Mtazamo: Kanda ya Kaskazini, CCM imechokwa mpaka basi!

Pasco,

..Kigoma ndiyo mkoa wa kwanza kuchagua mbunge toka upinzani, Dr.Walid Amani Kaborou alipokuwa CDM.

..pia mkoa huo umeendeleza rekodi yake ya kuchagua wabunge wa upinzani ktk kila uchaguzi.

..kinachonishangaza ni kuona kwamba Kigoma hawaandamwi kwa kuikataa CCM, kama inavyotokea kwa mikoa ya Kilimanjaro na Arusha.

..kwanini hatusikii shutuma za "Wakigoma/Ukigoma" au "Umagharibi" bali tunasikia "Ukilimanjaro" na "Ukaskazini"??

NB:

..Pasco anatetea na kushabikia ubaguzi akidai kwamba ni "facts"!!

LOL ... Kigoma inatakiwa iwe ngome ya NCCR, japo wapiga debe la u-kanda wanashindwa namna ya kui-justify na hasa ukizingatia kwamba Mwenyekiti wa NCCR anatokea Kaskazini.
 
Mkuu JokaKuu,

Hapo kwenye red na nimeongezea mkolezo, Prof. Malekela wa Kitivo cha Elimu pale UD (sijui kama bado yupo) aliwahi kufanya utafiti kuhusu quota system elimu ya sekondari. Anasema alikutana na vituko vingi sana: Kuna wanafunzi unakuta ana sir name inayotambulisha kwamba anatokea kabila fulani, lakini ukimuuliza anakuambia yeye ni kabila jingine. Wako watu kibao walikuwa wana majina kiislam lakini ni wakristo. Katika utafiti alikuja akagundua kwamba wanafunzi wa ukanda fulani wakimaliza shule na kutochaguliwa kwenda sekondari, walikuwa wakihamia shule za msingi za ukanda mwingine na kwenda kurudia darasa 6 au 7 kwa kutumia majina ya wanafunzi walio drop out kwenye ukanda huo and finally anakuja kuchaguliwa kwenda sekondari.

Quota system in a way haikuwa effective kama walivyotarajia na pia imesaidia kunyima fursa wanafunzi wenye uwezo darasani na wengine kucheleweshwa kwa kupita njia ndefu za kwenda kurudia shule za mikoa mingine.

Keil,

..LOL!!

..this is true story. mimi nilikutana na jamaa mmoja "mkaskazini" anatumia jina la ubini wa the real pasco!!

..Pasco mtafute huyu "nduyu yako ktk quota system" mjuane!!!
 
Nyie watu wa Kanda ya Kaskazini, msiichukie hivyo CCM, kwani pamoja na mabaya yake, pia kuna mema mengi imelifanyia taifa hili!.

haya ni maneno ya Pasco, inaonyesha alivyo na chuki na atu wa kanda ya kaskazini ...nimekudharau sana , ficha upumbavu wako......

kuna mahali pengine anasema kuwa kuna watu wa kanda fulani hawawezi kuwa marais .... huu nao ni ujinga wa kufichwa .........
 
Kwenye siasa kuna kitu kinaitwa ngome. Ngome ndipo pale ambapo umeota mizizi na unapoanzishia cheche ya moto wa nyika yako ambapo utasambaa!.

CUF wana ngome yao na mtaji wao waliowekeza na ndio maana wanavuna walichopanda!. CDM nao wana ngome yao na mtaji wao ni watu. CCM kwa vile kilikuwa chama tawala chenyewe kote ni ngome zake na mtaji wake ni mtandao wake ulioenea hadi vijijini. Ili kuleta mageuzi ya kweli ni lazima waokombe huo mtaji wa CCM na ili kuukomba lazima moto wako ukauanzishie kwenye ngome yako ndipo usambae kote!.

Lets face the bitter truth kwa kumeza the bitter pill ili kuutibu huu ugonjwa wa ukanda, udini na ukabila!.

Mimi binafsi ni muumini wa ukweli na hivyo naamini ukanda, ukabila na udini, upo kwenye siasa za Tanzania na dawa yake ni to set a thief to catch a thief, tuutumie ukabila huo huo, udini huo huo na ukanda huo huo kuutibu ugonjwa huo huo!.

Pasco!.

Mkuu Pasco,

Hoja yako ya Vyama vya Ukanda, Udini na Ukabila, sidhani kama ina mashiko. Najua conclusion yako inakoelekea kwamba given maelezo yako, ni CCM pekee ndio ambayo imesambaa nchi nzima na haina udini, ukanda wala ukabila na ndio maana ukasema kwamba CCM ina ngome nchi nzima!

