Chromium
JF-Expert Member
- Apr 17, 2008
- 589
- 187
Habari hii si propaganda kama za CCM. Pengine ni mwendelezo wa uthubutu wa viongozi wa dini (hasa Wakristo) wanaoamua kusema ukweli kwamba hali ya mambo si shwari serikalini.
na serikali hii ambayo haivumilii kusemwa tofauti na inavyotaka, inawakemea utadhani hawapendi kabisa kusikia udini wakati wakitokea viongozi wengine wa dini wakiwasifia (kama Kulola) wananyamza na kuomba waheshimiwe. Hii ni kawaida kabisa ya serikali dhalimu.
Sasa habari hii si njema kwa CCM lakini habari ndiyo hiyo.
Jumapili iliyopita nilikuwa kanisani kwa Askofu Lazaro na kwa masikio yangu nilimsikia mzee huyu akiwaonya wakristo kutokupoteza muda kuomba mambo ambayo Mungu hatayasikia. Akisoma kitabu cha Amos 4:6 na kuendelea, Askofu Lazaro alisema wazi kwamba Mungu amemwambia ataitikisa serikali kwa namna ambayo haikupa kutokea!
Mtawala anayegombea sasa hivi, hatapata. Na kwamba Mungu amempa jina la mtu ambaye atakuwa Rais wa nchi hii (japo hakuwa tayari kumtaja kuepuka itakavyopokelewa na watu)!
Na dalili ziko wazi. Kila mwenye macho naona namna CCM kilivyoishiwa na kubaki kutengeneza propaganda zisizona miguu. Naanza kuamini kwamba ni kweli mtawala anayegombea hatapata.
Tungoje tarehe 31 Oktoba!
na serikali hii ambayo haivumilii kusemwa tofauti na inavyotaka, inawakemea utadhani hawapendi kabisa kusikia udini wakati wakitokea viongozi wengine wa dini wakiwasifia (kama Kulola) wananyamza na kuomba waheshimiwe. Hii ni kawaida kabisa ya serikali dhalimu.
Sasa habari hii si njema kwa CCM lakini habari ndiyo hiyo.
Jumapili iliyopita nilikuwa kanisani kwa Askofu Lazaro na kwa masikio yangu nilimsikia mzee huyu akiwaonya wakristo kutokupoteza muda kuomba mambo ambayo Mungu hatayasikia. Akisoma kitabu cha Amos 4:6 na kuendelea, Askofu Lazaro alisema wazi kwamba Mungu amemwambia ataitikisa serikali kwa namna ambayo haikupa kutokea!
Mtawala anayegombea sasa hivi, hatapata. Na kwamba Mungu amempa jina la mtu ambaye atakuwa Rais wa nchi hii (japo hakuwa tayari kumtaja kuepuka itakavyopokelewa na watu)!
Na dalili ziko wazi. Kila mwenye macho naona namna CCM kilivyoishiwa na kubaki kutengeneza propaganda zisizona miguu. Naanza kuamini kwamba ni kweli mtawala anayegombea hatapata.
Tungoje tarehe 31 Oktoba!