Boflo
JF-Expert Member
- Jan 20, 2010
- 4,384
- 4,409
Magaidi washambulia Zanzibar | |
Wajeruhiwa katika tukio la kigaidi | Monday, January 23, 2012 12:42 PM Zanzibari, habari kutoka Zanzibar zinaripoti kuwa, Magaidi wasio na hurama wamewapiga risasa na kuwamwagia tindikali mtu na mkewe. Tukio hilo limetokea eneo la Kiponda. |
Bwana Alvind Asawla na mkewe Bimal Alvind walikumbwa na mkasa huo pale walipokuwa wanarejea nyumbani kwao wakitokea klabu ya pombe (bar). Akisimulia tukio hilo Alvind alisema kuwa, Watu wasiojulikana waliwavamia yeye na mkewe. Katika tukio hilo, Mkewe alimwagiwa tindi kali, na alipojaribu kumtetea akapigwa risasi iyozama kichwani mwake kwa masaa kumi na mawili. Kwa rehema za Mungu risasi haikuharibu ubongo wake. Alvind alisema kuwa, anaamini watu hao ni magaidi kwani wangekuwa majambazi wasingemwagia tindikali maana majambazi wana lengo la kupora mali wala sio kutia watu vilema. Akisisitiza dai lake hilo alieza kuwa, ameshawahi kupokea vitishgo vya mara kwa mara kwa njia ya kupelekewa barua za kumtishia kumuua kama hatoacha kuuza pombe. Baba yangu alimwagiwa tindikali na kupoteza maisha mwaka 2007, ameongezea Bw, Alvind. Naomba serikali ya SMZ iwachukulie hatua watu hawa. Maana hadsi leo hii matukio ya kigaidi kibao yametokea ila hakuna aliyekamatwa. Kama biashara hii ya kuuza pombe haitakiwa ZNZ naomba serikali itufahamishe na tufunge biashara zetu. |