Mauaji yako dunia nzima ila mauaji yenye harufu ya kibaguzi ndiyo yanayopelekea kelele ktk swala hili.
Harufu ya kibaguzi haimaanishi sababu ya mauaji ni ubaguzi wa rangi.
Takwimu zimetolewa na the Washington post ripoti ya desemba mwaka jana na kumbuka blacks ni kama 12% tu ya population ya USA lakini ndo wanaoongoza kuuawa unarmed. Sababu ni nini hasa?
Mpaka niione hiyo ripoti niisome mwenyewe ndiyo nitaweza kuitolea maoni maana kwanza hilo gazeti ni la mrengo wa kushoto. Kwa hiyo ni lazima kuisoma hiyo ripoti kwa jicho la tatu kwa sababu huenda ikawa iliandikwa kisiasa.
Kwa taarifa yako, vyombo vingi vya habari vya Marekani vimekaa kisiasa zaidi....lakini sitegemei ulijue hilo.
Na kuhusu sababu, well, hivi unajua kwamba sehemu zinazoongoza kwa uhalifu nyingi ni za African Americans? Wewe mwenyewe na weusi wako huo nakuhakikishia kuna sehemu nyingi tu za weusi huwezi hata kuthubutu kutembea peke yako...iwe mchana au usiku. Lakini kuna sehemu nyingi tu za weupe ambazo utajisikia amani hata kutembea peke yako muda wowote ule.
Kuna sehemu za weusi mpaka hata polisi wameshazikacha..hawaendi tena maana watu wenyewe hawataki hata kuishi kwa amani wenyewe kwa wenyewe.
Pointi yangu ni nini hapo? Pointi yangu ni kwamba kuna idadi kubwa sana ya watu weusi wafanyao uhalifu.
Haya mauaji ya weusi yasiyokuwa na sababu maalum ndiyo yanayofanya watu wapige kelele.
Mbona mauaji ya wazungu yasiyokuwa na sababu maalumu huwa hata hamyaongelei? Nimekuwekea hapo links za weupe waliouwawa tena wengine waliouwawa na polisi weusi...sijawahi kukuona ukija kulalama hapa na nahisi wala ulikuwa hujui!
Halafu sijui kwa nini unashangaa watu kupigia kelele hilo swala. Weusi ni minority na ni wageni.
Weusi ni wageni Marekani? Kumbe hujui hata historia vizuri. Weusi wamekuwepo Marekani kabla hata Marekani haijawa nchi. Jifunze historia.
Na kuhusu kelele...sababu kubwa ni kwa sababu ni Marekani tu. Ingekuwa yanatokea huko kwingine wala hata msingekuwa mnakuja kujiliza humu na kujifanya mmeguswa sana.
Kuhusu u-minority....hao hao unaowaita minority ndo wanaongoza kwa crime kama ukiziangalia takwimu proportionally. Na hapo juu nimekwambia hata wewe mwenyewe kuna neighborhoods nyingi tu za weusi wenzio ambazo huwezi hata kuthubutu kutembea peke yako au hata na mwenzako mchana...achilia mbali usiku.
hata itokee Tanzania wazungu kumi wauawe bila sababu maalum lazima watu wahoji. Hiyo haimaanishi kuwa wazungu wanakufa zaidi kuliko watanzania.
Ah wapi...sidhani hata kidogo. Huwezi kulinganisha Tanzania na Marekani kivile. Haya yanayotokea Marekani mnajali tu kwa sababu ni Marekani. Yangetokea North Korea huko wala msingehangaika.