DOKEZO Mtanzania huyu alikuja Marekani kusoma, akapata changamoto ya Akili, sasa hivi anaishi Mtaani, anahitaji msaada

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Sasa si ndo wee umsaidie hapo kwa kumuhifadhi na nk, huku ukisubiri ndugu zake wajitokezee.

Kumuacha ahangaike na huku unamtangaza, si unamchoresha tyuu.
Si rahisi kama unavyo sema hata kisheria huruhusiwi kwani itakuwa kama utekaji. Sababu huyo mdada hawezi kujieleza au tuseme hawezi kuridhia kitu. Ndiyo maana amesema wahuni 'wanajisevia', jambo jingine ni kosa kumuhifadhi mtu ambaye ni dangerous to the public. Pia hujui status ya ukaaji wake I mean visa nk. Pia huko ulaya na America sehemu ya kuishi ni wewe tu na familia yako. Hakuna Eti utalala sebuleni kwenye coach.
 
Mimi ni Mtanzania ninayeishi Marekani, kuna Mtanzania mwenzetu mbaye alikuja kama Mwanafunzi hapa, sijui vizuri kuhusu historia yake huko nyuma.

Miaka kadhaa iliyopita alipata changamoto ya Afya ya Akili, sijui nini kiliendelea baada ya hapo kati lakini kilichofuata amekuwa chizi na analala barabarani, amekuwa akifanyiwa ukatili wa kingono na Wanaume mara nyingi bila kuwa na msaada.

Nilienda Ubalozini mara kadha pia kuripoti ili ikiwezekana huyu Mtanzania asaidiwe lakini kinachoonekana wao (Ubalozi) ndio wanataka nianze kufanya kazi yao.

Wanataka kufuatilie na kujua details zaidi kuhusu huyo Mtanzania na mambo mengine kama hayo, mimi siwezi kuingilia hayo masuala ya wao, wenyewe ndio wataalam, mimi nikiwapa taarifa wanatakiwa kujua nini cha kufanya baada ya hapo.

Huyu mtanzania ninamfahamu kwa jina moja tu anaitwa Jane, mitaa ya Houston ndani ya Texas.

Maisha yake ni chini ya Daraja, amekuwa hivyohivyo akiishi chini ya Daraja.

Nilivyoanza kumjua
Kuna siku nikiwa na mke wangu kwenye bustani flani akasikia tunazungumza Kiswahili, akajumuika nasi na kuanza kuzungumza na kisha kujitambulisha.

Tukazungumza naye kwa Kiswahili na akajieleza naye anatoka Ukanda wa Kaskazini kama nilivyo mimi hapo nyumbani Tanzania.

Bahati mbaya nimesahau jina lake la pili na hata sas aukisema umuulie huwezi kupata jibu hilo.

Nimeshatoa picha zake mara kadhaa sehemu tofauti ili anayemjua iwe ni ndugu zake, jamaa au marafiki wamsaidie lakini sijafanikiwa katika hilo, ndio maana nimeona nitumie JamiiForums kufikisha ujumbe huu nadhani utawafikia wahusika na wanaweza kumsaidia.

Nipo tayari kuto ushirikiano kwa ambaye anaweza kuhitaji kumsaidia huyu au kama anawez kumtambua, nimewasilisha mawasiliano yangu kwa JamiiForums kwa mtu ambaye atahitaji kuwasiliana nami.
Tunaobakia Tanzania na kupambana na Hali zetu ( Shida ) huku tukisoma katika Vyuo Vikuu vyetu na Kula Maharage, Tembele na Dagaa huwa tunachekwa na kudharaulika mno na wale ambao huona Ulaya / Marekani ndiyo Pepo na Suluhu yao ya Maisha na Taaluma. Kudadadeki apambane na hali yake kama nasi tunavyopambana na hali zetu huku Madongo Kuinama Afrika.
 
Unatakiwa kuelewa mipaka yako na kuheshimu privacy ya mtu.

Kwanza umeenda kumrekodi bila ya ridhaa yake, unalazimisha kumpa msaada wa hela ambao auhitaji; halafu unamposti mitandaoni huo ni udhalilishaji.

