Mtoto wangu anataka kuniibia nimeona Dalili

Mtoto wangu anataka kuniibia nimeona Dalili

dogo anaonesha dalili ya mafanikio katika maisha hehehehe
 
Ushauri wangu
Fanya mawasiliano na shule aliyo pangwa upate utaratibu ulivyo wa kubadili combi,pili hata kama ni bure mpe hiyo pesa wewe vingapi umedanganya kipindi upo shule na chuo brother?
 
😂😂 daahhh nimemkumbuka jamaa aliyemdanganya mzazi wake kuwa kavunja assemble ya shule na pesa akapewa

Sasa waliokushtua wameharibu hesabu za dogo
 
Wakati nasoma advance Kuna classmates walihama toka PCM kwenda PCB BURE KABISA. Namaanisha hawakutoa pesa na shule ndo ilishughulikia. Kwani wamepangiwa na shule? Shule alopangiwa ina mchepuo anaotaka kuhamia?
 
Mpe hiyo hela. Kwa uzoefu wangu watoto ambao hawana tabia ya kuomba omba hela huwa wanatumia trick za namna hiyo kupewa na wazazi wao. Hata mimi pia ni miongoni mwao, nimefanya sana hiyo tabia nikiwa advance.

Huwa tunaona kuomba omba mtoto wakiume sio poa bora ukamla mdingi pigo kubwa likakufanya usurvive kwa kipindi kirefu.
 
Kapata B , Chemistry B , Physics C kwa ufupi
Kwa ufaulu huo, ni nadra sana kuchaguliwa arts, kuna mawili.

1. Huenda kachaguliwa Sayansi kakudanganya.
2. Kapangiwa arts kweli.

Cha kufanya, ulizia kama shule hiyo ina michepuo ya Sayansi, ili akabadilishe huko. Utaratibu huwa hivi. Anaandika barua ya kuomba kubadilisha mchepuo, akiambatanisha nakala ya "results slip" kwa ajili ya kurejea kuona kama anasifa za kusoma mchepuo husika.

Hamna mahali wanadai pesa ya kubadilisha mchepuo.
 
Ukimpa tunakuja kujenga taifa la[emoji16][emoji38] wapigaji
 
Wewe kama mzazi uwe unafatilia mambo ya shule sometimes hata bila yeye kujua.
Hiyo inaepusha sana mianya ya ipigaji.

Mfano hizi selction za form 5 zilivotoka tu na ww ulitakiwa ujiridhishe shule anayoend, mchepuo wake na sifa za shule husika chap kwa haraka ikiwezekana na connection za huko mapema kabisa.

Then unamuacha na yeye apalanganyike kivyake kusaka detail za iyo shule, hapo akija na kizinga uchwara kama hicho ni rahisi kumfutilia mbali.

Okay sasa hapo jibu ni kua kama shuleni kwao kuna hiyo combie anayotaka basi wewe uwasiloane na uongozi wa shule kuona uwezekano wa kubadilisha.
Ukiwa mvivu ukamwachia mwenyewe tegemea vizinga zaidi + nauli ya kwenda dodoma/dar + pesa ya kula njian ili aende ofisi za tamisemi ili akabadilishie huko 😀😀
 
"Anasema nimpatie haraka kwamba nikichelewa eti system inajifunga hadi mwakani"😆😆
Mpatie pesa kijana ana shida zake binafsi acha ubahili mkuu.
 
Huyo ni mbunge mtarajiwa! Hongera umekuza aisee!
Wapo wazazi wanalipia photophosphorylation kama shopping item
 
Nasubiri kwa hamu sana watoto wangu waje kunidanganya 😄😄
 
Back
Top Bottom