Elections 2010 Mugabe amponza Kikwete

Hatuwezi kula vyura ndugu yangu. Badala yake itatusaidia kukumbuka tunu za awali kabisa za utawala wa TANU na Mwl. Nyerere kuwa "nchi hii itajengwa na watanzania wenyewe, kila mtanzania, kila mzalendo na hasa kila mjamaa" Huu ndio ulikuwa mwanzo wa dhana ya kujitegemea ambayo viongozi wetu wameiweka kapuni na kuhubiri kuombaomba aka kuhemea.

Zamani hawa wanaoitwa wafadhili walikuwa na majina stahiki kama wakoloni mamboleo, mabeberu, wanyonyaji, makupe nk. Sijawahi kusikia katika siku za hivi karibuni kiongozi yeyote wa CCM akitumia majina hayo japo ukweli unabaki palepale kuwa huu tunaouita utandawazi ni uleule uliokuwa ukiitwa ukoloni mamboleo (neo colonialism) enzi hizo na Mwl Nyerere na viongozi wengine wenye akili wa Africa enzi hizo.

Salut!
 
Hivi ni nchi zipi mpaka sasa zimetuma salamu za pongezi kwa JK baada ya ushindi wa kuchakachua?
 
how come marafiki zake aliokuwa anawatembelea kila wakati kuwaalika waje hapa kututembelea sisi (pamoja na kwamba hawajaja hata mmoja,labda bush), mbona hata pongezi tu hazijaja wala wao hawajaja...ina maana safari zile zilikuwa za bure, hazikujenga urafiki wowote kati yya nchi yetu na hizo za magaribi? hata wachina hawajatuma salamu...hata hao wachina ambao ni mabingwa wa kuvunja haki za binadamu..dah..kweli dunia kijiji, ulifanyalo hapa dar kila mtu duniani analiona na kutafakari...ikulu kipindi hiki ni chungu kama pilipili iliyochanganywa na limao...kama mtu hajawai kuumwa pressure, basi kichwa kitauma...
 
Kuhudhuria kwa rais wa Zimbabwe Robert Mugabe wakati wa kuapishwa kwa rais Kikwete kunaelezwa na wanazuoni huenda ikawa sababu ya nchi nyingi hasa za magharibi kusita kumpongeza rais Kikwete aliyeapishwa leo.

Nchi hizo za magharibi zenye ushawishi mkubwa duniani zikiwemo Marekani na Uingereza, pamoja na kuwakilishwa na mabalozi wake inasemekana hadi sasa hazijatuma salamu za pongezi za kuchaguliwa kwa Kikwete kitu ambacho si kawaida yake.

Ikumbukwe kuwa wakati wa uchaguzi uliopita wa Zimbabwe ambao ulilalamikiwa sana na UK na USA kuwa haukuwa huru na wa haki umepelekea hadi leo Mugabe na familia yake kunyimwa hati ya kuingia katika nchi hizo isipokuwa kuhudhuria mikutano ya UN pekee.

Wachambuzi wa mambo wanahisi tukio la leo kwa Mugabe kuhudhuria linaweza kuwa limetia doa mahusiano ya Tanzania na nchi hizo ikizingatiwa kuwa kuna madai yanayotolewa na chama cha upinzani Tanzania kuwa kulikuwa na udanganyifu wa kura wakati wa kuhesabu.
taarifa wanazo za kuwa uchaguzi ulikuwa huru (kidogo) lakini haukuwa wa haki hata kidogo. Sina hakika kama na mwaka huu ataenda kuomba net za mbu marekani wakati zinashonwa Arusha
 
People are worring to loose support from western countries because our prez is only capable of thinking supports. Ndo maana aliwaambia wananchi wa shinyanga kuwa aingekuwa anasafirisafiri tungekufa njaa. Kwa hilo naamini kauli yake kuwa "I do not know why my country is poor". nadhani kwa mawazo yake ni kwamba hatujapata rais anayejua kutembeza bakuli huko ulaya.
 
