Mimi nimeolewa na nimefunga harusi na mume wangu, ila toka anioe mume wangu sijafurahia ndoa yangu ispokuwa siku ya honeymoon. Siku hizi mume wangu akija nyumbani anaanza kunigombeza bila sababu, ananipiga bila kosa, hataki kuniona, anarudi usiku sana nyumbani amelewa nikimuuliza anaipa kipigo cha mbwa, ananitukana matusi, yaani hapa nilipo sina amani na ndoa yangu.
Nishaurini jamani nifanyeje?