KwetuKwanza
Member
- Mar 13, 2023
- 34
- 82
Mtoto mmoja (12) mkazi wa kijiji cha Migato Wilayani Itilima, anadaiwa kufanyiwa vitendo vya ukatili na mtu asiyejulikana hadi kumsababishia majeraha makubwa sehemu zake za siri.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyu Kamishina Msaidizi wa Polisi ACP Edith Swebe, amasema kuwa katika tukio hilo mpaka sasa wanawashikilia watu wawili kuhusiana na tukio hilo huku uchunguzi ukiendelea.
Kamanda Swebe amesema kuwa mtoto huyo alikuwa anasoma darasa la tatu, ambapo tukio hilo limetokea Juni 04, 2023 majira ya saa tano 05:00 asubuhi katika kijiji cha Migato Wilayani Itilima.
“Tukio hili lilitokea wakati binti huyo alipokuwa kwenye shamba la nyumbani kwao akivuna karanga umbali wa mita 140 kutoka nyumbani anapoishi, na kwa sasa amelazwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa kwa matibabu zaidi” amesema Kamanda Swebe.
Kamanda huyo wa Polisi ameeleza kuwa mtoto huyo alifanyiwa tukio hilo na mtu asiyemfahamu, ambapo uchunguzi unaendelea ili kuweza kubaini nini kilitokea.
Kwa upande wake Mganga mfawidhi Hospitali ya rufaa mkoa Dkt. Athanas Ngambakubi amekiri kumpokea mtoto huyo, ambaye amesema alikuwa na jereha kubwa katika sehemu yake ya siri.
Dkt. Ngambakubi amesema kuwa jeraha hilo lilisababisha kutoka kwa baadhi ya viungo vya ndani ya mwili (Utumbo Mkubwa), ambapo baada ya kufikishwa hospitalini hapo walimfanyia huduma ya upasuaji mkubwa na kufanikiwa kurejesha viungo hivyo.
“Tumechukua vipimo vyote vinavyohitajika ili kujua ni nini kilitokea, kwa sasa hatuwezi kusema chanzo cha tukio hilo mpaka pale majibu ya vipimo yakitoka, ila kwa sasa amepatiwa matibabu na anaendelea vizuri” amesema Dkt. Ngambakubi..
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyu Kamishina Msaidizi wa Polisi ACP Edith Swebe, amasema kuwa katika tukio hilo mpaka sasa wanawashikilia watu wawili kuhusiana na tukio hilo huku uchunguzi ukiendelea.
Kamanda Swebe amesema kuwa mtoto huyo alikuwa anasoma darasa la tatu, ambapo tukio hilo limetokea Juni 04, 2023 majira ya saa tano 05:00 asubuhi katika kijiji cha Migato Wilayani Itilima.
“Tukio hili lilitokea wakati binti huyo alipokuwa kwenye shamba la nyumbani kwao akivuna karanga umbali wa mita 140 kutoka nyumbani anapoishi, na kwa sasa amelazwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa kwa matibabu zaidi” amesema Kamanda Swebe.
Kamanda huyo wa Polisi ameeleza kuwa mtoto huyo alifanyiwa tukio hilo na mtu asiyemfahamu, ambapo uchunguzi unaendelea ili kuweza kubaini nini kilitokea.
Kwa upande wake Mganga mfawidhi Hospitali ya rufaa mkoa Dkt. Athanas Ngambakubi amekiri kumpokea mtoto huyo, ambaye amesema alikuwa na jereha kubwa katika sehemu yake ya siri.
Dkt. Ngambakubi amesema kuwa jeraha hilo lilisababisha kutoka kwa baadhi ya viungo vya ndani ya mwili (Utumbo Mkubwa), ambapo baada ya kufikishwa hospitalini hapo walimfanyia huduma ya upasuaji mkubwa na kufanikiwa kurejesha viungo hivyo.
“Tumechukua vipimo vyote vinavyohitajika ili kujua ni nini kilitokea, kwa sasa hatuwezi kusema chanzo cha tukio hilo mpaka pale majibu ya vipimo yakitoka, ila kwa sasa amepatiwa matibabu na anaendelea vizuri” amesema Dkt. Ngambakubi..