Pili unalazimisha msaada kwa mtu ambae ajakuomba na hataki hiyo ni kuingilia rights zake. Dada anaonekana ni mzima maana unakiri umewahi kuongea nae na hata hapo kwenye video inaonekana anajielewa huo uchizi unampa wewe.

Tatu hujui changamoto zake za maisha hadi kua homeless, ungeanzia kudadisi hapo kimetokea nini kwenye maisha yake hadi kufikia alipofika.

Nne kama lengo ni kutaka ndugu zake wapate habari ungeweza anzisha mada kwa title yoyote na ku-crop sura yake tu na kuomba msaada kama kuna mtu anamfahamu huyo dada wakupe details za ndugu zake uwape taarifa, wao ndio wana mamlaka ya kwenda serikalini na kuomba msaada arudishwe.

Umemkosea sana huyo dada na kumdhalilisha.
Yani unachojua wewe ni kuandika kiswahili fasaha tu. Mengine 🚮🚮🚮
 
Kuwe na accountability kwa mabalozi wetu hii ni moja ya kazi zao raisi awawajibishe mabalozi wazembe kama huyu wa marekani
Ili mtu usaidiwe ukiwa huko nje ya nchi ni jukumu lako mhusika ujitambulishe pasipo shaka kuwa wewe ni Mtanzania. Sasa huyo Dada ni Kichaa, jee anavyo vitambulisho vyake? Na msaada mkubwa kwa balozi zetu huko nje ni kukupatia emergency travel document tu wala hata nauli hawatoi kisingizio kuwa hawana fungu hilo.
 
Eti msaada wa hela ambao hauhitaji!!!? Mgonjwa wa akili anajua anachohitaji? Jamaa kamtendea fadhili sana huyu dada.
Haya mambo ufanyiwe wewe harafu miaka kadhaa unarudi kawaida unajikuta mitandaoni kwamba ulikuwa unalala madarajani na unalawitiwa na wajinga kama mleta uzi ,unajisikiaje
 
Ili mtu usaidiwe ukiwa huko nje ya nchi ni jukumu lako mhusika ujitambulishe pasipo shaka kuwa wewe ni Mtanzania. Sasa huyo Dada ni Kichaa, jee anavyo vitambulisho vyake? Na msaada mkubwa kwa balozi zetu huko nje ni kukupatia emergency travel document tu wala hata nauli hawatoi kisingizio kuwa hawana fungu hilo.
Mtu kichaa atajitambulisha vipi, kama balozi kapelekewa taarifa na mleta mada hadi leo hajachukua hatua yoyote, na hapo ndipo tatizo lilipo kazi ya balozi sio tu kukupa emergency travel document it goes beyond that
Balozi ni kama nchi ndogo ndani ya nchi ,ni kufuatilia maslahi ya tanzania na watanzania ndani ya nchi husika, siyo kuvimbisha vitambi tu
 
Unatakiwa kuelewa mipaka yako na kuheshimu privacy ya mtu.

Kwanza umeenda kumrekodi bila ya ridhaa yake, unalazimisha kumpa msaada wa hela ambao auhitaji; halafu unamposti mitandaoni huo ni udhalilishaji.

Pili unalazimisha msaada kwa mtu ambae ajakuomba na hataki hiyo ni kuingilia rights zake. Dada anaonekana ni mzima maana unakiri umewahi kuongea nae na hata hapo kwenye video inaonekana anajielewa huo uchizi unampa wewe.

Tatu hujui changamoto zake za maisha hadi kua homeless, ungeanzia kudadisi hapo kimetokea nini kwenye maisha yake hadi kufikia alipofika.

Nne kama lengo ni kutaka ndugu zake wapate habari ungeweza anzisha mada kwa title yoyote na ku-crop sura yake tu na kuomba msaada kama kuna mtu anamfahamu huyo dada wakupe details za ndugu zake uwape taarifa, wao ndio wana mamlaka ya kwenda serikalini na kuomba msaada arudishwe.

Umemkosea sana huyo dada na kumdhalilisha.
Ndugu hapa ndio umefikiri mpaka mwisho au tusubiri mengine? Nadhani haujafikiri sawasawa. Rudia kusoma ulichoandika
 
Back
Top Bottom