Soma politics za Afrika, vyama vingi vya upinzani huwa vinaanzia mijini then vinasambaa kwenda vijijini, especially kwa nchi ambazo zimetawaliwa na mfumo wa chama kimoja kwa miaka mingi. Ushindi wa KANU ulikuwa unatoka vijijini, same applies kwa Mugabe, na hata CCM kwa sasa. Unadhani ni kwanini matokeo ya uchaguzi wa 1995 ya mkoa wa Dar es Salaam yalifutwa?

Mwaka 1995, sehemu nyingi ambazo NCCR walishinda au wapinzani walifanya vyema ilikuwa ni majimbo ya mijini. Reason iko simple, miundombinu ya mijini inaruhusu wagombea au vyama vya siasa kuwafikia wapiga kura wengi kwa gharama nafuu ukilinganisha na majimbo yenye miundombinu mibovu ambako ni gharama kubwa kuwafikia wapiga kura.

Ndio maana unakuta sehemu kama Arusha Mjini, Mwanza Mjini (Nyamagana na Ilemela), Shinyanga Mjini, Sumbawanga Mjini, Mpanda Kati. Iringa Mjini, Mbeya mjini, Lindi mjini, Musoma mjini, sehemu zote hizo asilimia kubwa ya wapiga kura wako accessible na ni rahisi kuwafikia. Sasa kwenye orodha hiyo naomba uniambie ukanda uko wapi?

Hivi ngome ya chama inaweza kuwa na mbunge mmoja tu wa kuchaguliwa mkoa mzima wa Arusha wenye majimbo 7? Au wabunge 3 tu mkoa wa Kilimanjaro wenye majimbo 9, au wabunge 2 wa kuchaguliwa kutoka mkoa wa Manyara wenye majimbo karibu 9? Au labda ni mimi ndiye ambaye sielewi maana ya neno "ngome"?

Pattern ya ushindi kwenye hayo majimbo haina tofauti na pattern ya ushindi kwenye majimbo mikoa mingine; ambayo ni ama majimbo yawe mjini au mtu binafsi anaweka network yake.

Wapinzani wengi wamekuwa wakilenga majimbo ambayo yanafikika kirahisi ambayo mengi yako maeneo ya mijini na pia yana eneo dogo. Majimbo mengine wanayoshinda wapinzani au kutoa upinzani mkali ambayo yako vijijini ni majimbo ambayo unakuta kuna juhudi za mgombea binafsi katika kuweka network mfano Mbozi Magharibi na Mashariki, Kilombero, Tandahimba, Iramba Mashariki, majimbo ya mkoa wa Kigoma na kwingineko ni juhudi binafsi za wagombea wenyewe katika kuweka mtandao.

Kwa hiyo hoja ya ngome mimi siioni na wala haina mantiki.
 
mkuu Pasco acha analysis za ki ccm, pale iringa mjini, mbeya mjini sumbawanga mlikoiba kura, songea mjini mliiba kura mbona hujataja km ni ngome ya upinzani, wewe ni mtu hatari sana comments zako zimejaa ubaguzi mtupu. Watu km nyie ndo mlioleta ubinafsi ccm. Ccm inachukiwa kwa kuwasahau na kutowajibika kwa wananchi na si kwa wapi viongozi wake wanatoka. Nyerere alishatuasa tuwaogope watu km nyie km UKOMA
 
Wajameni, hizi siasa za udini, ukabila na ukanda are they real au ni dhana tuu?.

Jee Watanzania si wana dini zao?, jee kuna ubishi kuwa alipoanza rais Mkristu, JK Nyerere, alipoondoka Mwinyi aliingia tuu by chance?. No miongoni mwa sababu za Mwinyi kuingia ni pamoja na dini yake, this is a fact!. Alipoondoka Mwinyi sialiingia Ben, inamaana aliingia tuu by a mare chance and by chance akawa ni Mkiristu na alipotoka JK nae akaingia by mare chance, na by chance akawa ni Mwislam?. Tutake tusitake, kuna kupokezana hata kama ni by chance, then tuendelee ku play by chance!. Niiteni mdini, ila ukweli ndio huu!.

Jee Watanzania hawana makabila yao?, Lazima tukubali tukatae, Tanzania kuna dorminant tribes na makabila madogo madogo. Kati ya hizi dorminant tribes lazima tukubali kuna baadhi yake wana ukabila wa kutisha!, kuna baadhi yake wana nyodo za ajabu!, kwani iliwahi kutamkwa au kuandikwa popote kuwa watu wamakabila fulani sio hawafai kuchukua urais wa nchi hii, bali hawawezi kupewa kwa sababu matokeo tunayajua!, hivi tuu walivyo na hizo nafasi kubwa kubwa tayari ni miungu watu, wakiukwaa urais si ndio wataota pembe kabisa!. Ni general unwritten public opinion kuwa rais wa nchi hii asitokee kwenye hizi dorminant tribes!. Niiteni mkabila lakini ukweli ndio huu!

