Nimesoma hapo kwa huyo jamaa wa Nairobi mwenye hiyo kampuni ambayo imethibitika haijasajiliwa Kenya (GR Construction Limited) nime- conclude hao Aga Khan nao wanastahili lawama, haiwezekani wafanye kazi na kampuni isiyosajiliwa, hapa nahisi baadhi ya maofisa wake watakuwa wanahusika na huo mchezo mchafu.
Lakini pia, kitendo cha FBI kutilia shaka nyendo za huyo jamaa mpaka waanze kumtafuta inaonesha jinsi taasisi zetu za kiuchunguzi hapa ndani zilivyolala, au inawezekana nao ni sehemu ya hilo dili kuna kitu walipewa wakafungwa midomo.
Nasema hivi kwasababu mabenki yetu mara nyingi yamekuwa yakitoa taarifa za wateja wao kwa serikali, na hao Baclays wana tawi Tz, sasa vipi kwa huyo muhusika ishindikane kumgundua mapema? hapa wafanyakazi wa hiyo benki wanatakiwa kujibu maswali.