Wont be the same
JF-Expert Member
- Aug 15, 2024
- 1,564
- 2,483
Mjumbe wa Kamati Kuu ya ACT Wazalendo, Mtutura Abdallah Mtutura, amedai kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilitamani ACT Wazalendo kisusie uchaguzi, ili waweze kushinda kwa urahisi, lakini ACT imekataa na kuamua kuwakabili vilivyo.
Akihutubia mkutano wa hadhara katika kijiji cha Mtina, kata ya Mtina, wilaya ya Tunduru, Jimbo la Tunduru Kusini mkoani Ruvuma, mara baada ya kuchukua fomu ya kugombea ubunge kupitia ACT Wazalendo, Mtutura amesema ACT Wazalendo siyo chama cha mapambio kwa CCM hivyo wameamua kukabiliana nao vilivyo.
Katika tukio hilo lililohudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Ado Shaibu, Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo, Mtutura amesisitiza dhamira yake ya kuleta mabadiliko katika jimbo la Tunduru Kusini.
Amesema kuwa ACT Wazalendo imejipanga vizuri na itaendelea kuwa sauti mbadala dhidi ya kile alichokielezea kuwa ni "mamlaka ya mabavu ya CCM" kwenye maeneo ya uchaguzi.
Akihutubia mkutano wa hadhara katika kijiji cha Mtina, kata ya Mtina, wilaya ya Tunduru, Jimbo la Tunduru Kusini mkoani Ruvuma, mara baada ya kuchukua fomu ya kugombea ubunge kupitia ACT Wazalendo, Mtutura amesema ACT Wazalendo siyo chama cha mapambio kwa CCM hivyo wameamua kukabiliana nao vilivyo.
Katika tukio hilo lililohudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Ado Shaibu, Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo, Mtutura amesisitiza dhamira yake ya kuleta mabadiliko katika jimbo la Tunduru Kusini.
Amesema kuwa ACT Wazalendo imejipanga vizuri na itaendelea kuwa sauti mbadala dhidi ya kile alichokielezea kuwa ni "mamlaka ya mabavu ya CCM" kwenye maeneo ya uchaguzi.