe katika muhula wa miaka 20. Hivi sasa wakulima wadogo wa pamba walio wengi wameachana na kilimo cha Bt cotton kwa sababu hakina faida.
Mwaka 2018 ndipo Mahakama Kuu ya India ilipoingilia kati na kupiga marufuku ku – ‘patent’ mimea ikinukuu katazo lililopo kwenye Katiba yao tangu 1970. Aidha Mahakama ilifutilia mbali mfumo wa tozo za “royalty or technology surcharges” ambazo Monsanto ilikuwa inawatoza wakulima.
Maswali ambayo Wahindi nao wanajiuliza ni haya: Je, wakati Monsanto wanaingiza hiki kilimo cha kiharamia nchini, hii Katiba ya 1970 ilikuwa wapi? Kwa nini hiyo Mahakama Kuu, ilichelewa kuingilia kati kwa kiasi hiki? Je, Viongozi walinunuliwa, walilaghaiwa au walitishwa?
Kwa wananchi wa Afrika Mashariki swali linguine la kujiuliza ni hili: Iwapo Monsanto walipandisha bei ya Bt cotton kwa asilimia 8,000 huko India, kuna sababu gani ya kuamini kuwa Monsanto hawatatupandishia bei kwa asilimia hizo hapo Afrika Mashariki? Jamani, ndiyo, ubepari ni unyama, lakini unyama ulio kwenye kilimo cha GMO upo katika daraja la peke yake.
Nadharia.
Aidha Dr. Ally anaendelea kusema: “Kuna hoja kwamba GMO si salama kiafya, si sahihi kusema hivyo, maana GMO ni neno la pamoja, hivyo hatuwezi kuhukumu GMOs zote kwa kauli moja.”
Ukweli ni Huu.
Hii kauli ya kuwa hiki kilimo si salama haikutokea kijiweni. Imesemwa na wataalamu baada ya kujiridhisha kwa utafiti. Kwa mfano tafiti za kitaifa za nchi zifuatazo zilithibitisha kuwa GMO si salama: Uingereza, Ufaransa, Austria na Urusi. Na hiyo Ripoti ya Umoja wa Mataifa yenye kurejewa hapo juu, inasema hivyo hivyo.
Pia kutokuwa na usalama kwa GMO kumejitokeza kwenye ‘documents’ 44,000 za siri za Food and Drug Administration (FDA) ambazo zilifunguliwa baada ya hukumu ya Mahakama huko Marekani. Kwenye hizo ‘documents’, wanasayansi wa FDA, yaani wanasayansi wa serikali wanaongelea ukosefu wa usalama wa GMO. Sasa Dr. Ally anaikana hii kauli kwa utafiti upi?
‘Public interest lawyer’, Steven M. Druker, aliyekabidhiwa hizo ‘documents’ 44,000 na Mahakama, baada ya kuzisoma ameandika kitabu kiitwacho:
Altered Genes, Twisted Truth – (How the Venture to Genetically Engineer Our Foods Has Subverted Science, Corrupted Government, and Systematically Deceived the Public).
Na Jeffrey M. Smith, mwandishi wa kitabu cha (Seeds of Deception & Genetic Roulette) kwenye “review” yake ya Altered Genes, Twisted Truth, aliandika hivi:
“Drukers’s brilliant expose catches the promoters of GE food red-handed: falsifying data, corrupting regulators, lying to Congress. He thoroughly demonstrates how distortions and deceptions have been piled one on top of another, year after year, producing a global industry that teeters on a foundation of fraud and denial.”
Nadharia.
Andiko la Dr. Ally linaendelea kusema:
“Utafiti uliofanywa na watafiti kutoka Shule Kuu Ya Biashara (UDBS) hapa Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam na wadau wengine kama COSTECH (2011), unaonesha kwamba, kama Tanzania ingeanza kulima mahindi ya GMO yanayostahimili ukame na wadudu kuanzia 2016 na miaka sita baadae, basi ingeongeza thamani ya uzalishaji wa zao hilo kwa zaidi ya shilingi za kitanzania trilioni 1.7.”
Ukweli ni Huu.
Utafiti huo si sahihi. Hayo mahindi “yanayostahimili” ukame yamelimwa Afrika ya Kusini kwa muda wa miaka 15, yalisababisha mlipuko wa “super weeds na super bugs” uliofanya kilimo kisiwe na faida na hatimaye kampuni ya Monsanto iliyopeleka hizo mbegu huko, kulipa fidia wakulima wa nchi hiyo kimya kimya. Hivyo basi, matokeo ya hizi tafiti zetu ni za kuzipokea kwa tahadhari kubwa sana.
Jambo la kushangaza ni kwamba kwa mara ya kwanza, Monsanto imejitolea kulipa faida waathirika wake bila kwenda mahakamani. Lakini haishangazi sana; kwa sababu hayo mahindi yenye kuleta hasara Afrika Kusini ndio yaliyosukumiwa Tanzania, Kenya, Uganda na Msumbiji, kwa ahadi ya kutozitoza hizo nchi “royalty”. Sasa kama kungalikuwa na “full-blown court case” juu ya hasara na madhara ya hizo mbegu, hizi nchi zisingeliingia mkenge wa kuzipokea. Marejeo yafanywe kwenye Makala haya: “Failed Monsanto GMO corn Pushed on African Countries with Help of Bill Gates.”
MH. BASHE YUPO SAHIHI, MBEGU ZA GMO ZINAJENGA UTEGEMEZI.
Dr. Ally pia anahoji kauli inayohusu utegemezi ya Waziri wa Kilimo, Mheshimiwa Hussein Bashe, kauli ambayo yamkini haina utata wowote.
