Muda Gani uoge unapomaliza Jogging?

Muda Gani uoge unapomaliza Jogging?

KwetuKwanza

Senior Member
Joined
Mar 13, 2023
Posts
121
Reaction score
218
Naomba msaada wa swali la Afya hapa.

Ukifanya mazoezi ya kukimbia Asubuhi (Jogging) unatakiwa kuoga muda Gani mara baada ya kumaliza mazoezi??? Je unatakiwa kuoga mara tu unapomaliza kukimbia au unatakiwa kukaa muda fulani unapomaliza kukimbia?
 
Maswali mengine!!!! Ukishamaliza ku Jorge unaweza Fanya jambo gani zaidi ya kukimbilia mafuni?
 
Inapaswa usubiri hadi mwili upungue joto, usiingie bafuni kuoga maji ya baridi huku unaloa jasho, ni hatari.
Pia jenga desturi ya kuosha miguu kwanza kabla kichwa au sehemu nyingine ya mwili.
 
Subiri jasho likauke ukimaliza jogging ili jasho lote litoke na ujisugue vizuri ukioga ukitoa uchafu mwilini

Ukikoga kbla ya jasho kukauka mwili utakua haujasafika mana jasho bado litakua halijaisha
 
Naomba msaada wa swali la Afya hapa.

Ukifanya mazoezi ya kukimbia Asubuhi (Jogging) unatakiwa kuoga muda Gani mara baada ya kumaliza mazoezi??? Je unatakiwa kuoga mara tu unapomaliza kukimbia au unatakiwa kukaa muda fulani unapomaliza kukimbia?
Mimi hua napoa kwanza aidha naswaki then ndo nioge,, na Kama unahitaji kua fit tembea usijog
 
Unatulia kwanza unapoa ndio unaoga...... na vizuri zaidi TUMIA MAJI YA MOTO/VUGUVUGU
 
Robo saa ndugu
Kamwe usioge wakati mwili bado haujapoa,utakuja kufia bafuni kwa kipigwa stroke ndugu zako wasingizie bafuni kuna majini
 
Back
Top Bottom