Jee Watanzania hawana kanda zao?. JK Nyerere alitoka kanda ya Ziwa, Mwinyi akatoka Zanzibar, Ben akatoka kanda ya Kusini, JK ametoka kanda ya Mashariki, Kanda ya kati by now haina mtu mwenye uwezo wa urasi kwa sasa (sorry), hivyo kanda iliyobakia ambayo haijatoa rais ni Kanda ya Kaskazini!, hivyo rais wa 2015 lazima atoke Kaskazini!. Niiteni Mbaguzi wa ukanda ila huu ndio ukweli wenyewe!.

Juzi nilipandisha hii thread iliyosema "Kanda ya Kaskazini CCM imechokwa mpaka Basi", nilishambuliwa sana kwa siasa za ukanda ili this is a fact!. Nikasisitiza CCM haina namna yoyote ya kujiokoa ili ipendeke na kutoa angalizo kuwa majaaliwa ya CCM kuendelea kutawala nchi hii, yanashikiliwa na kanda ya Ziwa, hivyo nikasema kama ikitokea na Kanda ya Ziwa wakaichoka CCM kama walivyochoka kanda ya Kaskazini, 2015 CCM inapigwa chini, kichwa chini miguu juu huku mnashuhudia bila kuamini macho yenu wala masikio yenu!.

Hii dhambi ya mbegu ya sumu ya siasa za udini, ukabila na ukanda, zimepandwa na CCM, zimelelewa na CCM na hatimaye 2015, CCM itavuna ilichopanda!.

Nilisisitiza, hatuwezi kupiga vita siasa za ukanda, za udini na za ukabila kwa denial, bali kwa facing them!.

Pasco
 
Wanabodi, Siku zote nimekuwa nikisema humu, CCM imekuwa ikichaguliwa na wengi sio kwa sababu ya kupendwa au kukubalika sana, bali kwa mazoea tuu wengi wakiwa ndicho chama pekee walichokifahamu tangu wamezaliwa, na wengine wakikichagua CCM kama asante ya kutuletea uhuru kupitia TANU, na idadi kubwa ya walio vijijini, wamekuwa wakiichagua CCM kwa ignorance tuu ya elimu ya uraia!. Sasa wale wanaichagua CCM kama asante ya kutupatia uhuru, ni oldguard, wanazidi kupungua na wachache waliobakia they days are numbered!. Wale wengi waliokuwa wakiichagua kwa ignorance, sasa wameamka!.Kama kasi ya upepo wa mwamko kama Kanda ya Kaskazini, utaingia kanda ya Ziwa kwa kasi hiyo hiyo, then hakuna jinsi yoyote ya kuiokoa CCM isipigwe mwereka uchaguzi wa 2015!.Determinant ya nani anakuwa rais wa nchi hii, ni wapiga kura wa Kanda ya Ziwa ambayo ndiyo inayoongoza kwa idadi kubwa ya watu!. Kati ya watu milioni 40 wa sensa ya mwaka 2002 kwa Tanzania yenye makabila 120, Wasukuma peke yao wako milioni 6!. Sasa ukiwajumlisha na Kanda ya Kaskazini, hata kama mikoa yote iliyobakia wataipigia kura CCM, bado kwa kanda hizo mbili pekee, zinatosha kabisa kuipiga chini CCM!. Mwelekeo huu ni uthibitisho kuwa ukombozi wa kweli wa pili wa Mtanzania, sio ndoto tena, ni kitu ambacho kinawezekana!.Natoa mwito kwa Watanzania wenye mapenzi mema na nchi yetu, tusiendekeze hizi siasa za chuki za kukichukia chama fulani bila sababu za msingi ya chuki hiyo, au kukipenda na kikishabikia chama fulani kwa upenzi tuu, matokeo ya mwisho ya siasa hizi ni kujengeana chuki zisizo na sababu!. Tupingane bila kupigana, tutofautiane kisiasa bila kuchukiana bali tupingane huku tukipendana!.Namalizia kwa kusisitiza, huu ni mtazamo tuu!Wasalaam.Pasco.
Nafanya mapitio ya matokeo ya sensa kikanda, ili kupima idadi ya watu kwenye baadhi ya kanda na mwelekeo wao kisiasa, ili kuangalia uwezekano wa kuwezekanika wa kupatikana mabadiliko ya kweli, 2015, au mambo ni yale yale!.Pasaka Njema,Pasco.
 