Vijana someni historia ili mjue mchango wa nchi hii kwa ukombozi wa nchi kama Zimbabwe. Wakina Mugabe wamelelewa hapa kwetu kisiasa kwahiyo uhusiano wa CCM na ZANU PF ni wa damu!! Ndio maana huwezi kusikia hata siku moja Tanzania ikimcriticize Mugabe.

Mkuu ni kweli kabisa,uhusiano wa ZANU PF na CCM ni wa damu kabisa. Marehemu Joshua Nkomo angekuwa hai angekueleza ni jinsi gani CCM ilivyomsaidia Robert Mugabe baada ya kufanyika uchanguzi wa kwanza wa Rais, huko siendelei wataalamu wa siasa wanaweza kuendeleza hapo.
 
2c2 just to let you know sio predictions. Brasil walituma salamu za pongezi right away kwani kuna mjadala kutuma salamu za pongezi. Huu ni ujumbe tosha kwa jk na serikali yake wamechemsha uchaguzi huu. Nilisema hawa watu sio kama wamelala usingizi tusubiri utasikia kama nchi jirani wanasema uchaguzi tz ni kama mchezo wa kuigiza unategemea nchi kama marekani na uingereza watasema nini????
 
Nadhani motto ingekuwa,
'JF- where we dare to think critically'

Hivi kweli ktk karne hii bado mtu anataka tuchaguliwe rafiki au adui?
 
kuhudhuria kwa rais wa zimbabwe robert mugabe wakati wa kuapishwa kwa rais kikwete kunaelezwa na wanazuoni huenda ikawa sababu ya nchi nyingi hasa za magharibi kusita kumpongeza rais kikwete aliyeapishwa leo.

Nchi hizo za magharibi zenye ushawishi mkubwa duniani zikiwemo marekani na uingereza, pamoja na kuwakilishwa na mabalozi wake inasemekana hadi sasa hazijatuma salamu za pongezi za kuchaguliwa kwa kikwete kitu ambacho si kawaida yake.

Ikumbukwe kuwa wakati wa uchaguzi uliopita wa zimbabwe ambao ulilalamikiwa sana na uk na usa kuwa haukuwa huru na wa haki umepelekea hadi leo mugabe na familia yake kunyimwa hati ya kuingia katika nchi hizo isipokuwa kuhudhuria mikutano ya un pekee.

Wachambuzi wa mambo wanahisi tukio la leo kwa mugabe kuhudhuria linaweza kuwa limetia doa mahusiano ya tanzania na nchi hizo ikizingatiwa kuwa kuna madai yanayotolewa na chama cha upinzani tanzania kuwa kulikuwa na udanganyifu wa kura wakati wa kuhesabu.

jana nilimuona balozi wa uingereza hapa nchaini katika dhifa ya kitaifa ya kumpongeza kikwete kwa ushindi
.
 
kumwalika Mugabe sioni kama tatizo, Mugabe alipita kwa njia gani hilo linaweza kuwa tatizo, ila kumtegemea mzungu aje akujengea hata choo, hii ni aibu kubwa tutabaki tegemezi mpaka lini??????
ukiwa tegemezi wewe ni mtumwa tuuu, huwezi kufanya maamuzi yako mpaka uulize wakubwa wako unaowategema, shame shame shame!
we need strong leader ambao hawatapiga magoti mbele ya wazungu na kuwa ombaomba
 
"Mugabe , like many African leaders is a dictator. The only difference is that Mugabe is brighter than Jey Key" Lockfellor...

Jamani nimequote tu.....
 
"Mugabe , like many African leaders is a dictator. The only difference is that Mugabe is brighter than Jey Key" Lockfellor...

Jamani nimequote tu.....

Wee nyumbu nauliza jamaa bado wamemchunia ngozi mpaka leo hawajampongeza?
 
Back
Top Bottom