Mtatiro unapoteza muda CUF...karibu CHADEMA!

Baada ya Faustin Sungura kujikomba jana kwenye mdahalo akikandia hoja ya haki ya kuandamana kwa sababu anazozijua mwenyewe, aliinuka kamanda Julius Mtatiro na kusema kwa ujasiri mkubwa kile Sungura alichoshindwa kusema tena akiwa amepoteza ujasiri kabisa. Wachambuzi wa public speaking mtaona wazi kabisa kuwa Sungura alikuwa akisema kana kwamba ameambiwa ukisema tofauti na haya umekwisha. Hakusema toka nafsini mwake bali out of pressure. Mtatiro alitetea demokrasia akijua wazi kuwa kama leo mtu mmoja amefanyiwa vile, basi kesho kuna mwingine aweza kufanyiwa vibaya zaidi na kumkanushia moja kwa moja mjeshi aliyemwakilisha Mkuu wa majeshi.

Tangu siku nyingi niliwahi kuwaambia baadhi ya vijana kuwa Mtatiro ni mwanasiasa mzuri ila nahisi yuko choo cha kike. Mifano inayoonyesha ni cha kike ni kauli ya mwenyekiti wake kufanya kampeni za waziwazi msikitini hivi karibuni na picha zake kupostiwa UTube na yeye kushindwa kukanusha.

Nadhani Mtatiro hujachelewa, msimamo wako tunaufahamu, wewe bado ni kijana...unangoja nini huko CUF? Toka ndugu yangu toka ukaungane na wapambanaji wenzako mkomboe nchi hii toka kwenye mikono ya mabeberu.
Mimi naamini kabisa ipo siku Mwenyezi Mungu mwanzilishi wa haki, ataongea na moyo wa Mtatiro ahamie chadema. Spirit aliyonayo ni ya chademaa!! Sio kwamba CUF sio chama kizuri, ila tu kwasababu tunapigania ukombozi na chadema ndio inaelekea kuokoa jahazi..Nchi ya Tanzania sasahivi ni kama jahazi linalozama.
 
Unamainisha ni kama vile alivyoekwa pro.Safari na Chadema ili kujisafisha na udini?

Kwani ni Profesa Safari tu ndie Muislamu alieko CDM? Mbona tu kunae wengi tena viongozi(Wabunge) mf Zito Kabwe,Said Amur Arfi,Mustapha Akonaay na wengine wengi! Embu nitajie jina la Mbunge mmoja Mkristo alieko CUF tofauti na Julius Mtatiro mlie mpa Unaibu!?

Mtatiro sio kuwa hataki kuja CDM,anataka ila shida yake anataka kugombea Ubunge Jimbo la Ubungo km alivyojaribu 2010 na kushindwa na JJ Mnyika ambae ndie kwa sasa mbunge jimbo hilo. Anajua kuwa hataweza kupata nafasi kugombea kwa CDM.

Nataka nikuhakikishieni kuwa endapo Jimbo la Ubungo litagawanywa leo lazima Mtatiro atajiondoa CUF na kuja CDM akijua wazi kuwa atapata nafasi ya kugombea na hatimae kushindwa!! Kujiunga CDM kwa sasa hawezi anasubiri hadi karibu na uchaguzi mkuu 2015 ili aendelee kuvuta vuta ile Ruzuku ya Bi mdogo CUF kwa mara ya mwisho!
 
Kwa wanasiasa wanataka mambo mawili

kwanza nafasi ya chama ndani ya Taifa

Pili ni nafasi yake ndani ya chama

kama hayo mawili hayafungamani basi mtashuhudia misimamo ya ajabu juu ya watu hawa
 
jamani msifikiri mtatiro anapenda kuwa CUF tatizo ni nafasi aliyopewa kwenye chama, naibu katibu mkuu bara, sio cheo kidogo hicho anapata marupurupu ya kutosha hivyo inataka moyo kuachia nafasi hiyo.
 
Back
Top Bottom