Mume wangu ni mlevi sana

Mume wangu ni mlevi sana

Mtu mzima ashauriki haswa kwenye maswala ya starehe kama pombe. Akichooka atatubu na kuacha mwenyewe, avumilie tu. Adhabu nzuri ya kumpa ni kumzidishia upendo, lakini akimfuatafuata atamzidishia machungu.
 
Hapo kazi kumtenganisha mlevi na chupa ni ngumu sana
 
"If you want to change the world you must change you first". Mwambie huyo "shosti" tatizo la mumewe linaanzia kwake, Ima moja kwa moja au "indirect". Mwambie aanze kubadirika yeye kwanza mume atabadilika baadae. Mchunguze na yeye aajichunguze.
 
Kuna baadhi ya nyakati na katika baadhi ya mazingira huwa nafikiria ya kwamba kumpuuzia mtu ni suluhisho zuri zaidi. Itamfanya aanze kujenga attension kwako na atatamani kujua kwa nini humsumbui wala kumuuliza siku hizi. Jaribu hilo ila kwa tahadhari kubwa.
 
Hapo kuna tatizo mwambie mwanamke ajichunguze!kama mwanzo hakuwa mlevi ameanza ghafla lazima kuna kitu kuna matatizo anakunywa asifikirie!Ni hayo tu kwa sasa!Namshauri aketi aongee nae siku akiwa sober na asimpe lawama nyingi amsikilize mumewe!
 
Habari zenu wana jamii form, mimi ni mgeni umu ndani naombeni ushirikiani wenu
Nnarafiki yangu ameolewa na anawatoto watatu, tatizo lake mumewake amekua mlevi sana kiasi kwamba hata akitoka kazini anapitia bar anarudi nyumbani akiwa amelewa, siku za weekiend ndio kabisaa anarudi saakumi za usiku wakati mwingine saa kuminambili za asubuhi, akimuuliza anamjibkwadharau nakumwambia yeye hatakaa abadilike iyo ndo tabia yake, nakama anaona awezi aondoke, jamani uyu rafiki yangu amechanganyikiwa ajui afanyaje naombeni mumsaidie uyu rafiki yangu jamani.


Mume wa rafiki yako au wako? Kwanza kuwa mkweli ndio tukupe msaada
 
Mithali 31 mstari wa sita na saba unasema mpe kilevi yeye aliye karibu na kupotea pamoja na maskin anywe asahau shida zake.
 
Mimi naamini tabia ya mtu haiwezi tu kubadilika tu ghafla lazima tu kuna sababu...pengine huyo rafiki yako ndio sababu ya mumewe kutumbukia kwenye ulevi....maana muda mwingine wanawake huwa na maudhi sana..na mtu anaona hakuna njia nyingine zaidi ya kulewa....jaribu kukaa na rafiki yako na akueleze kwa kina naaamini kuna mambo kibao tu amekuficha kwa sababu ya kero ya ulevi wa mumewe..
 
Mimi naamini tabia ya mtu haiwezi tu kubadilika tu ghafla lazima tu kuna sababu...pengine huyo rafiki yako ndio sababu ya mumewe kutumbukia kwenye ulevi....maana muda mwingine wanawake huwa na maudhi sana..na mtu anaona hakuna njia nyingine zaidi ya kulewa....jaribu kukaa na rafiki yako na akueleze kwa kina naaamini kuna mambo kibao tu amekuficha kwa sababu ya kero ya ulevi wa mumewe..

Yawezekana kwenye ndoa kuna mambo mengi sana......kuna jamaa mmoja kila siku unamkuta baa analewa na muda wa kwenda nyumbani saa 8,9 kila siku siku moja tukamwuliza daahh ni balaa
 
Bebii:

Mshauri rafikiyo kuwa Kubadili tabia mbaya ya mwanandoa yataka moyo na ujasiri mkuu. Ajishushe na kujifunza kusali kwa udhati wa moyo wake. Pili mumewe akirudi asimfokee bali awe wa kawaida tu , amuonyeshe upendo na akiwa kwenye very good mood, amsihi kuwa hapendi kumpoteza kwa ulevi wala ajali au magonjwa yatokanayo na ulevi. Amwambie kuwa anamuombea na atafurahi akipunguza ili apate muda wa kuwa karibu naye na watoto.

