Muhongo amfuata Jakaya Kikwete Uswisi

Muhongo amfuata Jakaya Kikwete Uswisi

Profesa Muhongo aalikwa Uswisi, Marekani
Atahutubia mikutano ya wasomi duniani


Na mwandishi wetu,

Waziri wa Nishati wa Tanzania Profesa Sospeter Muhongo amealikwa kuhudhuria mkutano unaoshirikisha viongozi na wataalamu kutoka mataifa mbali mbali nchini Uswisi.

Mkutano huo ujulikanao kama World Economic Forum unafanyika jijini Davos nchini humo. Aidha kutoka nchini Uswisi, Profesa Muhongo ataelekea nchini Marekani alikoalikwa na Serikali ya nchi hiyo kwenye mkutano mkubwa unaojadili masuala ya nishati ambapo yeye atakuwa mmoja wa watoa mada.
Akitoka nchini Marekani, Profesa Muhongo ataelekea nchini Italia ambako pia amealikwa kama mmoja wa wataalamu duniani. Wakati mataifa makubwa yakipigana vikumbo kuwasilisha mialiko kwa Profesa Sospeter kwa kuthamini na kuheshimu utalaamu wake, wanasiasa na wafanyabiashara hapa nchini wameendelea kupuuza utaalamu huo na kuwalaghai watanzania.
Kikundi hicho cha watu wenye kusaka madaraka wanaotafuta fursa ya kuiweka mkononi serikali ijayo, wamekuwa wakitumia vyombo vya habari kuchafua wataalamu na wasomi mahiri wanaoheshimika duniani kama Profesa Muhongo.
"Inasikitisha wapinga maendeleo hawa wanaotumiwa na mataifa yale yale yanayothamini utaalamu wa akina Muhongo, wameendelea kuwafanya watanzania wajinga wao wanaoweza kuwaburuza kwa propaganda na kuwchafua watu wema na wazalendo", ameeleza kwa masikitiko Bwana Swedi Mfanyabishara jijini Dar es salaam.
Aidha ameelezea kushangazwa na watu waliojipatia uheshimiwa ambao awali amedai walikuwa wezi na majambazi, wanavyoweza kuwa na ujasiri wa kuwatukana wataalamu kama Profesa Muhongo. "Umefika wakati sasa kwa wazalendo wa nchi hii kusimama imara kupambana na watu hawa ili kuwaokoa watanzania wasiangukie mikononi mwa mabepari na wezi wa rasilimali zao", amedai.
Wakati huo huo, Waziri Muhongo ameiagiza Bodi ya TANESCO ifuatilie miradi ya umeme ya makaa ya mawe ili kumaliza kabisa tatizo la upatikanaji wa umeme nchini.
Aidha mradi wa umeme vijijini(REA) unatarajiwa kupeleka umeme kwenye vijiji 1,500 nchini kote na kwamba Waziri Muhongo ameagiza mikoa na wilaya kuhakikisha mradi huo unakamilika kabla ya Aprili 30 mwaka huu. ( Source; ALHUDA)
Go to hell with your useless propaganda. Sospeter Muhongo ni mwizi tu wa pesa za umma kama walivyo wezi wenzake wote wa serikali na CCM. Tumechoka na hizi propaganda za kipuuzi za CCM kwenye mitandao ya kijamii.
 
Ucha ujinga wa kulishwa mdomoni dogo. Onesha kwa vithibitisho mahali alipoiba. Angekua mwizi angealikwa na wanaoichukia rushwa? unafikiri Marekani hawana data zake? Wajinga mtamchukia werevu wanamgombania!
 
Go to hell with your useless propaganda. Sospeter Muhongo ni mwizi tu wa pesa za umma kama walivyo wezi wenzake wote wa serikali na CCM. Tumechoka na hizi propaganda za kipuuzi za CCM kwenye mitandao ya kijamii.

Kaiba nini labda mbona unatoka post
 
Profesa Muhongo aalikwa Uswisi, Marekani
Atahutubia mikutano ya wasomi duniani


Na mwandishi wetu,

W
aziri wa Nishati wa Tanzania Profesa Sospeter Muhongo amealikwa kuhudhuria mkutano unaoshirikisha viongozi na wataalamu kutoka mataifa mbali mbali nchini Uswisi.

