Mtu mmoja akutwa amefariki ndani ya basi

Mtu mmoja akutwa amefariki ndani ya basi

Kwa haya ndiyo tutaanza kuelewa hatari iliyopo maana naona bado tupo gizani na tunaota
 
Kwa hali yakushangaza mtu mmoja ambae alikuwa akitokea Dar kwenda Mpwapwa, Dodoma akutwa amefariki dunia wakati basi ilipotia Nanga kwenye stendi ya busi ya wilaya ya Mpwapwa

Mtu huyo inasemekana alivyokuwa njiani alikuwa na mafua makali na pamoja kuhema kwa shida.

Mungu tusaidie

Mkuu naomba kuitikia hapo kwenye sala tu:

Mungu tusaidie - "amina". Mwisho wa itikio.
 
Vifo vya namna hiyo vimekuwa vya kawaida kwa waathirika wa Covid 19. Wanasema ukifikia stage ya ARDS, bila Respiratory Ventilator, una only 20 minutes before death.

Huko Ecuador, maiti nyingi za waliofariki kwa Covid 19 zimekuwa zikiokotwa kwenye mabasi, vituo vya mabasi na majumbani kiasi cha kushindwa kupata hata takwimu halisi za waliokofa na kuugua.

Huko Kahama, nako kuna kisa kinachunguzwa. Kuna mchina na mkewe walichukua chumba hotelini. Wahudumu waligundua mchina mwanamke alikuwa ni mgonjwa hasa japo hakusema. Walipoujulisha uongozi wa hotel, walichukuliwa kwenda hospitali. Uchunguzi unaendelea lakini hwakuruhusiwa kurudi hotelini japo walikuwa wamekwishalipia kwajili ya kukaa siku kadhaa. Kuna hisia walitaka kuifanya hoteli ndiyo isolation place yao.

Ushauri: Kipindi hiki, kama siyo lazima sana, ni aheri kujizuia kusafiri. Na ukisafiri, kama una usafiri binafsi, ukichoka, pumzika ndani ya gari kuliko kulala hotelini.


OMG...Kahama? Nimekwisha!
 
Kwahiyo abiria wengine walipoona hiyo hali ya mafua makali humo ndani ya basi walitulia tu waone kitatokea nini...?
 
Ameendika dalili gani hapo au umekurupuka?

Wacha kukariri kila kifo COVID-19
Hata mwanzo hamkuamini, mlisimama kidete kumpinga yeyeto aliyesema taifa liko hatarini dhidi ya Covid 19.
Leo hata vifo hutaki kuamini . Poor U. Unafikiri hao wanaokufa kwa Corona ni wazembe ??!!!

Odhis *
 
Chanzo cha taarifa na picha ya tukio mkuu!
Unajua sasa kila mauti inahusishwa na COVID 19!
Ni sawa na mtu akiwa Malaya sana hata akifa kwa ajali watasema ni ukimwi tu ila ajali ilikuwa kusudi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Sasa mtu analeta taarifa humu halafu anasema inasemekana, sioni haja ya mtu kukimbia kuanzisha uzi huma kwa taarifa za kusadikika.
 
Kwa hali yakushangaza mtu mmoja ambae alikuwa akitokea Dar kwenda Mpwapwa, Dodoma akutwa amefariki dunia wakati basi ilipotia Nanga kwenye stendi ya busi ya wilaya ya Mpwapwa

Mtu huyo inasemekana alivyokuwa njiani alikuwa na mafua makali na pamoja kuhema kwa shida.

Mungu tusaidie
Tutasikia visa kadhaa vya corona huko Dodoma muda si muda.
 
Hata mwanzo hamkuamini, mlisimama kidete kumpinga yeyeto aliyesema taifa liko hatarini dhidi ya Covid 19.
Leo hata vifo hutaki kuamini . Poor U. Unafikiri hao wanaokufa kwa Corona ni wazembe ??!!!

Odhis *
Upuuzi mtupu

Unaandika hata mwanzo hamkuamini, kuamini nini?

Then uwe unajibu ulichoulizwa sio mwanzo hamkuamini sikuamini nini na lini nilisema siamini?
 
Back
Top Bottom