Mtatiro: UKAWA imeinyanyua CUF

Mtatiro: UKAWA imeinyanyua CUF

Mtatiro umenena vizuri sana ukawa tutapambana na changamoto tulizokutana nazo
 
Mie nampongeza sana Mtatiro. Iwapo UKAWA utaendelea kusimama na kuwa na watu kama Mtatiro nina hakika kwamba tutafanya mambo makubwa siku zijazo. Tuwe na malengo ya muda mrefu. Mungu ibariki Tanzania.
 
Hivi kweli uongozi wa CHADEMA ulifanya kazi yake kuhakikisha hiyo kadhia ya Segerea haitokei? Pamoja na kutambua mchango wa yule mama katika kukijenga chama jimboni lakini ilipaswa uongozi uhakikishe kuwa anakwenda na uhalisia mpya wa UKAWA. Ilitakiwa wachukue hatua zote stahiki kuhakikisha hajitokezi kama mgombea pale. Seems a case of laxity on the part of CHADEMA leadership. So sad kwetu sisi wakazi wa jimbo hilo!
 
Serious nimesoma huo waraka wa mtatiro mpaka chozi limenitoka.
Katika watu ambao nilikuwa naomba mungu wapate nafasi a kuingia bungeni, ni julius mtatilo, ila roho imeniuma sana.

Uzembe huu usiendelee kwa ustai wa ukawa
 
Kilichotokea Segerea pia kimetokea Kigamboni. Mgombea wa CUF alifamfanyia vurugu wa Chadema baada ya kukubalika kwamba Kigamboni Ibaki Chadema na Segerea iwe na Mgombea wa CUF. Tatizo kubwa huyu wa Kigamboni aligoma hata kukaa meza ya mazungumzo na yule wa Chadema. CCM wameshinda Kigamboni kwa kura chache sana. Makao makuu ya vyama vyote hivi viwili hawakuchukua hatua za dhati kumaliza migogoro hii
 
Sijui niseme nini, Julius Mtatiro wewe ni mwanasiasa wa aina yake.
Mungu akulinde na you should remain focused the way you are. In short UKAWA au ushirikiano wa vyama vya siasa kama ilivyo sasa UKAWA na mshikamano miongoni mwao ndio njia pekee ya kukuza na kuimarisha vyama vyetu.

Ikitaka kujua umuhimu au madhara kushirikiana au kutoshirikiana angalia mfano wa jimbo lako la Segerea na kupoteza kwa majimbo ya upinzani mkoa wa Kigoma kwa kumpa advantage mgombea wa sisiemu huku wapinzani wakigawana kura miongoni na kupoteza ushindi wa dhahiri!
 
Nadhani na CUF nayo imeinyanyua sana Chadema ZNZ. Lowasa kashinda majimbo mengi zaidi na kupata kura nyingi sana Zanzibar.
 
Kazi iliyopo ni kuanza kujipanga na kujiimarisha mapema sana,viongozi wa vyama waandae strategies za kujenga vyama imara na kuhakikisha kwamba we formally aggragate our parties into strong coalition. Nadhan wabunge wa UKAWA waliolazimisha kugombea jimbo moja wamejifunza jambo...

wameamua kutumia kauli ya 'tukose wote'! mbaya sana!
 
Mpaka muda huu CUF wamelamba viti 20 hapa bado vile pending vya Temeke na Kinondoni...masikini Lipumba sijui anajisikiaje sasa hivi huko alipo...ila inaniuma Mtatiro kufanyiwa fitna na yule dada wa CHADEMA...
 
Hivi Mtatiro hana nafasi ya kupata uenyekiti bara kama akigombea?

Naona ni mtu ambae anapenda ushikamano na hana tamaa za uongozi kwa manufaa take binafsi bali maendeleo.

Ni muhimu sana huyu katika kuendeleza mshikamano huu wa vyama vya upinzani.

Kila la kheri Tanzania.
 
Huwa namfurahia sana Mtatiro, ni mwana-Siasa wa ukweli sana.
 
Mpaka muda huu CUF wamelamba viti 20 hapa bado vile pending vya Temeke na Kinondoni...masikini Lipumba sijui anajisikiaje sasa hivi huko alipo...ila inaniuma Mtatiro kufanyiwa fitna na yule dada wa CHADEMA...

Fitina zimefanyika kote kote hata Kigamboni wa CDM alifanyiwa hivyo hivyo na hata Kule kwa wenje nako kuna wa CUF alimfanyIA Fitina wenje
 
ukawa imeleta neema sana mwaka huuuu..sema baadhi tu ya sehemu ndio issue ndogo ndogo zimeharibu kama segerea ilala na kigamboni
 
kuna watu bila aibu walikua wanasema ACT Wazalendo watafanya vizuri zaidi ya CUF....narudia tena CUF inazaliwa upya mpaka sasa wabunge 20 hapa bado pale Temeke na kinondoni...madiwani kwa DAR chama cha CUF kimefanua vizuri sana...heshima kwa Maalim Seif Sheriff Hamada, Mama Sakaya na Mtatiro...
 
siku zinavyosogea mbele mamluki waliochangia ndoto zetu za kuunganisha upinzani zinafeli watajipambanua na tutaikomboa Tanzania toka kwa mkoloni mweusi ccm. peooopleeeesss
mapambano ni lazima yaenelee no matter wht.
 
Back
Top Bottom