Chakaza
Platinum Member
- Mar 10, 2007
- 41,009
- 74,643
Waziri wa Ardhi au mpishi mkuu Ikulu? Maana kwa huba anayoionyesha basi chakula lazima kiwe salama.Nahisi utateuliwa na kikwete kua Waziri wa ardhi
Waziri wa Ardhi au mpishi mkuu Ikulu? Maana kwa huba anayoionyesha basi chakula lazima kiwe salama.Nahisi utateuliwa na kikwete kua Waziri wa ardhi
![]()
WAKATI Watanzania wakisubiri kujua hatima ya Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, aliyewekwa kiporo na Rais Jakaya Kikwete baada ya kuhusishwa na kashfa ya uchotwaji wa zaidi ya Sh bilioni 300 kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow, waziri huyo amesafiri kwenda Davos nchini Uswisi kuungana na rais katika Mkutano wa Jukwaa la Uchumi Duniani maarufu kama World Economic Forum.
Kwa mujibu wa chanzo cha habari kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Profesa Muhongo ameondoka nchini jana. Profesa ameondoka leo (jana) kwenda Switzerland (Uswisi) ambako ataungana na rais kwenye mkutano huo utakaoanza Januari 21 hadi 24, kilipasha chanzo hicho.
MTANZANIA ilipomtafuta Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Salva Rweyemamu, ili kuthibitisha taarifa hiyo, hakuweza kutoa jibu na badala yake kumporomoshea mwandishi matusi huku akimwambia aachane na habari hiyo.
Acha habari zenu za kipumbavu hizo, alisema Salva.
Alipoulizwa habari za kipumbavu ni zipi na kwanini anatukana badala ya kutoa majibu alisema: Nimekwambia acha upumbavu, kama unataka habari nipigie na kama hutaki usinipigie, siyo kila kitu mnachoandika tu lazima nizungumzie, alisema na kukata simu.
Akizungumza na wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam Desemba 22 mwaka jana, Rais Kikwete alitangaza kumuweka kiporo Profesa Muhongo akisubiri kupata ufafanuzi kuhusu mambo kadha wa kadha ili kujiridhisha kabla kuujulisha umma juu ya hatua atakazochukua dhidi ya waziri huyo.
Wakati akimuweka kiporo Muhongo, Rais Kikwete alitangaza kutengua uteuzi wa aliyekuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka baada ya vyombo vya Serikali kubaini na kujiridhisha amekiuka maadili ya utumishi wa umma kwa kuingiziwa Sh bilioni 1.65 kwenye akaunti yake binafsi.
Rais Kikwete alifikia hatua hiyo akitekeleza moja ya maazimio manane ya Bunge kuhusu sakata la uchotwaji wa fedha kwenye akaunti ya Tegeta Escrow yaliyofikishwa serikalini lililopendekeza kuwajibishwa kwa Bodi ya Shirika la Umeme (Tanesco), Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Eliakim Maswi ambaye amesimamishwa kazi kupisha uchunguzi, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Tibaijuka, pamoja na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Muhongo.
Source:Mtanzania
Upo dunia ipi wewe? ukiwa Mara huwezi kwenda UswisiJamani upotoshaji huu hadi lini? Leo asubuhi muhongo alikuwa mara,kaenda mda gani uswisi?
Wakati baadhi ya wapinga maendeleo nchini wakipuuza uwezo wa Prof. Sospeter Muhongo ktk utendaji kazi wake, wanaotambua uwezo wake wanatumia mawazo na taaluma yake kuendeleza nchi zao kwenye sekta ya Nishati na Madini. Prof. Muhongo amealikwa Davos nchini Uswisi kuhudhuria kwenye World Economy Forum, mkutano huo mkubwa unashirikisha viongozi na wataalamu kutoka mataifa mbalimbali.
Pia waziri Muhongo amealikwa na serikali ya Marekani kwenye mkutano mkubwa unaojadili masuala ya Nishati ambapo atakuwa mmoja wa wazungumzaji kwenye mkutano huo. Aidha, Prof. Muhongo akitoka Marekani, atakwenda nchini Italia kwa mwaliko wa nchi hiyo kwa ajili ya kutoa mada kwenye mkutano unaojadili masuala ya Madini. Huyo ndo waziri mchapakazi Prof. Sospeter Muhongo ambaye hatuoni thamani yake lakini wenzetu wanaiona na kuitumia, ipo siku tutamkumbuka!!
Wakati baadhi ya wapinga maendeleo nchini wakipuuza uwezo wa Prof. Sospeter Muhongo ktk utendaji kazi wake, wanaotambua uwezo wake wanatumia mawazo na taaluma yake kuendeleza nchi zao kwenye sekta ya Nishati na Madini. Prof. Muhongo amealikwa Davos nchini Uswisi kuhudhuria kwenye World Economy Forum, mkutano huo mkubwa unashirikisha viongozi na wataalamu kutoka mataifa mbalimbali.