Zimwi la udini lifanyieni kazi kuna watu wanaichukia chadema kwa hisia hii tu
 
Pasco heshima kwako mkuu, unaonyesha kuwa hujajua kwa nini watu wa kizazi hiki wengi hawaipendi na wanaichukia CCM. Chama hiki kimejijengea maadui chenyewe kwa kuweka viongozi wa aina ya Mwigulu,Nape, Lusinde hata na Wassira. Hivi unadhani mwananchi wa kawaida toka kwa mfano Kilimanjaro na ni mpenzi au mwanachama wa CCM halafu anasikia zile kauli za kila siku kuwa Chadema ni chama cha Wachaga na kuwa wachaga sio watu wakuaminika katika nchi hii?
Kauli na matendo ya hawa viongozi vijana wa CCM yameijengea chuki,bahati mbaya kwa CCM mwenyekiti ndio mwisho wa maneno,akikupenda yeye basi hata uwe bogas kiasi gani hakuna wa kukutoa. Mfano Mwigulu,huyu kwelikwa yote aliyo yafanya alistahili kweli kuendelea kushika hata wazifa kwenye kata?
CCM imejiua na inaendelea kujiua yenyewe. Ndugu yangu Pasco kukisaidia chama hiki ni kukiruhusu kife haraka ili kiepuke kifo cha mateso.
 
Wanabodi,

Kama kawaida yangu, nipatapo fursa, hupita huku na kule na kubadilishana mawazo na watu mbalimbali wa kada tofauti. Kwa takriban siku 3 zilizopita, nimepata fursa ya kutembelea mikoa ya Kilimanjaro na Arusha ambayo ndiyo inayo dorminate Kanda ya Kaskazini, kiukweli CCM Imechokwa mpaka basi!.

Siku zote nimekuwa nikisema humu, CCM imekuwa ikichaguliwa na wengi sio kwa sababu ya kupendwa au kukubalika sana, bali kwa mazoea tuu wengi wakiwa ndicho chama pekee walichokifahamu tangu wamezaliwa, na wengine wakikichagua CCM kama asante ya kutuletea uhuru kupitia TANU, na idadi kubwa ya walio vijijini, wamekuwa wakiichagua CCM kwa ignorance tuu ya elimu ya uraia!. Sasa wale wanaichagua CCM kama asante ya kutupatia uhuru, ni oldguard, wanazidi kupungua na wachache waliobakia they days are numbered!. Wale wengi waliokuwa wakiichagua kwa ignorance, sasa wameamka!.

Kwa mujibu wa kada mbalimbali nilozungumza nao, wamethibitisha kuwa hakuna jinsi Ole Sendeka, Ole Medeye na Ole Nyaguro wataweza kusalimika, sehemu salama mpaka sasa ni Jimbo la Monduli tuu!.

Kama kasi ya upepo wa mwamko kama Kanda ya Kaskazini, utaingia kanda ya Ziwa kwa kasi hiyo hiyo, then hakuna jinsi yoyote ya kuiokoa CCM isipigwe mwereka uchaguzi wa 2015!.

Determinant ya nani anakuwa rais wa nchi hii, ni wapiga kura wa Kanda ya Ziwa ambayo ndiyo inayoongoza kwa idadi kubwa ya watu!. Kati ya watu milioni 40 wa sensa ya mwaka 2002 kwa Tanzania yenye makabila 120, Wasukuma peke yao wako milioni 6!. Sasa ukiwajumlisha na Kanda ya Kaskazini, hata kama mikoa yote iliyobakia wataipigia kura CCM, bado kwa kanda hizo mbili pekee, zinatosha kabisa kuipiga chini CCM!.

Mwelekeo huu ni uthibitisho kuwa ukombozi wa kweli wa pili wa Mtanzania, sio ndoto tena, ni kitu ambacho kinawezekana!.

Natoa mwito kwa Watanzania wenye mapenzi mema na nchi yetu, tusiendekeze hizi siasa za chuki za kukichukia chama fulani bila sababu za msingi ya chuki hiyo, au kukipenda na kikishabikia chama fulani kwa upenzi tuu, matokeo ya mwisho ya siasa hizi ni kujengeana chuki zisizo na sababu!. Tupingane bila kupigana, tutofautiane kisiasa bila kuchukiana bali tupingane huku tukipendana!.

Hata mimi uchaguzi wa Arumeru, nilisimama na Sioi, tumekutana na Nasari pale Dodoma, tumekumbatiana, na kiukweli kutoka moyoni mwangu, sina chuki na Nasari, namkubali kwa dhati japo namhurumia Sioi kwa sababu ni rafiki!.

