ladyfurahia
JF-Expert Member
- May 10, 2011
- 14,758
- 9,589
- Thread starter
- #41
yani umenifafanulia vyema bestito nashukuru sana kwa kunielewesha ila nimependa hii page hii imenigusa sana tena sana 4;NGUVU YA MAOMBI😛rayers are very powerful tools.Funga na kusali kwa imani utafanikiwa tu.Biblia ilishasema "Mke mwema hutoka kwa bwana"LIKEWISE mume mwema hutoka huko huko kwa bwana.Sio rahisi kuanza kumtafuta tu mume/mke mwema...na ukampata ni vizuri kumtanguliza Mungu ktk hili.
Swali lako ni gumu na "complex" kidogo kwa sababu kwa maoni yangu lina-cover sio tu psychology lakini hata spiritual matters.Majibu yangu ntayagawa katika maeneo ya kiroho na ya kisaikologia kama ifuatavyo:
1;SIFA UNAZO?:Ili kumpata mume/mchumba mwema....jiulize "wewe ni mwema?' na unadhani mume mwema ana vigezo gani?wewe unavyo?Kwa sababu utaidanganya nafsi yako bure kama umeweka viwango ambavyo hata wewe huna!Kumbuka ndege waliofanana huruka pamoja.
2;UMRI:Mwanaume kijana mwenye umri kati ya miaka 32-35 mpaka 40 ni mwenye uzoefu na mambo mengi na anaweza kuhimili misukosuko ya ndoa na maisha.Kwa lugha nyingine huu ni umri ambao mwanaume anajua vipaumbele vyake na nini anatakiwa afanye na ni kwa wakati gani!Huu ni wakati ambao hata kama alikuwa ni mwenda disco sana basi anweza kupunguza na kuacha kabisa na kuwa tayari katika maisha ya ndoa...tofauti kabisa na kijana wa miaka 25,28 nk.
3;ELIMU:Dunia imebadilika na ina changamoto nyingi sana.Ni muhimu kwa mume unayemtaka awe na elimu angalau ya advance diploma/bachelor degree.Hili litasaidia sii katika changamoto za kifedha hata katika malezi ya watoto na mahusiano yenu.Lakini elimu pia inasaidia hata uelewa wa mambo complex kama ya kiimani na kupunguza uhafidhina(unoko usio wa lazima).
4;NGUVU YA MAOMBI:Prayers are very powerful tools.Funga na kusali kwa imani utafanikiwa tu.Biblia ilishasema "Mke mwema hutoka kwa bwana"LIKEWISE mume mwema hutoka huko huko kwa bwana.Sio rahisi kuanza kumtafuta tu mume/mke mwema...na ukampata ni vizuri kumtanguliza Mungu ktk hili.