Mbelwa Germano
JF-Expert Member
- May 7, 2011
- 789
- 289
Mimi ni mmoja wa Watanzania ninayeamini kwamba Naibu katibu mkuu wa CUF ndugu Julius Mtatiro ana influence kubwa kisiasa tatizo hana jukwaa la kusimamia ndani ya chama dhaifu cha CUF japo simjui kiundani(wadau mtamchambua). Naamini Bwana Mtatiro anapoteza tu muda kwa kuwepo kwenye chama kinachopoteza umaarufu kila uchao kwa kitendo chao cha kufunga ndoa na CCM.Mfumo wa vyama vingi sio tu mwanzo wa mabadiliko ya kweli, bali vyama makini ndio mwanzo cha mabadiliko ya kweli yenye tija kwa taifa.Viko wapi NCCR,UDP,TLP n.k., yale matusi ya vyama vya msimu toka CCM hayajawagusa kwa sababu tu wao ni matawi ya CCM. Tanzania kuna chama kimoja tu cha upinzani. Ndugu Mtatiro, CHADEMA:A S 103: ndio chama sahihi kwa ndoto zako za kisiasa. Tafakari..Usipoteze muda..Fanya Maamuzi!