mume wa mtu

mume wa mtu

tommy d

Member
Joined
Dec 20, 2012
Posts
13
Reaction score
0
kuna kaka mmoja ni rafiki yangu na ana mpenzi wake lakin kwa muda kidogo wamekua kama hawaelewani na wanaishi nyumba moja hawajaoana asa kaka ananitaka mim niwe mpenzi wake akimaanisha kashoshwa na kutoelewana na mpenzi wake nimejitahidi mwelewesha kwamba sitaweza kua nae kwasababu nami ninampenzi wangu hanielewi labda nimjibu nin anielewe?mana amekua msumbufu kwangu
 
Hivyo anavyoshindwa kuelewana na mpenziwe ndivyo atakavyoshindwa kuelewana na wewe?as long as hulazimishwi em tumia hekima yako,unafikiri kama ameshindwa kumuealewa mpenzi wake,atakuelewa wewe?au we mzuri sana au una nini cha ziada kumzidi huyo mpenziwe?na we si mwanamke kama yeye,so amka kuwa makini na uamuzi wako.Huyo kijana ni mchezeaji tu a.k.a playboy hana lolote.
 
kuna kaka mmoja ni rafiki yangu na ana mpenzi wake lakin kwa muda kidogo wamekua kama hawaelewani na wanaishi nyumba moja hawajaoana asa kaka ananitaka mim niwe mpenzi wake akimaanisha kashoshwa na kutoelewana na mpenzi wake nimejitahidi mwelewesha kwamba sitaweza kua nae kwasababu nami ninampenzi wangu hanielewi labda nimjibu nin anielewe?mana amekua msumbufu kwangu
kwa hiyo unataka ushauri wa jf wakati kinafahamika kabisa
1.endelea na msimamo wako wa kuwa una mpenzi
2.ikishindikana hebu mwambie mpenzi wako kuwa kuna mtu ananifatilia ili akushauri
3.mwambie kuwa kama yuko serious amuite mpenzi wake na wa kwako harafu aongee jambo lako kama ana akili atakataa na atakoma kabisa
4.kuwa na msimamo akutishe nini hayo ni majaribu tu
 
Mbona unaonekana kama vile na wewe unampenda huyo jamaa, maana kama ulishamkataa na ukamweleza kwamba una mpenzi wako yanini akuumize akili?????
Asikusumbue akili kiasi hicho, hebu endelea kufanya kazi zako usipoteze muda bure.
Tulia na mpenzi wako acha kutangatanga.
 
Sasa unataka ushauri gani?
Hujui uaminifu? Wewe una mpenzi wako kilichopo ni kuwa mwaminifu kwa mpenzi wako,unadhani kuwa na mpenzi utatongozwa tena, hata ukiolewa utatongozwa pia ni wewe tu kuamua kukituliza kwa mpenzi wako sio unauliza uliza hapa.au unamtaka nini?
 
Hakuna kitu kinaponza kama kumpa mwanaume nafasi ya kumsikiliza wakati unaelewa nini anataka.!

Umeshamwambia una mpenzi wako.. Sasa unampa nafasi ya kukubughudhi kwa nini?

Kama akikupigia simu usipokee, sms usimjibu..! Au na wewe unampenda??
 
ha ha ha ha ha ha ..wonders shall never end in jf..lolz
Yaani hata maneno ya kumwambia mtu kuwa humtaki huna!
The easiest thing for you is 'if you cant fight him join him'......
 
kuna kaka mmoja ni rafiki yangu na ana mpenzi wake lakin kwa muda kidogo wamekua kama hawaelewani na wanaishi nyumba moja hawajaoana asa kaka ananitaka mim niwe mpenzi wake akimaanisha kashoshwa na kutoelewana na mpenzi wake nimejitahidi mwelewesha kwamba sitaweza kua nae kwasababu nami ninampenzi wangu hanielewi labda nimjibu nin anielewe?mana amekua msumbufu kwangu

Mwambie humtaki kwa sababu una mpenzi tayari huku unamaanisha. Ukimwambia huku unacheka cheka na kung'ata vidole unafikiri ataelewa? Wanaume tulio wengi huwa hatutishwi na kibuti cha mara ya kwanza, hivyo kama unamaanisha inabidi ung'ang'anie sana msimamo wako vingenevyo, ataonja mwenzio!
 
Hahahaaa..... Mwambie kwamba nawe wampenda sana!
 
Jamani hata vyama vya siasa vinahamishaga wanachama kutokana na sera,ah bwana check na mbayuwayu!
 
Kila mtu ameumbwa na hulka yake.. So cishangai huyu dada kushindwa kuyafanya hayo mnayoshangaa mbona hayafanyi..
Anyway cha kwanza ambacho nimekiona ni kwamba jamaa's very selfish.. Anajifikiria mwenyewe tu.. Hilo ndilo tatizo letu wanaume (especially wa kiafrika).. Anatakiwa amfikirie huyo anaeogambana nae mara kwa mara.. Na tatizo la ugomvi linatokea wapi.. Na anadhani kwako ndo hakutakuwa na ugomvi..? Possibility kubwa jamaa ana matamanio.. hajatulia na kwa sababu hizo hawezi kupigana ili mahaba yaendelee..
 
Kama wewe hutaki si unakata mawasiliano madam!

Nini kuvuta vuta mambo lolz.

Kaza buti upate wako, achane na kojoleo za watu hizo.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom