Haya maswala ya Wazanzibar kumtukana Mwalimu ni utovu tu adabu tu ambao kama umegundua Sisi tuna hulka ya kuwasema watu vibaya wakisha fariki tena kwa habari za kusimuliwa.Na katika Uislaaam, ni kosa kubwa (Dhambi) kumsema vibaya marehemu ambae weee binaadam sii hakimunwala huijua hatmanyako siku ya Kiyam Kwa hiyo hayo matusi ya Wazanzibar najua yametokana na Siasa za Upotoshaji ambazo zimekuja toka tuanzishe mfumo wa vyama vingi.
Mkuu haya matusi ya Wazanzibar kwa Nyerere yalikuwa deliberate na kwasababu ya imani yake. Kama muungano uliundwa na Nyerere na Karume kwanini hatukuwasikia wakisema Karume Laanatullah!
Ikiwa kiongozi anabeba lawama za maamunzi kama nyerere, mbona hatusikii laanataullah kwa aliyesababisha Oct 29. Main point hapa ni kwamba, chuki ya Wazanzibar ni katika misingi ya dini! wamepandikiza mbegu hii sana
In fact Wananchi walikataa vyama vingi kwa asilimia 80 lakini ni mwl. Alolazimsha tuanzishe Mfumo wa Vyama vingi kinyume kabisa cha matakwa ya Wananchi wengi. So was he wrong? Nambieni nyie mlotokana na asilimia 80!
Nyerere alitoa sababu akisema hili ni wimbi linalovuma duniani akamtolea mfano rafiki yake Nicolae Cieasescu. Nyerere alisema Nicolae alisubiri wanaompinga wakawa wengi.
Nyerere alimaanisha ni muhimu viongozi wawe 'ahead of time' katika kufikiri. Tatizo la Oct 29 ni viongozi kutokuwa 'ahead of time' licha ya red flags zote zilizokuwemo. Hapa JF tulionya na kuna bandiko tulilosema '' nchi imevimba, viongozi wawe na busara, kinachosubiriwa ni njiti ya kiberiti''. Viongozi hawakusikiliza, hawakuwa mbele ya muda, yakatokea
Vyama vingi vilikuwa ni wakati wake. Watanzania 80% waliokataa ilikuwa ni ''fear of unknown'' kwamba vyama vingi vitaleta fujo, infact ni CCMwaliowatisha Wananchi.
Mwalimu alijua fika kwamba wananchi wanataka ili wanahofu ndio maana aliingilia. Ukisoma alama za nyakati zile, madhara makubwa yangetokea ikiwa suala hilo lingekataliwa.
Mungu alijaalia tukawa na Nyerere mwenye akili, Elimu, asiye na kiburi, anayesoma na anayaelewa.
Mwisho niseme hivi, nionavyo mimi katika UTU wetu. Wewe nitukane unavyotaka, mimi sitorudisha matusi kwa sababu ni sawa na kumfukuza Kichaa au mgonjwa wa akili. Wazungu walitubagua kwa miaka 500, haina maana nasi tulipize kisasi tuwabague, isipokuwa tutawaambia Ukweli ambao wao wenyewe wataamua kubaki nasi ama.warudi makwao!
Nakuelewa sana mkuu, lakini kumbuka imeachukua Watanganyika zaidi ya miaka 50 kuvumilia.
Imefika mahali Wazanzibar kwa kuvumiliwa wanajiona ni Raia wa daraja la juu na kwamba wanathamani sana katika Muungano.
Watanganyika hasa vijana wamehoji nini kinapatikana kwa muungano na Zanzibar watu 1.8 kati yao milioni 1 wanaishi Tanganyika. Wanahoji nje ya Muungano Tanganyika inapoteza nini. Jibu lake ni hakuna na ndipo wanasema sasa wanataka Tanganyika yao ili waache Wazanzibar wajitenge.
Ukisikiliza waumini wa Muungano kama Warioba, Butiku n.k. utaona kuna kuchoshwa na kelele za Wazanzibar.
Binafsi, simkubali rais Samia kama.Kiongozi, hili naliweka wazi kabisa ila sii kwa sababu yeye ni Mzanzibar au Muislaam bali sioni kama anazo Sifa na Uwezo wa Kuongoza Taifa.
Utamtenga vipi na Uzanzibar wakati alikwenda na kusema 'uchaguzi huu hakuna Mzanzibar aliyenyakuliwa''
Kuhusu udini tunarudi pale pale, Nyerere hakuua Wazanzibar lakini ni laanatullah, kwanini leo isiwe laanatullah kwa mauaji ya Oct 29? what goes around comes around! dude.
Nakubaliana nawe though! kwamba mambo ya dini na ukanda hayana maana. Nisichokubaliana ni kuhusu Zanzibar. Tumefika point of no return, hakuna namna ya ku rescue muungano! Tanganyika has nothing to lose. Wazanzibar watajuta!