Mtoto wa Lowassa kugombea ubunge Monduli?

Mtoto wa Lowassa kugombea ubunge Monduli?

KUNA TETE KUWA LOWASSA ANAMWAANDAA MTOTO WAKE KUGOMBEA UBUNGE-MONDULI
Kutokana na kashfa nyingi zinazomkabili Lowassa anasita kugombea tena Ubunge-Monduli 2010,hivyo anamwandaa Mtu (Mtoto)wake kwa ajili ya kugombea.Hata hivyo wananchi wa Monduli wasioendekeza takrima wanaonekana kutaka waongozwe na Mbunge safi na asiye tokana na Mtu yeyote mwenye kashfa ya ufisadi au kashfa yoyote ile.Mwenye undani wa suala hili aturushie.

Nilishuhudia kwenye lununga mapokezi mazito ya Lowasa mara baada ya kujiuzuri kwa kasfa ya ufisadi/uwajibikaji aliyofanyiwa kwenye jimbo lake. Sidhani kama ni wananchi walewale waliokuwa wakimkumbatia, watakuwa wamebadilika na kutomhitaji uchaguzi wa 2010.

Hata hivyo, Ubunge sio ajira!, hiki ni kitu ambacho kinatakiwa kifahamike miongoni mwa watanzania. Hivyo basi kunahaja kama ilivyo kwa upande wa rais, katiba isema pea ukomo wa ubunge sio kwa njia ya kura tu. Hii ndio sababu wanasiasa wanachukulia ubunge ni ajira na hivyo wanafanya juu chini kupambana na new rivals ili kulinda nafasi zao hivyo kuzorotesha uwezo wao wa kufikiri katika kuleta maendelea ya nchi yao.
 
lisemwalo lipo na kama halipo linakuja ......!!!
 
ni kweli kuwa mtoto wa lowasa ana haki kama watanzania wengine, kinachotusumbua ni huyu anaye mwandaa yaani lowasa, je ule wizi aliofanya nakufaidika na mabilioni yasije yakawanunua wananchi wa monduli wakachagua bomu kwa kulambishwa takrima

It is called "DOMESTICATION OF POWER".....Utamaduni huu ni hatari sana kwa nchi zilizogubikwa na Rushwa na Ukabila kwani ni chachu za matumizi mabaya ya vyombo vya dola kuhalalisha utawala kwa manufaa ya kifamilia....

Hata hivyo naamini kuwa watanzania watakuwa wamesoma kupitia kwa majirani zetu Kenya walipofagilia mbali FAMILIA ya MOI kisiasa...angalau katika ubunge..

omarilyas
 
Toure?!! uganga ukuu wa mkoa ameuweza?

Naungana na wewe Nkamangi...Huyu jamaa hovyo tu hakuna chochote...aliwahi kuwa mganga mkuu wa hospitali ya Monduli hakuna kitu. On the other hand...sidhani kama hizi habari za Lowassa (Edward) kumuandaa mtoto wake (I think we are talking of Fred..ama Kadet) kuwa mbunge ni sahihi. Jamaa bado ana ushawishi mkubwa sana, na kwa hela aliyonayo bado sijaona wa kumnyang'anya kiti. Not in 2010.
 
