Hivi nchi hii ukiwa na kilabu cha usiku ni 'dhambi kubwa' kiasi chama chako hakipaswi kuongoza nchi...bali ukiwa fisadi na mbadhirifu wa rasilimali za umma unakuwa umepikika 'kimaadili' na kutamba kuwa unastahili kuongoza nchi! Kama vilabu vya usiku ni vibaya kiasi hicho, walifuata nini 'Maisha Club'? Kwa nini Mukama hakukataa alipoalikwa kwenda Maisha Club ikiwa watu wanaojihusisha na hizo club hawana maadili na hawafai kushika uongozi wa nchi!?
huyo hata hana hadhi...,ebu tu kwanza angalieni mavazi yake pamoja na kofia anayovaaga....!
hana jipya huyo asubirie 2015 ifike aone wanavogaragazwa kama mbwa mwizi
Hao viongozi wa CCM anajitapa kama"WAMEIVA KIMAADILI"ndiyo hawa akina Chenge na akina Lowassa?Ndiyo hawa akina JK waliokataa kujiuzia nyumba ZETU mwaka 2004 kwa sababu ya mahesabu yake ya kugombea U-Rais lkn aliposhinda "AKAIKOMBA" kwa bei ya bwerere?
Ama kweli AKUTUKANAYE hakuchagulii tusi!