Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 1,814
- 4,547
Muhsein Awadhi Said (Dkt. Cheni) Muigizaji Mkongwe na Mshereheshaji maarufu amechukua fomu ya kuwania Ubunge katika Jimbo la Ilala kupitia Chama cha Mapinduzi.
Baada ya zoezi la kuchukua fomu hiyo Dkt. Cheni aliongea kwa kifupi na Waandshi wa habari kuwa yeye ni mzaliwa wa Ilala kwa sasa amechukua fomu akiwa na nia ya kugombea Ubunge kwenye jimbo hilo lakini mambo mengine zaidi atayazungumza wakati sahihi ukifika.
Zaidi ya hayo, Viongozi mbalimbali kutoka Vyama tofauti wameonesha nia ya kutaka kuwania Ubunge katika Jimbo hilo la Ilala. Mathalani, Muigizaji mwingine Rashidi Mwinshehe Saidi maarufu kama (Kingwendu) ametangaza nia ya kutaka kugombea Ubunge katika jimbo hilo Kupitia chama cha CUF.
=> Uchaguzi 2020 - Rashid Mwinshehe(Kingwendu) achukua fomu ya kugombea Ubunge jimbo la Ilala
Hata hivyo, kwa sasa Jimbo hilo la Ilala linaongozwa na Mh. Mussa Azzan Zungu wa Chama cha Mapinduzi.
Baada ya zoezi la kuchukua fomu hiyo Dkt. Cheni aliongea kwa kifupi na Waandshi wa habari kuwa yeye ni mzaliwa wa Ilala kwa sasa amechukua fomu akiwa na nia ya kugombea Ubunge kwenye jimbo hilo lakini mambo mengine zaidi atayazungumza wakati sahihi ukifika.
Zaidi ya hayo, Viongozi mbalimbali kutoka Vyama tofauti wameonesha nia ya kutaka kuwania Ubunge katika Jimbo hilo la Ilala. Mathalani, Muigizaji mwingine Rashidi Mwinshehe Saidi maarufu kama (Kingwendu) ametangaza nia ya kutaka kugombea Ubunge katika jimbo hilo Kupitia chama cha CUF.
=> Uchaguzi 2020 - Rashid Mwinshehe(Kingwendu) achukua fomu ya kugombea Ubunge jimbo la Ilala
Hata hivyo, kwa sasa Jimbo hilo la Ilala linaongozwa na Mh. Mussa Azzan Zungu wa Chama cha Mapinduzi.