Hapa napata shida sana,kumtofautisha Lowasa na mtoto wake!Kwani kama ufisadi ulifanyika ulimnufaisha nani?Si familia yake?Mtoto akiwa mmojawapo?Je kuna uhakika gani kama hizo fedha za ufisadi hazitatumika katika kampeni ya mtoto.Lakini angalizo lingine ni kwa mtoto,kweli kama yeye ni mzalendo tofauti na baba yake basi angeona aibu kuingia kwenye siasa zilizoifedhehesha familia yao!Kwa upande mwingine huyu mtu Lowasa tunayemtuhumu kuwa hastahili kuiongoza Tanzaia katika nafasi yoyote ya kutumikia umma,Mbona bado anapeta kama mtu mwingine huru tuu?Tena mjumbe wa NEC ,CC na kamati kibao ?Si alipaswa kuwa katika mstari wa mafisadi walioko Keko na Segerea?
Sasa kama Lowassa hayupo huko na wala hatuna mpango wa kumpeleka huko?Kwa nini tumnyime haki yake ya kikatiba yeye pamoja na wanaomzunguka akiwemo mtoto wake?........)
Jambo moja ambalo akili ya kawaida haitaki kulikubali ni kuwa Lowasa ametutia katika hali ngumu kimaisha yeye akiwa kama kiongozi wa juu mwenye dhamana ya Watanzania,Akiwa na wadhifa wa Waziri Mkuu.Ina maaana kweli sisi wananchi hatupati uchungu kumfikiria tena huyu Lowasa kuingia madarakani hata kama ni kwa ngazi ya Kijiji tuu??Lowasa,Mtoto wake wote hawana tena nafasi wa kupewa dhamana ya kuongoza katika nchi hii kwani sifa kubwa ya uongozi wa kuwatumikia wananchi wameipoteza.Wananchi wa Monduli hata msiwasingizie kitu hawa maskini,Kwani hapo awali walidhani kuwa Lowassa angefaa hata kuwa Kiongozi wa jamii yao ya kimasai,Lakini waligundua kuwa wamdhaniaye ndiye kumbe siye.
Umefika wakati Watanzania kuelewa kwamba viongozi tunao wengi sana katika jamii zetu,Tatizo ni huo mwanya wa kuchaguliwa hasa kupitia katika chama chetu cha Mapinduzi.Chama kimechoka,kimekosa mwelekeo na dira kwa kuwa na wazee vikonngwe madarakani .Huku wakiwanyima nafasi vijana wenye upeo wa kutuvusha katika matatizo tuliyonayo.Chama cha watu wakongwe wasiotaka mabadiliko,Wenye uroho wa madaraka hata kufikia kurithishana madaraka!Iweje sisi wapiga kura tuendelee kulalama tuuu wakati tuna uwezo kabisa wa kuwatoa kina Lowasa na wengine wa aina yake? Kama ikishindikanika kwa sababu za ukongwe wa chamaTawala basi shime tuungane kuanzisha vuguvugu la waungwana ndani ya chama chetu na kukiacha njia panda kwa kuanzisha Cha Cha Fikira Endelevu ndani ya CCM.Kigumu sana Chama cha Mapinduzi.
 
Lakini tumesahau kuwa Mtanzania mwenyae umri ya miaka 18 ni mtu mzima, sio tena mtoto wa mtu, ni mtoto wa dunia... Lowasa anaweza kuingia kwenye kinyang'anyiro cha ubunge huyo mtoto wake kwa tiketi ya ccm! Atakayeshindwa na kotoridhika anaweza pia kuhamia CHADEMA!
 
Mtoto wa Sokoine wa Ubalozi DC ni mchapa kazi sana mimi namuunga mkono kama anagombea.
 
Kuna mtoto wa Sokoine ambaye watu wa Monduli wanamtaka sana awe mbuge wao. Lakini kwa influence ya Lowasa huyu jamaa amepelekwa kufanya kazi kwenye balozi zetu na umoja wa mataifa siku nyingi mno na huwa anahamishwa tu kutoka sehemu moja kwenda nyingine ali mradi tu asirudi nchini ili Lowasa aendelee kulimiliki jimbo hilo. Mwenye data zaidi aongezee.

Nitakubaliana na wewe mtoto wa sokoine yupi yule wa pale ubalozini DC?.
 
Joseph Sokoine ndio chuguo la wananchi wa Monduli siku nyingi lakini kutokana na fitina na nguvu za Lowasa amekuwa akipangiwa kazi nje ya nchi sasa 2010 wangetamani sana ajitokeze na kuwania ubunge kwani wana imani kuwa atafuata nyayo za Edward Sokoine kuwatetea wanyonge na si kujilimbikizia mali na kuwatetea matajiri na mafisadi.
 