Nyie watu wa Kanda ya Kaskazini, msiichukie hivyo CCM, kwani pamoja na mabaya yake, pia kuna mema mengi imelifanyia taifa hili!.

Namalizia kwa kusisitiza, huu ni mtazamo tuu!

Wasalaam.

Pasco
Arusha.

Kwa namna hii lazma tuwe waviv wa kusoma,maneno meengi kumbe upumbav kbsa,unaeneza chuki na ghilliba za kikanda..huna hata aibu mtoto wa kiume,kichaa kbsa
 
Uelewa/ufahamu, maendeleo kwa ujumla ndiyo vitu vinafanya kanda ya kaskazini wawe aware na kila kitu kinachofanywa na CCM na Serikali yake.

Ukimuangalia Nchemba, yeye anaweza kwenda kuwadanganya wana Iramba kwa kuwapa T-shirts n kofia akawaambia hayo ni maendeleo na wakakubali 100% lkn watu hao hawana huduma muhimu kama maji, elimu, afya, miundombinu etc. Hapa ndiyo CCM inapotaka kwa sababu huu ndiyo mtaji wake. Mwananchi azidi kuwa maskini uchaguzi ukikaribia analeta pilau(chakula) kwa sababu mna njaa na hamna uelewa wowote mnakula na kura mnampa kwa kumuona huyu ndiyo mkombozi.
Kumbe ukombozi ni kiakili, fikra sahihi ya mwanadamu anavyotakiwa kuishi.

Sasa bwana Pasco kaskazini wana ukombozi wa kiakili na kifikra since before CCM ndiyo maana CCM hawawataki watu wa Kaskazini(siyo kaskazini ni Kilimanjaro especially Wachaga) kwa sababu pale hawana mtaji.
Nadhani bwana Pasco umeshawasikia sana wakisema 'Chama cha Wachaga' 'Chama cha wakristo' sasa ukijiuliza kama wewe unaweza kutengwa kichama, kikabila, kidini ndani ya nchi yako kwanini na wewe usijitenge na huyo anayekutenga?

Ukabila, udini, uchama wameuleta wao CCM ktk jamii Sasa ukombozi wa kifikra unasambaa nchi nzima na mud si mrefu wataanzisha kujitenga na watu wa mkoa/kanda nyingine kwa kusingizia udini/ukabila/uchama.

Sasa wanachokitafuta nadhani mmeshaanza kukiona, mfa maji haachi kutapatapa. mengi yanakuja.
 
Wanabodi,

Kama kawaida yangu, nipatapo fursa, hupita huku na kule na kubadilishana mawazo na watu mbalimbali wa kada tofauti. Kwa takriban siku 3 zilizopita, nimepata fursa ya kutembelea mikoa ya Kilimanjaro na Arusha ambayo ndiyo inayo dorminate Kanda ya Kaskazini, kiukweli CCM Imechokwa mpaka basi!.

Siku zote nimekuwa nikisema humu, CCM imekuwa ikichaguliwa na wengi sio kwa sababu ya kupendwa au kukubalika sana, bali kwa mazoea tuu wengi wakiwa ndicho chama pekee walichokifahamu tangu wamezaliwa, na wengine wakikichagua CCM kama asante ya kutuletea uhuru kupitia TANU, na idadi kubwa ya walio vijijini, wamekuwa wakiichagua CCM kwa ignorance tuu ya elimu ya uraia!. Sasa wale wanaichagua CCM kama asante ya kutupatia uhuru, ni oldguard, wanazidi kupungua na wachache waliobakia they days are numbered!. Wale wengi waliokuwa wakiichagua kwa ignorance, sasa wameamka!.

Kwa mujibu wa kada mbalimbali nilozungumza nao, wamethibitisha kuwa hakuna jinsi Ole Sendeka, Ole Medeye na Ole Nyaguro wataweza kusalimika, sehemu salama mpaka sasa ni Jimbo la Monduli tuu!.

Kama kasi ya upepo wa mwamko kama Kanda ya Kaskazini, utaingia kanda ya Ziwa kwa kasi hiyo hiyo, then hakuna jinsi yoyote ya kuiokoa CCM isipigwe mwereka uchaguzi wa 2015!.

Determinant ya nani anakuwa rais wa nchi hii, ni wapiga kura wa Kanda ya Ziwa ambayo ndiyo inayoongoza kwa idadi kubwa ya watu!. Kati ya watu milioni 40 wa sensa ya mwaka 2002 kwa Tanzania yenye makabila 120, Wasukuma peke yao wako milioni 6!. Sasa ukiwajumlisha na Kanda ya Kaskazini, hata kama mikoa yote iliyobakia wataipigia kura CCM, bado kwa kanda hizo mbili pekee, zinatosha kabisa kuipiga chini CCM!.

