Mukama aibuka, aishambulia CHADEMA!

ila ye anasahau kuwa chama chake kinawahonga watu wa upinzani ili wakihamia ccm wapewe vyeo. mbona pia hajasema wao wanategemea viongozi kutoka upinzani?
 
Watu waliopikaka wangefanya chaguzi zao kwa kutumia mlungura, uku tukiona wengine wakirushiana viti.
 
Verbal diarhea, CDM inafanya ofisi zisikalike, wewe Mukama tangu kifo cha kamanda BOB MAKANI tulikusoma
 
RC Kilimanjaro kasema CCM lazima ipandikize wana ccm CHADEMA ili ife. Kwa kauli hii ya RC ni kwamba viongozi wa CCM ni dhaifu hivyo wakiingia CHADEMA itakufa.
 
katibu mkuu asiye katibu mkuu wa ccm.hana political influence then anatafuta umaarufu kwa kuitaja chadema.uzee wake ktk chama chake ni kuangamiza profile ya chama chake.2015 si mbali majawabu yatakuwa wazi!
 
Huyu mzee nae hii kazi ya kuropoka ana iweza Nape!

Huyu mzee amesubiri cdm wamenyamaza ndio ana ongea!

Naomba haache tumalize msiba wa Barlow!
 
Hivi nchi hii ukiwa na kilabu cha usiku ni 'dhambi kubwa' kiasi chama chako hakipaswi kuongoza nchi...bali ukiwa fisadi na mbadhirifu wa rasilimali za umma unakuwa umepikika 'kimaadili' na kutamba kuwa unastahili kuongoza nchi! Kama vilabu vya usiku ni vibaya kiasi hicho, walifuata nini 'Maisha Club'? Kwa nini Mukama hakukataa alipoalikwa kwenda Maisha Club ikiwa watu wanaojihusisha na hizo club hawana maadili na hawafai kushika uongozi wa nchi!?

Anaumwa ugonjwa uitwao WASIWASI,also known as Uchizi.
 
Inasikitisha hawa ndio viongozi wetu, jamaa anadhani wananchi wanaochaguliwa CDM kuwa viongozi wanaokotwa! hajui CDM ni chama cha wananchi Na kila mtu anaweza kugombea uongozi bila kujali elimu yake, bila kujali ni Mtoto wa kigogo gani au uwezo wake kifedha! sifa kubwa ikiwa ni kukubalika na wananchi. mbona tunaowaona CCM ambao jamaa anadai wamepikwa kwenye tanuru ndio mafisadi, Wala rushwa Na watoa rushwa ili wachaguliwe. wengine jana wana kashfa ya kuwa Na viwanda vya kuchakachua ARV halafu leo wanachaguliwa kuwa viongozi! Ama kweli CCM ni sikio la kufa!
 
MASKINI MUKAMA,HIVI ANAJUA KUWA CCM ANAIMALIZA? Maana kati ya makatibu bora wa vyama vya siasa anapitwa na Dr.NA MAALIMU.
 
Nina uhakika Mzee Mangula au Marehemu Kolimba asingesema maneno haya, na hapo ndipo wepesi wa hoja za Mukama unapozidi kushika kasi; Viongozi wa CCM wanaokataa kwamba CCM imechuja kwa kila hali ndio wanaokipeleka chama chetu kaburini; Hata Nyerere miaka michache kabla ya kufariki, alizungumzia CCM kwa lugha kinyume na hii ya Mukama; Pia aliwahi kusema kwamba:

"WATANZANIA WANATAKA MABADILIKO, NA WASIPOYAPATA CCM, WATAYATAFUTA KUPITIA CHAMA KINGINE".

Tunahitaji viongozi ndani ya CCM, wanaogundua kwamba nguvu ya Chadema ipo na inazidi kukua, na nguvu hii inatokana na CCM kusaliti historia yake yenyewe;
 
Maskini Mukama! Chama chake kimeshindwa kufanya kampeni ya udiwani Arusha, yeye yupo Dar anakisifu!
 
Hao viongozi wa CCM anajitapa kama"WAMEIVA KIMAADILI"ndiyo hawa akina Chenge na akina Lowassa?Ndiyo hawa akina JK waliokataa kujiuzia nyumba ZETU mwaka 2004 kwa sababu ya mahesabu yake ya kugombea U-Rais lkn aliposhinda "AKAIKOMBA" kwa bei ya bwerere?

Ama kweli AKUTUKANAYE hakuchagulii tusi!
 
huyo hata hana hadhi...,ebu tu kwanza angalieni mavazi yake pamoja na kofia anayovaaga....!

Huyu jamaa hajitambui, angekuwa anajitambua saa hizi angekwisha funga virago vyake na kuelekea kwao Musoma kwani mkweree hana imani nae kabisa; ndio maana hata amedharau mapendekezo ya utafiti wake wa jinsi ya kukarabati chama chao cha magamba!! Utasikia , kwanza atakosa kuchaguliwa kuwa mjumbe wa NEC toka kwenye kapu na baada ya hapo kibarua chake kitaota mbawa!!
 
hana jipya huyo asubirie 2015 ifike aone wanavogaragazwa kama mbwa mwizi

ukali wa CDM unamfanya kila alieko ccm kuota kama anatupwa motoni!!! maana kila anaye ibuka anakuwa kama katangulia dakika tatu mbele.CHADEMA MOTOOOOOO!
 
Hao viongozi wa CCM anajitapa kama"WAMEIVA KIMAADILI"ndiyo hawa akina Chenge na akina Lowassa?Ndiyo hawa akina JK waliokataa kujiuzia nyumba ZETU mwaka 2004 kwa sababu ya mahesabu yake ya kugombea U-Rais lkn aliposhinda "AKAIKOMBA" kwa bei ya bwerere?

Ama kweli AKUTUKANAYE hakuchagulii tusi!

Huyu Mukama anazungumzia maadili gani wakati yeye ndiye aliyempa Mzee Kingunge tenda ya kifisadi ya kukusanya ushuru pale stendi ya Ubungo!! Mpaka leo hii Pinda anaona aibu kuiweka wazi ripoti ya tume alioiunda kuchunguza ufisadi ule wa ukusanyaji ushuru pale Ubungo. Inaelekea hajui maana ya maadili.
 
Back
Top Bottom