(Emancipate from mental Slavery)
Watanzania kwa ujumla wetu bado tumelala usingizi mzito tukiota ndoto za jinamizi kuhusu mustakabali wa Taifa letu.
Mambo nayoyasoma na kuyasikia yakitoka vinywani na maandishi kusema kweli ni aibu kwa taifa ambalo waasisi wetu walitujengea misingi bora ya Taifa letu. Leo hii tumezama katika ombwe la Ubaguzi ambao tunaivunja misingi hiyo makusudi kama kwamba tumechoka, liwalo na liwe.
Kuna haya mambo mawili nayasoma na kuyasikia sana yakinadiwa bila hekima chini ya mwanvuli wa UDINI na UKANDA katika majukwaa ya mihadhara mbali mbali ya Kijamii tena wazi kabisa huhitaji elimu ya saikologia.
Leo hii kuna watu hawaoni aibu kabisa kuzungumzia Uzanzibari na Utanganyika, wala hawana uso wa soni kutuonyesha wazi chuki zao kwa Waislaam ama Wakristu kama kwamba ni jambo la kheri kabisa kwa ulinzi wa jamii zao ama Taifa hili.
Binafsi kuna wakati hudhani pengine mimi ndiye naota ndoto hizi kwa sababu misingi tuloachiwa na Waasisi wetu ilikuwa thabiti haiwezekani kabisa ikavunjwa kupitia Ubaguzi wa aina yeyote.
Niseme hivi, kama kweli sababu ya migongano yote hii ni rais Samia Suluhu Hassan ambaye ni Mwanamke, Mzanzibar na Muislaam basi yawapasa Wanawake, Wazanzibar na Waislaam wote wasimame naye kwa sababu ni mwenzao, ama iwe Wanaume, Watanganyika na Wakristu wasimkubali rais huyu kwa sababu sii mwenzao!
Basi huu utakuwa ni Upumbavu mkubwa ulopita vipimo vyote vya mapana na marefu. Ni Upumbavu uso kifani ambao mwalimu Nyerere alituasa mapema kabisa katika moja ya hutuba zake. Tunachotakiwa ni kumlaani shetani alochukua nafsi zetu kwa ahadi hizi za kutupeleka Jahanam hapa hapa duniani tukiwa hai ndotoni kabla hata ya Kiyama!
Kibaya zaidi, leo tunashuhudia baadhi Viongozi ama Wanasiasa wakizungumzia Uzanzibar wakidai nchi yao sii kwa sababu nyingine ya maana isipokuwa kuwakana Watanganyika na Wakristu! Vile vile Upande wa Bara pia kuwakana ndugu zao kwa sababu ni Wazanzibar na Waislaam - Heeee!
Mimi nitoe rai yangu kwa watu wote wanaotumia Dini na Ukanda kutaka kutugawa Watanzania kwa sababu ya nia na dhamira zao chafu ambazo aidha wanadhani hili ndio koti lilowabana, nawashauri wajipime wenyewe upya isije kuwa wao ndio wamenenepa sana ama wamekondeana kiasi cha kuhatarisha afya zao.
Yawezekana kabisa rais Samia ana mapungufu mengi kama kiongozi wa nchi, lakini inapotumiwa sababu za Udini na Ukanda kuashiria ndio sababu za mapungufu yake, basi haya mapungufu sii yake yeye bali ya wale wanao mshutumu. Vile vile kwa wale wanaomsifia Samia wasiyaone mapungufu yake kwa sababu hizo hizo nao pia wamepikwa chungu kimoja.
Amkeni, amkeni Watanzania toka usingizi wa pono unatesa ndoto zetu tukifukuzwa na jinamizi baya lilojaa hasada mpaka tunapaa hewani na ufagio bado likiwa nyuma yetu.
Maasalaam
Watanzania kwa ujumla wetu bado tumelala usingizi mzito tukiota ndoto za jinamizi kuhusu mustakabali wa Taifa letu.
Mambo nayoyasoma na kuyasikia yakitoka vinywani na maandishi kusema kweli ni aibu kwa taifa ambalo waasisi wetu walitujengea misingi bora ya Taifa letu. Leo hii tumezama katika ombwe la Ubaguzi ambao tunaivunja misingi hiyo makusudi kama kwamba tumechoka, liwalo na liwe.
Kuna haya mambo mawili nayasoma na kuyasikia sana yakinadiwa bila hekima chini ya mwanvuli wa UDINI na UKANDA katika majukwaa ya mihadhara mbali mbali ya Kijamii tena wazi kabisa huhitaji elimu ya saikologia.
Leo hii kuna watu hawaoni aibu kabisa kuzungumzia Uzanzibari na Utanganyika, wala hawana uso wa soni kutuonyesha wazi chuki zao kwa Waislaam ama Wakristu kama kwamba ni jambo la kheri kabisa kwa ulinzi wa jamii zao ama Taifa hili.
Binafsi kuna wakati hudhani pengine mimi ndiye naota ndoto hizi kwa sababu misingi tuloachiwa na Waasisi wetu ilikuwa thabiti haiwezekani kabisa ikavunjwa kupitia Ubaguzi wa aina yeyote.
Niseme hivi, kama kweli sababu ya migongano yote hii ni rais Samia Suluhu Hassan ambaye ni Mwanamke, Mzanzibar na Muislaam basi yawapasa Wanawake, Wazanzibar na Waislaam wote wasimame naye kwa sababu ni mwenzao, ama iwe Wanaume, Watanganyika na Wakristu wasimkubali rais huyu kwa sababu sii mwenzao!
Basi huu utakuwa ni Upumbavu mkubwa ulopita vipimo vyote vya mapana na marefu. Ni Upumbavu uso kifani ambao mwalimu Nyerere alituasa mapema kabisa katika moja ya hutuba zake. Tunachotakiwa ni kumlaani shetani alochukua nafsi zetu kwa ahadi hizi za kutupeleka Jahanam hapa hapa duniani tukiwa hai ndotoni kabla hata ya Kiyama!
Kibaya zaidi, leo tunashuhudia baadhi Viongozi ama Wanasiasa wakizungumzia Uzanzibar wakidai nchi yao sii kwa sababu nyingine ya maana isipokuwa kuwakana Watanganyika na Wakristu! Vile vile Upande wa Bara pia kuwakana ndugu zao kwa sababu ni Wazanzibar na Waislaam - Heeee!
Mimi nitoe rai yangu kwa watu wote wanaotumia Dini na Ukanda kutaka kutugawa Watanzania kwa sababu ya nia na dhamira zao chafu ambazo aidha wanadhani hili ndio koti lilowabana, nawashauri wajipime wenyewe upya isije kuwa wao ndio wamenenepa sana ama wamekondeana kiasi cha kuhatarisha afya zao.
Yawezekana kabisa rais Samia ana mapungufu mengi kama kiongozi wa nchi, lakini inapotumiwa sababu za Udini na Ukanda kuashiria ndio sababu za mapungufu yake, basi haya mapungufu sii yake yeye bali ya wale wanao mshutumu. Vile vile kwa wale wanaomsifia Samia wasiyaone mapungufu yake kwa sababu hizo hizo nao pia wamepikwa chungu kimoja.
Amkeni, amkeni Watanzania toka usingizi wa pono unatesa ndoto zetu tukifukuzwa na jinamizi baya lilojaa hasada mpaka tunapaa hewani na ufagio bado likiwa nyuma yetu.
Maasalaam