Mwelekeo huu ni uthibitisho kuwa ukombozi wa kweli wa pili wa Mtanzania, sio ndoto tena, ni kitu ambacho kinawezekana!.

Natoa mwito kwa Watanzania wenye mapenzi mema na nchi yetu, tusiendekeze hizi siasa za chuki za kukichukia chama fulani bila sababu za msingi ya chuki hiyo, au kukipenda na kikishabikia chama fulani kwa upenzi tuu, matokeo ya mwisho ya siasa hizi ni kujengeana chuki zisizo na sababu!. Tupingane bila kupigana, tutofautiane kisiasa bila kuchukiana bali tupingane huku tukipendana!.

Hata mimi uchaguzi wa Arumeru, nilisimama na Sioi, tumekutana na Nasari pale Dodoma, tumekumbatiana, na kiukweli kutoka moyoni mwangu, sina chuki na Nasari, namkubali kwa dhati japo namhurumia Sioi kwa sababu ni rafiki!.

Nyie watu wa Kanda ya Kaskazini, msiichukie hivyo CCM, kwani pamoja na mabaya yake, pia kuna mema mengi imelifanyia taifa hili!.

Namalizia kwa kusisitiza, huu ni mtazamo tuu!

Wasalaam.

Pasco
Arusha.
Baada ya kuiposti hii kitu miaka miwili iliyopita, uthibitisho sasa ndio huu unaanza kujitokeza!.
Hizi ni habari ambazo nimezipokea kwenye text

Mgombea wa ccm Kiboroloni ametangaza kujitoa kwenye kinyang'anyiro leo
Pasco
 
Pamoja na haki yako ya mtazamo tu, mimi huangaliaga ndani ya mistari; ujumbe unaoutoa una taswira mbili.

1. Hukutegemea kuwa kanda unazozitaja zinaweza kuigeuka CCM

Jibu langu kwa hili weka kinyume CCM imewageuka watanzania kwa kuwasahau kabisa katika maisha yao ya kila siku. Kwa hiyo CCM imetoa elimu kwa makusudi isiaminiwe kwa mifano hai ya kuwapora imani na mategemeo waliyokuwa nayo watanzania. NAKUHAKIKISHIA SI UKANDA angalia Tandahimba ni kanda gani?

2. Unatafuta suluhisho la maovu ya CCM yaliyojenga chuki.

Hapo nawaelewa Watanzania kuwa ni wanadamu wakawaida viumbe wa Mungu waliojaliwa uelewa na hiari ya kusema SASA BASI baada ya kufanyiwa waliofanyiwa na CCM ambayo unayajua vema.

Uchambuzi wangu

Chaguzi zote hadi sasa kuna neno mvuto linajitokeza, mimi najifunza kuwa linahusu wajihi zaidi kuliko dhamira ya uwajibikaji. Wajihi huchujuka kama ua nadhani ndiyo yanayoipata CCM. Dhamira ya uwajibikaji inahusisha ahadi na matendo; wazungu wanasema TO WALK THE TALK. Hiki ndicho kinakosekana kwa CCM (labda na wewe) kwa sababu ukichulia kuwapa matumaini watu juu ya maisha bora halafu kila siku inakuwa afadhali ya jana nani atavumilia?

Mifano mingi sana mishahara midogo na tofauti kati ya wafanyakazi, wakulima kuhujumiwa na wafanyabiashara wa kati kwa msaada wa utawala wa CCM huna haja ya kutambulishwa kumjua mbaya ni nani.

Kwa kiwango CCM ilipofikia hata ukienda nyumba kwa nyumba kutoa maelezo yako utasikilizwa na sikio la kushoto yatatokea sikio la kulia kwa kukosekana WALKING THE TALK. Kusini mwa TZ wanapokudharau ni pale kauli zako zisipoendana na matendo yako.

Kauli za CCM na hata wewe Pasco mziainishe na kuzilinganisha na matendo yenu. Hata angalau mseme mnaweza nini na hamuwezi nini maana kwa sasa mmebakia kuhodhi dola mnachoongea tofauti na mnachoweza kufanya. Wenye akili wamewagundua kuwa ni ...................
Nadhani Pasco aisome vizuri hiyo,yake ina mapungufu,imekosa uchambuzi linganifu,Amekosa kutujuza Mtanzania anawaza nini kuhusu ccm.Mporomoko wa ccm huu umetokana na nini,napengine nini hatima yake
 
Wanabodi,

Kama kawaida yangu, nipatapo fursa, hupita huku na kule na kubadilishana mawazo na watu mbalimbali wa kada tofauti. Kwa takriban siku 3 zilizopita, nimepata fursa ya kutembelea mikoa ya Kilimanjaro na Arusha ambayo ndiyo inayo dorminate Kanda ya Kaskazini, kiukweli CCM Imechokwa mpaka basi!.