KUNA TETE KUWA LOWASSA ANAMWAANDAA MTOTO WAKE KUGOMBEA UBUNGE-MONDULI
Kutokana na kashfa nyingi zinazomkabili Lowassa anasita kugombea tena Ubunge-Monduli 2010,hivyo anamwandaa Mtu (Mtoto)wake kwa ajili ya kugombea.Hata hivyo wananchi wa Monduli wasioendekeza takrima wanaonekana kutaka waongozwe na Mbunge safi na asiye tokana na Mtu yeyote mwenye kashfa ya ufisadi au kashfa yoyote ile.Mwenye undani wa suala hili aturushie.

Mmungu ampe nguvu na baraka zake ashinde kwa kishindo na amudu kazi yake kadri atakavyomuwezesha kulitumikia Taifa hili
 
KUNA TETE KUWA LOWASSA ANAMWAANDAA MTOTO WAKE KUGOMBEA UBUNGE-MONDULI
Kutokana na kashfa nyingi zinazomkabili Lowassa anasita kugombea tena Ubunge-Monduli 2010,hivyo anamwandaa Mtu (Mtoto)wake kwa ajili ya kugombea.Hata hivyo wananchi wa Monduli wasioendekeza takrima wanaonekana kutaka waongozwe na Mbunge safi na asiye tokana na Mtu yeyote mwenye kashfa ya ufisadi au kashfa yoyote ile.Mwenye undani wa suala hili aturushie.

Sasa naona Lowassa wa watu anaonewa... lazima huu ni uongo.
 
Kuna mtoto wa Sokoine ambaye watu wa Monduli wanamtaka sana awe mbuge wao. Lakini kwa influence ya Lowasa huyu jamaa amepelekwa kufanya kazi kwenye balozi zetu na umoja wa mataifa siku nyingi mno na huwa anahamishwa tu kutoka sehemu moja kwenda nyingine ali mradi tu asirudi nchini ili Lowasa aendelee kulimiliki jimbo hilo. Mwenye data zaidi aongezee.

Naelewa unamzungumzia Joseph Sokoine, niliwahi kusikia hivyo lakini nilimuuliza yeye mwenyewe habari hizi za Ubunge akawa anachomoa. Kulikuwa kuna habari kuwa aliwahi kujadiliwa kuwa PM. Na habari hizi aliwahi kuchomoa kabisa, lakini the way alivyokuwa akipangua hiyo hoja ukimuona machoni unagundua hakuwa mkweli.
Hata hivyo ningependa kurekebisha kidogo. Huyu jamaa hafanyi ubalozi umoja wa Mataifa bali anafanya kwenye Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani.
 
Watoto wa Lowassa, wa Sokoine ni WATANZANIA. Wagombee tu.
 
Watoto wa Lowassa, wa Sokoine ni WATANZANIA. Wagombee tu.

Ni kweli kabisa mkuu na wengi tutawaangalia vile watakavyokuwa machoni kwetu.Hatutawarisisha madhambi au mazuri ya baba zao. Wataamua wenyewe nini cha kuchukua kama urithi kutoka kwa wazazi.
 
Watz msihofu sana kuhusu Monduli, wazee wa KIMASAI walishamuita siku nyingi Mmasai mwenzao ambaye ni Profesor anayepigania haki za wa fugaji (Pastoralists and Rangelands) agombee na Lowasa alishapata habari akamuita na akajibiwa yeye hana la kusema ila Lowasa akawaulize wazee. Unajua WAMASAI wanafuata MILA zao sana, wazee wakiamua ndilo linalofuata. Lowasa anajua hatopata kwa hiyo anjaribu longolongo tu lakini Umasaini kumekucha.Be informed
 
Back
Top Bottom