Leo katika kufatilia taarifa ya habari katika kituo kimoja cha television hapa nyumbani, imeonesha Mkaguzi Mkuu wa hesabu wa Serikali amekabidhi ripoti yake kwa Mh. Rais ikulu.
Katika makabidhiano hayo, Rais ameenda mbali zaidi na kumpa kazi nyingingine, "akimtaka" Mkaguzi huyo akakague migodi ya madini na aje na ripoti ya kuonesha taifa/serikali ina nufaika vipi na mchanga unaosafirishwa kwenda nje.
Mbali na kumuagiza huko, Rais kasema kwamba, ataunda tume nyingine ichunguze suala hili hilo, na ataunda "timu" nyingine hisiyojulikana (invisible team) kuchunguza jambo hilo hilo pia.
Sasa hapa najiuliza, kuna ulazima gani tena Rais aunde tume na invisible team, wakati ameishamwagiza CAG kufanya jambo hilo?
What if, kama hiyo tume na team zikaja na majibu tofauti na ya CAG?
Je Kazi anayofanya CAG haiaminiki kwa serikali au Rais ndio hana imani na CAG?
Taasisi ina macho ila rais kajipofusha.
Angetumia macho angeweza kuina Bashite galasha.
Hatuwezi kuota. Magufuli kaweka kodi mpaka ya ndoto tunabana matumizi.Bashite kawashika patamu sana.
Hamumuoti?
Hatuwezi kuota. Magufuli kaweka kodi mpaka ya ndoto tunabana matumizi.
mkuu upo sahihi inaonyesha dhahiri kuwa mwenye nchi hana mahusiano mazuri na mkaguzi mkuu wa serikali (hana imani nae).Inaweza kuwa mbinu nzuri, ila inategemea inatumika Je, na wakati gani?
Kwa hili mpaka kumuambia moja kwa moja kuwa kafanye hivi ila na mimi nitafanya hivi kujua nilichokuambia ukafanye kuona kama kipo sawa, sidhani kama ni sahihi. Kwanza unaonesha wazi pengine huna imani na ninachofanya au nifanye iwapo ikitokea nimekosea sehemu basi ndio itumike kama sehemu ya kunisemea.
CAG ni muislamu................... Hachomoki Kwa mtego huu. Ni enzi ya Pombe
Magufuli yeye ni bunge, mahakama, serikali ya mitaa na mpaka kanisa.Si kweli.
Magufuli hawezi kuweka sheria mpya bila kuipitisha hiyo sheria bungeni. Sijaona kodi yoyote mpya.
Sema upinzani hamna hoja ya siasa mlichobaki nacho ni hoja za kurukia, mnataza wapi kuna uoenyo ndiyo mnabwabwaja.
Nnashangaa sana pale nnapoona upinzani unakosa mawazo mapya (ideas), unakosa hata kuongolea matukio (events) unabaki kuongelea watu.
Hoi.
Only in God we trust...Inaweza kuwa mbinu nzuri, ila inategemea inatumika Je, na wakati gani?
Kwa hili mpaka kumuambia moja kwa moja kuwa kafanye hivi ila na mimi nitafanya hivi kujua nilichokuambia ukafanye kuona kama kipo sawa, sidhani kama ni sahihi. Kwanza unaonesha wazi pengine huna imani na ninachofanya au nifanye iwapo ikitokea nimekosea sehemu basi ndio itumike kama sehemu ya kunisemea.
Tatizo, kama ulivyosema, anataka kujiridhisha yeye badala ya kuridhisha wananchi.Mimi naona raisi yupo katika mkakati mzuri na nia yake ni kutaka kujiridhisha tu.
Haina ubaya
Umechangia mini sasa hapa!?Hapa kazi tu
Ni kwamba wahusika wasidanganye na amewajulisha hilo kihivyo.
Magufuli oyeeeeeee
Rais makini wakati wote huweka msisitizo kuonesha kazi hiyo ni muhimu. Hapa sio issue ya kuaminiana bali ni kulinda maslahi ya Taifa. Na kama CAG yupo tentative lazima atakwenda kufanya kazi bora zaidi. Mazoea ya kuaminiana ndiyo yamefanya nchi imekuwa na ulaji na walaji kila kona. Ni mjinga pekee anayeweza kuhoji ubora wa Rais tuliyenaye Tanzania kwasasa. Ukifuatilia kwa makini utaona wanaohoji ni wale waliokuwa kwenye mtandao wa kuifanyia maovu nchi yetu Tanzania. Either wapiga deals haramu au wauza unga. You are no more. Go to hell. Leave our country alone.
Magufuli yeye ni bunge, mahakama, serikali ya mitaa na mpaka kanisa.
Sijui unaongelea bunge gani wakati kashaliamrisha bunge litunie fedha za tafrija yake kwenye habari za hospitali.
Utaongelea mahakama gani wakati Magufuli kahutubia Mahakama na kuipangia kazi.
Utaongelea serikali za mitaa gani wakati Magufuli kaenda kwa Mzee wa Upako na kuaguza barabara itengenezwe.
Anaenda kanisani na kutoa hotuba ya kisiasa mbele ya kanisa.
Na juzi kaingikia mpaka wasanii anaaanza kuwapangia mistari ya kuandika kwenye nyimbo zao.
Sasa hivi ataomba atoe single na Ney wa Mitego.