Muda huu nimetoka lock up, kisa mapenzi

Muda huu nimetoka lock up, kisa mapenzi

Tukiwa bado tunatafakari miaka miwili ya Rais Magufuli, kuna majanga yamenikuta mwenzenu. Kwa kifupi toka Jumapili nilikua lock up, sababu kubwa ikiwa ni mapenzi yani kuna mwanamke nilidhani nimepata kumbe nimepatikana.

Mwishoni mwa week nimetoka kwenye mizunguko yangu sikumkuta ghetto, ufunguo kaacha kwa jirani na kaondoka bila kuniaga, nikasema ngoja nimuwekee mtego nione atarudi na nani na akiwa katika hali gani.

Nikamtumia text nikamwambia niko nacheck game ya man u na chelsea,so nitachelewa kurudi na nikiwahi sana basi itakua ni saa 5 usiku, muda huo huo nikaweka patrol mitaa ya pale gheto ili kumnasa adui, mara nikashangaa prado nyeupe inapark pale gheto na yule mwanamke akashuka na lijamaa flani wameshikana mikono, nikaona wamesimama na lile janaume pale muda mrefu.

Mara paa na mimi nikawaibukia pale, sikutaka kuuliza nani ni nani nikatembeza kichapo kwa wote kwa kutumia rungu langu ambalo hua nalihifadhi ndani kama silaha ya kujilinda in case nikivamiwa, yule jamaa nikamg'oa meno mawili ya mbele pale pale na ngeu za kutosha, msichana nikampiga mpaka nikamvunja mkono, tunavyoongea saivi kawekewa POP tayari, jamaa yake kashonwa nyuzi sita usoni, so police waliokua doria wakasikia zile kelele wakaja wakanikamata wakanipeleka central.

Toka Jumapili nilikua lock up, nimefunguliwa kesi ya kushambulia na kudhuru miili ya watu wawili kinachoendelea ni kwamba jamaa niliyembonda hataki masuala ya mahakamani ni mume wa mtu anasema anaona aibu watu wakijua kuwa nimemdunda kisa alikua na kidosho mwingine, kwa hiyo ameniomba haya mambo yaishie police tu me nilipe gharama za kufuta kesi, nimerudi gheto muda huu cha kwanza nimefika nikachukua kila kitu cha yule mwanamke na nimetia kiberiti.

Ahsanteni.
Kumbe polisi kuna gharama za kufuta kesi??.Ni bei gani na unapewa risiti??
 
Hongera sote mura.......
Angekua mwanaume wa Dar, angekuja kuomba ushauri eti kamkuta bibi wake na jamaa na akashuhudia wanaingia ghetto kwa bibie, then akaamua kurudi ghetto kwake na chakwanza ni kuandika uzi wa kuomba ushauri...
 
Duuuh hiyo inaitwa vunjavunja meno ya kibarazani shubaaaaaakengemiti zake well done mkuu hekoo siku nyingine unanishtua maana sijawahi piga mtu alieshikwa ugoni.

Kwa vijana wenzetu wanaopendi hii mchezo iwe fundisho walahi.
 
Umemfurushia mbali huyo mwanamke au ndio unatibu akipona arudi?
 
Gharama ya kufuta kesi isifike mahakamani alipe yeye
 
Ila angeshuka kwenye nissan nyeupe naamini ucngemfuata na rungu ungekimbia uwache.
 
Vurugu yote hiyo kumbe hata sio mke wako. Huwa mnawapata wapi wanawake wanaochepuka kizembe hivyo?
 
Unapigania mke kisa jamaa nalo lingeamua kujibu likutoe meno nalo
 
Hii chai imetiwa vitunguu saumu badala ya tangawizi!
 
Baada ya hapo ukaamka? Au ndoto ikaendelea?
 
Back
Top Bottom