Sumu kubwa kwa mlevi ni kumtanganza : hivyo mwambie rafiki yako asimtangaze ovyo kwa mashoga yake , unless imekuwa ni hatari harudi nyumbani unaweza kuwa na ndugu mmoja wa karibu au rafiki ukashare naye.

Tatu: huyu mke mtu ajichunguze mienendo yake; je yeye ni sehemu ya stress , analalamika kila saa, mgomvi bila sababu, hamueheshimu mbele za watu, hana upendo na ndugu etc ; ajichunguze na amwombe Mungu amfanye Mke mwema ili awe chachu ya mabadiliko kwa mwenzie.
 
Na nyie wanawake siku hizi mnasumbua sana kwa jeuri na dharau kwa waume zenu. ndiyo mwanamke anaweza kulazimisha mambo kwa mume wake hadi mwanaume akabadilika tabia aidha akatafuta kidosho kingine au akakazia swaumu kwenye tungi ama vyote kwa pamoja. kuna rafiki yangu ilimkumba hiyo na ilifikia kipind hadi ananyimwa k.. hamuaminik.
 
amnunulie pombe hapo home
kama ni beer aweke kreti nzima baridi na za moto kama ni konyagi dozen moja ya chupa
alafu aanze kupunguza dozi ya pombe kila siku hadi chupa moja
 
waujua upande wa pili wa shilingi,,,, isijekuwa yeye ndo chanzo cha yote,,,, jamaa kaamua mahaba yake ayapeleke kunako pombe..
 
Tafutamaziwa ya nguruwe akiwaanakunywa weka roboyakifuniko chasoda narudia robo usigiogope atatapikasanasana,,nextym same ukimfanyia maratatu anakupaneno lauzima keshoyake uweziamini unaitajiuvumilivu
 
habari zenu wana jamii form, mimi ni mgeni umu ndani naombeni ushirikiani wenu nnarafiki yangu ameolewa na anawatoto watatu, tatizo lake mumewake amekua mlevi sana kiasi kwamba hata akitoka kazini anapitia bar anarudi nyumbani akiwa amelewa,

siku za weekiend ndio kabisaa anarudi saakumi za usiku wakati mwingine saa kuminambili za asubuhi, akimuuliza anamjibkwadharau nakumwambia yeye hatakaa abadilike iyo ndo tabia yake, nakama anaona awezi aondoke,

jamani uyu rafiki yangu amechanganyikiwa ajui afanyaje naombeni mumsaidie uyu rafiki yangu jamani.
maishayandoa niwatuwawili,,tungejuarafikiyo uamuziwake upi else mnawezakuwa misukule kutoamawazo aendeleekuvumilia kumbeashaanza kupeleka navyombo kwao,,tupewazo lakekwanza
 
Habari zenu wana jamii form, mimi ni mgeni umu ndani naombeni ushirikiani wenu Nnarafiki yangu ameolewa na anawatoto watatu, tatizo lake mumewake amekua mlevi sana kiasi kwamba hata akitoka kazini anapitia bar anarudi nyumbani akiwa amelewa,

Siku za weekiend ndio kabisaa anarudi saakumi za usiku wakati mwingine saa kuminambili za asubuhi, akimuuliza anamjibkwadharau nakumwambia yeye hatakaa abadilike iyo ndo tabia yake, nakama anaona awezi aondoke,

Jamani uyu rafiki yangu amechanganyikiwa ajui afanyaje naombeni mumsaidie uyu rafiki yangu jamani.

Alcohol abuse is sign of underlyng disease
 
Back
Top Bottom