Pia waziri Muhongo amealikwa na serikali ya Marekani kwenye mkutano mkubwa unaojadili masuala ya Nishati ambapo atakuwa mmoja wa wazungumzaji kwenye mkutano huo. Aidha, Prof. Muhongo akitoka Marekani, atakwenda nchini Italia kwa mwaliko wa nchi hiyo kwa ajili ya kutoa mada kwenye mkutano unaojadili masuala ya Madini. Huyo ndo waziri mchapakazi Prof. Sospeter Muhongo ambaye hatuoni thamani yake lakini wenzetu wanaiona na kuitumia, ipo siku tutamkumbuka!!
Taarifa ya uongo hiyoMbona kuna taarifa kwamba JK amewaita mawaziri wake wote warudi Dar, na ambao tayari wako Dar wasitoke.
Vipi hiyo taarifa ni ya uongo au haimuhusu Prof Muhongo.
Wakati baadhi ya wapinga maendeleo nchini wakipuuza uwezo wa Prof. Sospeter Muhongo ktk utendaji kazi wake, wanaotambua uwezo wake wanatumia mawazo na taaluma yake kuendeleza nchi zao kwenye sekta ya Nishati na Madini. Prof. Muhongo amealikwa Davos nchini Uswisi kuhudhuria kwenye World Economy Forum, mkutano huo mkubwa unashirikisha viongozi na wataalamu kutoka mataifa mbalimbali.
Pia waziri Muhongo amealikwa na serikali ya Marekani kwenye mkutano mkubwa unaojadili masuala ya Nishati ambapo atakuwa mmoja wa wazungumzaji kwenye mkutano huo. Aidha, Prof. Muhongo akitoka Marekani, atakwenda nchini Italia kwa mwaliko wa nchi hiyo kwa ajili ya kutoa mada kwenye mkutano unaojadili masuala ya Madini. Huyo ndo waziri mchapakazi Prof. Sospeter Muhongo ambaye hatuoni thamani yake lakini wenzetu wanaiona na kuitumia, ipo siku tutamkumbuka!!
![]()
WAKATI Watanzania wakisubiri kujua hatima ya Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, aliyewekwa kiporo na Rais Jakaya Kikwete baada ya kuhusishwa na kashfa ya uchotwaji wa zaidi ya Sh bilioni 300 kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow, waziri huyo amesafiri kwenda Davos nchini Uswisi kuungana na rais katika Mkutano wa Jukwaa la Uchumi Duniani maarufu kama World Economic Forum.
Kwa mujibu wa chanzo cha habari kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Profesa Muhongo ameondoka nchini jana. Profesa ameondoka leo (jana) kwenda Switzerland (Uswisi) ambako ataungana na rais kwenye mkutano huo utakaoanza Januari 21 hadi 24, kilipasha chanzo hicho.
MTANZANIA ilipomtafuta Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Salva Rweyemamu, ili kuthibitisha taarifa hiyo, hakuweza kutoa jibu na badala yake kumporomoshea mwandishi matusi huku akimwambia aachane na habari hiyo.
Acha habari zenu za kipumbavu hizo, alisema Salva.
Alipoulizwa habari za kipumbavu ni zipi na kwanini anatukana badala ya kutoa majibu alisema: Nimekwambia acha upumbavu, kama unataka habari nipigie na kama hutaki usinipigie, siyo kila kitu mnachoandika tu lazima nizungumzie, alisema na kukata simu.
Akizungumza na wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam Desemba 22 mwaka jana, Rais Kikwete alitangaza kumuweka kiporo Profesa Muhongo akisubiri kupata ufafanuzi kuhusu mambo kadha wa kadha ili kujiridhisha kabla kuujulisha umma juu ya hatua atakazochukua dhidi ya waziri huyo.
Wakati akimuweka kiporo Muhongo, Rais Kikwete alitangaza kutengua uteuzi wa aliyekuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka baada ya vyombo vya Serikali kubaini na kujiridhisha amekiuka maadili ya utumishi wa umma kwa kuingiziwa Sh bilioni 1.65 kwenye akaunti yake binafsi.
Rais Kikwete alifikia hatua hiyo akitekeleza moja ya maazimio manane ya Bunge kuhusu sakata la uchotwaji wa fedha kwenye akaunti ya Tegeta Escrow yaliyofikishwa serikalini lililopendekeza kuwajibishwa kwa Bodi ya Shirika la Umeme (Tanesco), Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Eliakim Maswi ambaye amesimamishwa kazi kupisha uchunguzi, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Tibaijuka, pamoja na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Muhongo.
Source:Mtanzania
Roho zinawauma na uongo wa billioni 300 hamjauacha tu?
Kikwete haburuzwi.