Siku zote nimekuwa nikisema humu, CCM imekuwa ikichaguliwa na wengi sio kwa sababu ya kupendwa au kukubalika sana, bali kwa mazoea tuu wengi wakiwa ndicho chama pekee walichokifahamu tangu wamezaliwa, na wengine wakikichagua CCM kama asante ya kutuletea uhuru kupitia TANU, na idadi kubwa ya walio vijijini, wamekuwa wakiichagua CCM kwa ignorance tuu ya elimu ya uraia!. Sasa wale wanaichagua CCM kama asante ya kutupatia uhuru, ni oldguard, wanazidi kupungua na wachache waliobakia they days are numbered!. Wale wengi waliokuwa wakiichagua kwa ignorance, sasa wameamka!.

Kwa mujibu wa kada mbalimbali nilozungumza nao, wamethibitisha kuwa hakuna jinsi Ole Sendeka, Ole Medeye na Ole Nyaguro wataweza kusalimika, sehemu salama mpaka sasa ni Jimbo la Monduli tuu!.

Kama kasi ya upepo wa mwamko kama Kanda ya Kaskazini, utaingia kanda ya Ziwa kwa kasi hiyo hiyo, then hakuna jinsi yoyote ya kuiokoa CCM isipigwe mwereka uchaguzi wa 2015!.

Determinant ya nani anakuwa rais wa nchi hii, ni wapiga kura wa Kanda ya Ziwa ambayo ndiyo inayoongoza kwa idadi kubwa ya watu!. Kati ya watu milioni 40 wa sensa ya mwaka 2002 kwa Tanzania yenye makabila 120, Wasukuma peke yao wako milioni 6!. Sasa ukiwajumlisha na Kanda ya Kaskazini, hata kama mikoa yote iliyobakia wataipigia kura CCM, bado kwa kanda hizo mbili pekee, zinatosha kabisa kuipiga chini CCM!.

Mwelekeo huu ni uthibitisho kuwa ukombozi wa kweli wa pili wa Mtanzania, sio ndoto tena, ni kitu ambacho kinawezekana!.

Natoa mwito kwa Watanzania wenye mapenzi mema na nchi yetu, tusiendekeze hizi siasa za chuki za kukichukia chama fulani bila sababu za msingi ya chuki hiyo, au kukipenda na kikishabikia chama fulani kwa upenzi tuu, matokeo ya mwisho ya siasa hizi ni kujengeana chuki zisizo na sababu!. Tupingane bila kupigana, tutofautiane kisiasa bila kuchukiana bali tupingane huku tukipendana!.

Hata mimi uchaguzi wa Arumeru, nilisimama na Sioi, tumekutana na Nasari pale Dodoma, tumekumbatiana, na kiukweli kutoka moyoni mwangu, sina chuki na Nasari, namkubali kwa dhati japo namhurumia Sioi kwa sababu ni rafiki!.

Nyie watu wa Kanda ya Kaskazini, msiichukie hivyo CCM, kwani pamoja na mabaya yake, pia kuna mema mengi imelifanyia taifa hili!.

Namalizia kwa kusisitiza, huu ni mtazamo tuu!

Wasalaam.

Pasco
Arusha.
Hii ilikuwaga kanda ya Kaskazini,
leo nimesoma mahali hii kitu kuhusu matokeo ya chaguzi wa serikali za mitaa Mkoani Lindi!.

CUF mitaa 35, CCM 53, CDM 16, NCCR 5 name TLP 1 kwa ujumla wpinzani wamefanya vizuri katika uchaguzi huu kwa kupata jumla ya viti 58 dhidi ya 53 vya ccm.
 
Pasco unafikiria wameichukia tu kama mama mjamzito anavyoweza kuchukia tu mtu??? nafurahi kwanza kwamba umeandika uzi huu, lakni ni ukweli kuwa CCM imekera hadi watoto, maana dawa hospitalini hazibagui mtoto au mtu mzima, maabara, madawati, walimu wenye sifa na morale ya kufundisha hakuna kutokana na kupunjwa mshahara, kutolipwa kwa wakati madai yao, uchumi umekuwa wa kina fulani na fulani, wizi wa mali ya umma mchana kweupe, rais kufanya mzaha na mali za umma kama ambavyo aliona ni vyema asema kuhusu tezi dume ambao sio yeye tu ameugua duniani achilia mbali TZ, badala ya kusema neno airport kuhusu wezi anaongelea ugonjwa wake utadhani nchi ni yake binafsi, Pinda kushabikia polisi wapige tu watu ambao wanadai haki eti wanakaidi amri halali, hata kulinda mafisadi ni amri halali??? sio TZ, hali hii ya kutojali hisia za waatanzania imetufikisha hapo, tuache tupumue kwa kuikataa CCM hatuna namna ndo njia ya kuishi maisha mapya.
 
