Mtoto / Watoto kwanza

Mtoto / Watoto kwanza

ERTUGRUL BEY

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2020
Posts
11,541
Reaction score
21,551
Upande wa pili kwenye Simu "Ujue mtoto toka Jana homa imepanda sijampeleka hospitali kwasababu hujatuma hela''.
Mshikaji ''inamaana umeashindwa kupata buku la kumpeleka hospitali mpaka uningojee mimi'' wakaanza kurushiana maneno mtu na bwana wake.
Ikabidi niingilie Kati nikamwambia jamaa,ndugu hapo anaepata tabu ni Mtoto fanya Jambo la Busara utume au uende uhakikishe mtoto anaenda hospitali.
Hii ni truu Stori ambayo imenifanya niufungue huu Uzi,haya ni mambo ambayo huwa yanatokea Kwa wapenzi mmestarehe Kwa Raha zenu mwisho wa siku mkaleta kiumbe hapa duniani.
Ni jukumu la Baba na Mama kuwajibika kumlea huyo mtoto,kama mnatofauti zenu hazi mhusu huyo mtoto,pambaneni na Hali yenu mkihakikisha mtoto haathiriki na mahusiano yenu.
Wanaume mkisha mzalisha binti basi ebu muwe mnawajibika katika malezi ya watoto,sio tunajifanya vidume vya mbegu halafu hiyo mbegu ikileta matunda tunayakimbia,tunawatesa Sana masingle mama,Sawa humtaki basi msaidie katika malezi ya mtoto,hayo ndio majukumu ya kila Baba aliye na akili timamu,tusikimbie majukumu tupambane kutoa matunzo Kwa viumbe wasio na hatia.

Ni hayo tu
 
Daaah ni singo maza??

Halafu huyo jamaa akitaka kuoa atasema sitaki kuoa mwanamke mwenye mtoto
Ndio maana Mimi huwa napinga Sana wanaume ambao wanaongea upuuzi kuwa haifai kuoa single Maza, swali linakuja je huo usingle Maza umetokeaje tokeaje kama sio Sisi wanaume tunawazalisha halafu tuna wabwaga! Kongole Sana Kwa wanaume wote ambao wameoa single Maza nikiwemo Mimi.
 
Ndio maana Mimi huwa napinga Sana wanaume ambao wanaongea upuuzi kuwa haifai kuoa single Maza, swali linakuja je huo usingle Maza umetokeaje tokeaje kama sio Sisi wanaume tunawazalisha halafu tuna wabwaga! Kongole Sana Kwa wanaume wote ambao wameoa single Maza nikiwemo Mimi.
Ni kweli,halafu wanapinga singo maza
 
Ni kweli,halafu wanapinga singo maza
Wanaboa sana

Mimi bwana hata mwanaume akiwa mlevi au mzinzi ingawa sio Tabia nzuri lakini akiwa anajali familia yake daah nampa kongole Sana pamoja na Tabia zake mbaya.

Lkn utakuta mtu mlevi,mzinzi halafu huko nje anaspend Sana lkn home matunzo hakuna,nakereka Sana aisee
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom