Muhimbili: Kuanzia Julai Mosi, hakuna ndugu kutembelea mgonjwa muda wa saa 6-8 mchana

Lazima ulipie elfu 30000 kwa ajili ya chakula kwa siku tatu kama mgonjwa wako atalazwa. Ni upfront payment, kama huna mgonjwa wako halazwi.

Maswali ya kujiuliza
1. Kama chakula wanachotoa sitaki nitafanyaje. Mfano mimi nataka supu asubuhi, mchana maini na jioni kuku je watanipa?

2. Je wenye bima na bina tunajua haihusiki na chakula cha mgonjwa bali matibabu na dawa itakuwaje.

Nadhani hii ni namna ya kusema watuwasiende mujimbili kutibiwa.
Ngoja tuone huo utaratibu mpya leo nimesikia kuwa hakuna tena matibabu ya bure lazima mgojwa achangie ( gazeti la mwananchi la leo) mchango ni 60%. Ninavyojua mimi chakula kwa mgonjwa ni sehemu ya tiba. Tanzania ina zalisha maskini wengi sana kadri tunavyokwenda mbele. Sehemu kubwa ya mafanikio ni stasticks tu. Tunaongeza idadi ya mashule huku tunapunguza ubora elimu tunayotoa ( kielelelezo ni matokeo, yakiwa mabaya tunabadilisha taratibu kwa kupanua gori) tunaongeza vituo vya afya huku tukipunguza ubora wa huduma etc etc. Tunakounda kugumu kuliko tunakotoka ingewezekana mimi ningerudi tunakotoka.
 
Hii mwendo kas sasa imepitiliza hii nikuuwa watu kabisa je wale ambao hawana ndugu nan atawalipia izo ela au wafe to
 
Hospitali ya Taifa Muhimbili kupitia msemaji wake bwana Aminieli Bubelwa Eligaesha, imesema kufuta utaratibu wa ndugu kutembelea wagonjwa muda wa mchana kuanzia saa sita mpaka nane mchana, badala yake Hospitali ya Taifa imetangaza utaratibu mpya wa kulisha wagonjwa.

Utaratibu huo umefutwa kutokana na kuingiliana na shughuli za kitabibu kwa wagonjwa muda huo wa mchana.

Muda wa kuona wagonjwa utabaki kuwa asubuhi saa 12 na jioni saa 12.

Maoni Yangu
Ni vyema utaratibu huo lakini bado nina mashaka kama wataweza kuhudumia wagonjwa wote kwa huduma iliyo bora kabisa.

Muhimbili ina wagonjwa wengi sana kuanzia wazazi,watoto,walopata ajali,waathirika wa VVU.

Tunajua huduma zilivyo mbovu,miundombinu hovyo na sasa wanajitishwa hili la kulisha wagonjwa, si ndio mwanzo wa kulishana Ugali na Maharage!! Kumbuka kila mgonjwa kuna chakula anachokipenda pindi aumwapo, nafikiria itakuwaje.Hakika nina mashaka.


Mwanzo mgumu ila time will tell kama hiyo service ni nzuri au la.
 
Kuna wakati muhimbili alieumwa kichwa alipasuliwa mguu na wa mguu kichwa. Tangu hapo sijawahi kuiamini muhimbili.

Nafanya kila niwezalo nisiumwe sana, hadi watu wawe makini kazini.

Hii ya kutoa chakula nayo italeta mashida makubwa sn. Watu wetu wengi hawapendi umakini ktk utendaji. Ni KUKURUPUKA tu!! Na sasa hii awamu ndo dah... kosea kwanza utatatua tu baadae!!
 
Tunajua huduma zilivyo mbovu,miundombinu hovyo na sasa wanajitishwa hili la kulisha wagonjwa, si ndio mwanzo wa kulishana Ugali na Maharage!! Kumbuka kila mgonjwa kuna chakula anachokipenda pindi aumwapo, nafikiria itakuwaje.Hakika nina mashaka.

Mkuu, nilikuwa na mgonjwa wiki mbili zilizopita. Alipata ajali na alikuwa hajitambui kabisa kwa muda wa siku tano. Hakuwa na kitambulisho chochote hivyo alihudumiwa kama unkown person hadi pale alipopata fahamu na akaweza kutufahamisha ndugu. Niwe mkweli kabisa, kwa jinsi nilivyomkuta sikuamini kama yale ninayoyaona ni Muhimbili ile ninayoifahamu na kupata shuhuda mbalimbali kutoka kwa wadau wengine. Muhimbili ya sasa imebadilika sana. Mgonjwa wangu amehudumiwa vinzuri sana utadhani yupo hospitali binafsi. Nilijaribu kumpa pesa nesi mmoja kama ahsante lakini alikataa katakata. Kiukweli kwa sasa Muhimbili wanafanya kazi ipasavyo. Sina uhakika kwa wagonjwa wengine ila kwangu mimi niliridhika na huduma alizopewa mgonjwa wangu hasa ukizingatia alikaa siku tano bila kujitambua. Kwa hili nawapongeza Muhimbili kwa kukubali kubadilika.
 
image.jpeg
image.jpeg
MUHIMBILI KUSITISHA WAGENI KUPELEKA CHAKULA KWA WAGONJWA.

Hospitali ya taifa ya Muhimbili imesitisha utaratibu wa kuwapeleka wagonjwa chakula toka nyumbani kuanzia tarehe 1-7-2016. Badala yake chakula kitaandaliwa hospitali kwa gharama ya sh 50,000. Ktk hiyo gharama, sh 10,000 ni ya kulazwa, sh 10,000 ya kumwona daktari na sh 30,000 ni ya chakula. Gharama hizo ni kwa siku 5. Hivyo kuanzia tarehe hiyo, ukienda kumwona mgonjwa wako , utaenda kama ulivyo bila kubeba chochote zaidi ya matunda tu.

Jukumu la kulisha wagonjwa litabaki mikononi mwa Wauguzi ambao kimsingi ndio jukumu lao.Kampuni ya Usambara Catering ndio imepewa zabuni ya kupika chakula hicho cha wagonjwa kwa hitaji la kila mgonjwa
 
Lakini chakula hiki hakita kuw na magumashi???

Wasijelishwa kama wapo boarding school na poor hospitality??

Maana huduma ya kawaida tu watu wanasumbuliwa na kunyanyisika , kwenye msosi huku wajipange
 
Nimependa mchanganuo wa hiyo hela . Hivi walimu pia wana hela maalum ya kuwaona ofisini. ? Here in Sweden teachers are paid more than other public servants.
 
Hofu yangu kupata huduma nzuri, chakula kizuri na hata unyenyekevu kwa wagonjwa wasiojiweza, huko mawodini kuna vitimbi sana hadi unatamani umrudishe magonjwa wako nyumbani awe anakuja kupata huduma tu..
 
Back
Top Bottom