Habari za leo ndugu zangu wapendwa? Ni matumaini kuwa mpo safi kabisa. nimekuja hapa kwenye hili jukwaa nikiwa nina shida moja inayonitatiza.
Jana nilikuwa nampa chakula mwanangu (ana miezi 7 na siku kadhaa), sasa wakati nampa nikaona kuwa ameanza kuota meno ya juu badala ya meno ya chini kama ilivyokuwa kawaida.
Hali hii nilishangaa na hata baadae nikamwambia mke wangu ambae nae pia alishangaa na hakuwa na majibu. Sasa nimeleta hii mada hapa kwenu mnipe ushauri kama kutakuwa na shida yeyote katika maendeleo na ukuaji wa mwanangu mpendwa.
Nitashukuru sana kwa michango yenu.
NB: Kama hautakuwa na mchango wa maana tafadhali pita wima,
this is serious case.
===
JF doctors na wazee wa mila naombeni msaada kwa hili tafadhali,
Kwa kawaida mtoto hutakiwa kuanza kuota meno ya chini then meno ya juu hufutia!
Lakini kuna wale watoto ambao huanza kuota meno ya juu, Kwa mila za kiafrika hawa watoto wanaogopwa sana.
Miaka ya nyuma waliishia kutupwa maporini, na uchunguzi unaonesha watawala yaani machifu waliogopa kwamba watoto hao wakikua watawapindua kwani wana vipaji vya ajabu.
Kwenye makabila mengine hapa Tanzania watoto hawa hawaoi kisa atafiwa na wake wote.
Na mila nyingine nyingi tu!
Sasa leo nimeamua kukata mzizi wa fitina kuomba ushauri wa kitaalamu, nini kinatokea hapa!