Mtoto amepotea, msaada please

Status
Not open for further replies.

Jacaranda

Member
Joined
Oct 23, 2011
Posts
45
Reaction score
20


Mtoto huyu anaitwa Benedicto Tungaraza. Amepotea leo tarehe 8/1/2013 maeneo ya kimara-baruti. Alikuwa amevaa shati la drafti mchanganyiko wa rangi nyeupe na damu ya mzee, suruali ya rangi ya kaki , open shoes za blue na soksi nyekundu. Kwa yeyote atakayemwona, please, naomba tuwasiline kwa namba 0713692533, au 0759065635.




 
Inshaalah atapatikana tu.
 
Pole sana mkuu naamini utampata tu.
 
Mkuu, Mungu ni mwema, anamlinda na atamrudisha tu!
 
In Jesus Name, the name above all names mtoto huyo tuna-declare kwamba yuko salama na kwamba jama kuna namna yoyote ile mbaya basi ishindwe na mtoto huyu atarudi na kuungana na familia yake akiwa hai na mwenye Afya. Sisi tunamwamini MUNGU na MUNGU huyu ndie atakayemrudisha mpendwa wetu
 
inshallah mungu akipenda ataonekana kwa kipindi kifupi tu
 
Wasalamu ndg wanaJF......

Nimepotelewa na mtoto jana jioni maeneo ya KIMARA BARUTI mwenye wasifu ufuatao:

JINA: BENEDICT TUNGARAZA

UMRI: MIAKA 7

WAJIHI: MWEMBAMBA, MAJI YA KUNDE

ANAKOTOKA: IRINGA

ANASOMA: GANGILONGA S/M - IRINGA MJINI

MAVAZI: SHATI LA DRAFT NYEUPE NA DAMU YA MZEE, SURUALI YA KAKI, SANDALS ZA BLUE
 
Pole sana, mungu amlinde na hatimaye arudi akiwa salama. ameen
 
Nadhani JF pekee haitoshi, ni vyema wahusika wakatembelea vituo vya luninga ili kupata msaada zaidi pia waende na hiyo picha ili iweze kuonyeshwa na vituo hivyo. Naamini atapatikana mapema
 

ameeeeen
 
Ooh pole sana. Maombi na sala mtoto apatikane salama. Mwenyezi Mungu amlinde huko aliko aweze kurudi nyumbani, alikuwa akielekea wapi na ni mgeni kiasi gani hapo Kimara
 
Nadhani JF pekee haitoshi, ni vyema wahusika wakatembelea vituo vya luninga ili kupata msaada zaidi pia waende na hiyo picha ili iweze kuonyeshwa na vituo hivyo. Naamini atapatikana mapema

oh yeah
 
Oh noooo. Mungu awajaalie subira na amlinde mpaka mutakapokutana.
 
Naomba uwasiliane na Tumaini Radio (wako Tabata) ........wana msaadasana katika masuala haya kwa kufikisha ujumbe kwa jamii........pole mkuu na be strong about this
 
In the name of Jesus Christ atapatikana akiwa na afya njema, Mungu amlinde na wabaya maana huyo ni malaika.
 
Mungu baba uliyeumba mbingu na nchi na macho yako yakimtazama kila mmoja,ambaye wajua hesabu hata za nywele zetu na uliyetuchora ktk vitanga vya mikono yako, Ninaomba popote alipo mtoto BENEDICTO TUNGARAZA aweze kujitokeza kwa njia yoyote ile na arudi akaungane na familia yake,Ninaomba malaika zako wamlinde na mabaya yote na aweze kurudi kwa ndugu zake salama,Nashukuru kwasababu umesikia na utatenda,ktk JINA TAKATIFU LA BABA,MWANA NA ROHO MTAKATIFU. AMEN!!!
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…