Mkutano huo ujulikanao kama World Economic Forum unafanyika jijini Davos nchini humo. Aidha kutoka nchini Uswisi, Profesa Muhongo ataelekea nchini Marekani alikoalikwa na Serikali ya nchi hiyo kwenye mkutano mkubwa unaojadili masuala ya nishati ambapo yeye atakuwa mmoja wa watoa mada.
Akitoka nchini Marekani, Profesa Muhongo ataelekea nchini Italia ambako pia amealikwa kama mmoja wa wataalamu duniani. Wakati mataifa makubwa yakipigana vikumbo kuwasilisha mialiko kwa Profesa Sospeter kwa kuthamini na kuheshimu utalaamu wake, wanasiasa na wafanyabiashara hapa nchini wameendelea kupuuza utaalamu huo na kuwalaghai watanzania.
Kikundi hicho cha watu wenye kusaka madaraka wanaotafuta fursa ya kuiweka mkononi serikali ijayo, wamekuwa wakitumia vyombo vya habari kuchafua wataalamu na wasomi mahiri wanaoheshimika duniani kama Profesa Muhongo.
"Inasikitisha wapinga maendeleo hawa wanaotumiwa na mataifa yale yale yanayothamini utaalamu wa akina Muhongo, wameendelea kuwafanya watanzania wajinga wao wanaoweza kuwaburuza kwa propaganda na kuwchafua watu wema na wazalendo", ameeleza kwa masikitiko Bwana Swedi Mfanyabishara jijini Dar es salaam.
Aidha ameelezea kushangazwa na watu waliojipatia uheshimiwa ambao awali amedai walikuwa wezi na majambazi, wanavyoweza kuwa na ujasiri wa kuwatukana wataalamu kama Profesa Muhongo. "Umefika wakati sasa kwa wazalendo wa nchi hii kusimama imara kupambana na watu hawa ili kuwaokoa watanzania wasiangukie mikononi mwa mabepari na wezi wa rasilimali zao", amedai.
Wakati huo huo, Waziri Muhongo ameiagiza Bodi ya TANESCO ifuatilie miradi ya umeme ya makaa ya mawe ili kumaliza kabisa tatizo la upatikanaji wa umeme nchini.
Aidha mradi wa umeme vijijini(REA) unatarajiwa kupeleka umeme kwenye vijiji 1,500 nchini kote na kwamba Waziri Muhongo ameagiza mikoa na wilaya kuhakikisha mradi huo unakamilika kabla ya Aprili 30 mwaka huu. ( Source; ALHUDA)
Susuma kwa nza kabisa wewe umejiunga jamvi hili 2015; nachelea kusema wewe ni sawa na buku saba wa Lumumbubumba...

Pili, hakuna anayepinga kuwa profesa si msomi mahiri na mtaamu wa madini, anayeheshimika duniani kote, shida yake ni kuingia kwenye shimo la wezi tu!! Kachota mgapo wake..na yeye kawa kama wenzake, maana kwa sasa wanamuita "mwenzao"

Sisi tunajua, kuwa huyu huyu profesa unayempigia chapuo... aah kwanza siyo kumpigia chapuo, yaani umeingizwa kwenye orodha ya wapiga debe wake ili tumfafishe huyu "mwenzetu" kama wanavyojiita na wezi wenzake...ili akagombee jimbo mkoani Mara...

Wewe bana chukua buku zako saba...sepa kwenye viroba, maisha yaendelee...
 
Last edited by a moderator:
Nashukuru tokea uhuru kijiji chetu kimepata umeme mwaka jana.MUHONGO JEMBE.
 
Unaona namna unavyoendeleza ujinga wa kulishwa sumu? nani kakuambia Prof anahitaji Jimbo? Usimfananishe na wasomi njaa wanaogombea majimbo. Wasomi wanaojitambua hawagombei wanachaguliwa!
 
Uriria umeona eh, nani mwingine kawasambia umeme kama Muhongo!
 
Hizo ziara ni mpango mahsusi kuenda kuweka sawa mabilion ya wizi.

Kuhakikisha account zinasoma vema, zinakuwa na usiri wakutosha na kujuwa masario halisi.

Kiporo hiki kiliachwa na kikwete kwa sababu maalum, baada ya kujiridhisha kila kitu kipo sawa ikiwemo fedha

kuhifadhiwa vema ndipo kikwete atazuka na kujifanya anapeleka kiporo jalalani.
 
Yan watz tunataka wanasiasa kama Mr two. Apo ndo tunatosheka.Naombea muhongo akae kwenye hyo wizara mpaka mungu atakapomchukua.
 
Go to hell with your useless propaganda. Sospeter Muhongo ni mwizi tu wa pesa za umma kama walivyo wezi wenzake wote wa serikali na CCM. Tumechoka na hizi propaganda za kipuuzi za CCM kwenye mitandao ya kijamii.

Moja ya mazao ya kukaririshwa kila kitu
 
Muhongo lazima Jk amfukuze kabla tarehe 27.01.2015
 
Team ushuzi mtasubiri sana mwaka huu! Muhongo jembe . Mzee wa nguzo, go , go , go, muhongo
 
hAZOMEWI MTU HAPO, aZOMEWE KWA LIPI? MTASHUPAA SANA SHINGO KUSUBIRI MUHONGO AONDOLEWE. BABA RIZ MWENYEWE ANAMKUBALI KAMANDA WAKE, UKISIKIA JEMEDARI , BASI NI MUHONGO.
 
Mleta mada shida iko wapi hapo,nyie mnadhani kila mnaepiga makelele aondolewe anaondolewa,acheni ulofa na ukanjenje.

Muhongo alitangaza mchana kweupu akifukuzwa nchi itatikisika. Lazima kumheshimu bwana kubwa.Aisee sijui watu wanapata jeuri wapi.
 
Back
Top Bottom