Utegemezi unaoongelewa haupo kwenye hizo mbegu zinatoka wapi (nje au ndani ya nchi) utegemezi upo kwenye tabia (characteristic) ya mbegu zenyewe.
Mbegu za asili popote zitakapotoka, ukipanda, mavuno yake unaweza kutumia kama mbegu za kupanda msimu au mwaka unaofuata. Lakini mbegu za GMO popote zitakapotoka, mavuno yake hayawezi kutumiwa kama mbegu, msimu unaokuja – ukipanda mavuno ya GMO hayaoti; ndiyo kusema wakulima wanategemezwa kwa wauza mbegu milele; yaani kunafutwa kujitegemea kwa wakulima. Hilo si suala jepesi.
Utafiti uliofanywa kwa muhula wa miaka 14 wa Chuo Kikuu cha Wisconsin-Madison, uliolenga wakulima wa mahindi wa Wisconsin, Minnesota, Illinois, Iowa na Nebraska ulionyesha kuwa kilimo ambacho siyo cha GMO kina tija zaidi, na ile hali ya kuwa wakulima wasio wa uhandisi jeni hawakulazimika kununua mbegu kila msimu ndio uliofanya faida ipatikane.
Mwaka 2008 Ripoti ya utafiti wa “Organic Agriculture and Food Security in Africa ambayo ilifadhiliwa na United Nations Conference on Trade and Development (UNCTAD) kwa kushirikiana na United Nations Environment Programme (UNEP) ulionyesha kuwa miradi yote ambayo ilihama kutoka kwenye kilimo cha GM na kurudi katika kilimo cha kikaboni “Organic farming” iliongeza mavuno yao. Pia, Ripoti hiyo ilisisitiza kuwa kilimo cha kikaboni (organic) kinaleta lishe (nutrition) bora katika jamii. Hapa napo kutokuwepo kwa utegemezi katika kupata mbegu nako kulichangia kuleta haya matokeo.
Hivyo basi, kauli ya Mh. Bashe kwenye hili, haina dosari, ni kweli tupu.
“Confined field trials” ni kiini macho.
Dhana ya ‘confined field trials’ ni kiini macho, kwani mmea ukishipandwa sehemu ya wazi shambani, hakuna njia ya kuu – “confine” huo mmea; kwa sababu “cross pollination” kupitia upepo, ndege na wadudu haijapata kuwa “confined.”
Na hii “cross pollination” ndio inayofanya uthibiti wa uhakika wa madhara ya kilimo cha GMO ni kukipiga marufuku kabisa, kwani aina hii mbili ya kilimo (GMO and Non-GMO) haviwezi kudumu bega kwa bega – (cannot co-exist).
Mwisho wa andiko lake, Dr. Ally ameandika hivi:
“Hivyo maamuzi haya yanapaswa kufanywa na wataalamu kutoka wizara husika (mfano afya, uvuvi na kilimo) wataalamu hao ndio wanajua zaidi ni wapi wanahitaji nguvu/teknolojia ya ziada (GMOs) kwa maana zile njia za kitaalamu za asili zimeshindwa kutatua changamoto husika.”
- Tatizo ni kwamba mara nyingi baadhi ya hao wataalamu ndio wanaowekwa kwenye mifuko ya nyuma ya haya makampuni ya bioteknolojia na kuishia kutoa ushauri ambao haunufaishi umma bali haya makampuni.
- Hapo juu nimelezea tafiti zilizoonyesha kuwa kilimo cha asili kina -“out- perform” hicho cha GMO. Mifano mingine ya hii kweli ni hii hapa chini.
“A 2008 United Nations report looked at 114 farming projects in 24 African countries and found that adoption of organic or near-organic practices resulted in yield increases averaging over 100%. In East Africa, a yield increase of 128% was found.”
Moreover, a 2001 review of 200 developing country agricultural projects involving a switch to agroecological techniques, conducted by University of Essex researchers, found an average of yield gain of 93 per cent.
HITIMISHO.
Kurejesha kilimo cha uhandisi jeni (GMO) nchini Tanzania ni kuteleza kwa upeo wa juu. Faida nyingi zinazoelezwa za kilimo hiki hazina uhalisia lakini hatari zake zote ni za kweli. Kila walikokijaribu kilimo hiki matokeo yamekuwa si murua – ni vilio: India, Afrika ya Kusini, Burkina Faso, Mexico, United States of America. Na 2018 Burkina Faso imepiga marufuku hiki kilimo kilichokumbatiwa kwa mbwembwe zote 2003.
Watu wanaopigia chapuo kilimo cha uhandisi jeni, wawe ni wanasiasa, watumishi wa serikali (civil servants) au wasomi kwenye vyuo na taasisi mbalimbali -waangaliwe kwa macho mawili: watakuwa aidha hajui wanachokishabikia au wanafanya makusudi. Watatuponza hawa.
Marufuku iliyopitishwa Tanzania tarehe 22/11/2018 dhidi ya kilimo cha uhandisi jeni ni ya kuzingazitiwakwa juhudi zote. Inalinda maslahi mapana ya Tanzania na Watanzania. Ni marufuku ya kishujaa na kizalendo. Idumishwe.
Kufuta hilo katazo, ni kufuta uhuru wetu wa chakula na kuvuruga afya zetu pamoja na za mazingira yetu. Watu waliolambishwa asali hawataweza kuyasema haya ingawa wanayaona.
Hapa chini ni documentary iliyoelezea madhara ya kilimo cha GMO kwa kina:
“Seeds of Death: Unveiling The Lies of GMO’s Full Documentary HD