Naona unathibitisha maneno ya Marealle aliyoitoa miaka ile kule UN kuwa Kanda ya Kaskazini wako tayari kujitawala lakini kanda zingine zinachechemea!!! 50 year plus down the road maneno yake yanatimia na ndoto ya Tanzania tunayoitaka inaanza kunukia... Itoshe kusema Mungu ni Mwema... akiamua jambo lake lazima litimie "KUN FAYA KUN" ...

Wanabodi,

Kama kawaida yangu, nipatapo fursa, hupita huku na kule na kubadilishana mawazo na watu mbalimbali wa kada tofauti. Kwa takriban siku 3 zilizopita, nimepata fursa ya kutembelea mikoa ya Kilimanjaro na Arusha ambayo ndiyo inayo dorminate Kanda ya Kaskazini, kiukweli CCM Imechokwa mpaka basi!.

Siku zote nimekuwa nikisema humu, CCM imekuwa ikichaguliwa na wengi sio kwa sababu ya kupendwa au kukubalika sana, bali kwa mazoea tuu wengi wakiwa ndicho chama pekee walichokifahamu tangu wamezaliwa, na wengine wakikichagua CCM kama asante ya kutuletea uhuru kupitia TANU, na idadi kubwa ya walio vijijini, wamekuwa wakiichagua CCM kwa ignorance tuu ya elimu ya uraia!. Sasa wale wanaichagua CCM kama asante ya kutupatia uhuru, ni oldguard, wanazidi kupungua na wachache waliobakia they days are numbered!. Wale wengi waliokuwa wakiichagua kwa ignorance, sasa wameamka!.

Kwa mujibu wa kada mbalimbali nilozungumza nao, wamethibitisha kuwa hakuna jinsi Ole Sendeka, Ole Medeye na Ole Nyaguro wataweza kusalimika, sehemu salama mpaka sasa ni Jimbo la Monduli tuu!.

Kama kasi ya upepo wa mwamko kama Kanda ya Kaskazini, utaingia kanda ya Ziwa kwa kasi hiyo hiyo, then hakuna jinsi yoyote ya kuiokoa CCM isipigwe mwereka uchaguzi wa 2015!.

Determinant ya nani anakuwa rais wa nchi hii, ni wapiga kura wa Kanda ya Ziwa ambayo ndiyo inayoongoza kwa idadi kubwa ya watu!. Kati ya watu milioni 40 wa sensa ya mwaka 2002 kwa Tanzania yenye makabila 120, Wasukuma peke yao wako milioni 6!. Sasa ukiwajumlisha na Kanda ya Kaskazini, hata kama mikoa yote iliyobakia wataipigia kura CCM, bado kwa kanda hizo mbili pekee, zinatosha kabisa kuipiga chini CCM!.

Mwelekeo huu ni uthibitisho kuwa ukombozi wa kweli wa pili wa Mtanzania, sio ndoto tena, ni kitu ambacho kinawezekana!.

Natoa mwito kwa Watanzania wenye mapenzi mema na nchi yetu, tusiendekeze hizi siasa za chuki za kukichukia chama fulani bila sababu za msingi ya chuki hiyo, au kukipenda na kikishabikia chama fulani kwa upenzi tuu, matokeo ya mwisho ya siasa hizi ni kujengeana chuki zisizo na sababu!. Tupingane bila kupigana, tutofautiane kisiasa bila kuchukiana bali tupingane huku tukipendana!.

Hata mimi uchaguzi wa Arumeru, nilisimama na Sioi, tumekutana na Nasari pale Dodoma, tumekumbatiana, na kiukweli kutoka moyoni mwangu, sina chuki na Nasari, namkubali kwa dhati japo namhurumia Sioi kwa sababu ni rafiki!.

Nyie watu wa Kanda ya Kaskazini, msiichukie hivyo CCM, kwani pamoja na mabaya yake, pia kuna mema mengi imelifanyia taifa hili!.

Namalizia kwa kusisitiza, huu ni mtazamo tuu!

Wasalaam.

Pasco
Arusha.
 
Back
Top Bottom