Katibu mkuu ndio injini ya chama chochote kile. Katibu mkuu makini, hufanya chama kuwa imara. Geuza na kinyume chake. Angalia kwa CDM chini ya Dk Slaa na CUF kabla maalim Seif hajawa makamu wa kwanza wa rais.
Katika historia ya CCM, haijapata kutokea katibu mkuu aliyefunikwa kama mzee Mukama. Watangulizi wake wote walikuwa machachari katika duru za siasa. Angalia enzi za Pius Msekwa, Marehemu Rashidi Kawawa, Marehemu Horace Kolima, Marehemu Lawrence Gama, Mangula na hata mzee Makamba. Hawa wote sauti zao zilikuwa zinasikika.
Au kawa katibu mkuu wa heshimu "ceremonial chief secretary"? Maana viongozi wa heshima ni nadra sana kupaza sauti zao, na hata wakipaza huwa ni ushauri/maoni tu. Kwa CCM, inavyoonesha katibu mtendaji ni Nape Nauye.
Mukama, ibuka kutoka huko ulikofichwa, uje ujibu hoja za Dk Slaa na M4C. Dk Slaa anasema Nape (Katibu wa uenezi) si saizi yake. Anakutaka wewe katibu mkuu mwenzake.
Katika historia ya CCM, haijapata kutokea katibu mkuu aliyefunikwa kama mzee Mukama. Watangulizi wake wote walikuwa machachari katika duru za siasa. Angalia enzi za Pius Msekwa, Marehemu Rashidi Kawawa, Marehemu Horace Kolima, Marehemu Lawrence Gama, Mangula na hata mzee Makamba. Hawa wote sauti zao zilikuwa zinasikika.
Au kawa katibu mkuu wa heshimu "ceremonial chief secretary"? Maana viongozi wa heshima ni nadra sana kupaza sauti zao, na hata wakipaza huwa ni ushauri/maoni tu. Kwa CCM, inavyoonesha katibu mtendaji ni Nape Nauye.
Mukama, ibuka kutoka huko ulikofichwa, uje ujibu hoja za Dk Slaa na M4C. Dk Slaa anasema Nape (Katibu wa uenezi) si saizi yake. Anakutaka wewe katibu mkuu mwenzake.