Mtandao wa Yahoo Wadukuliwa Tena kwa Mara Nyingine

muvika online

JF-Expert Member
Nov 27, 2016
375
283
Mtandao-wa-Yahoo.jpg



Mtandao wa Yahoo kwa mara nyingine tena umetangaza kwa wateja wake kuwa huwenda akaunti zao zikawa haziko salama kutokana na kugundulika kwa udukuzi mwingine uliofanyika kati ya kipindi cha mwaka 2015 na 2016.

Katika hudukuzi huu Yahoo ilituma meseji maalum kwa watumiaji wake ikiwataka kuchukua hatua za kuongeza ulinzi kwenye akaunti zao kwa mujibu wa tovuti za bgr na thenextweb kwenye shambulio hilo wadukuzi hao hawakutumia password ili kupata uwezo wa kuingia kwenye akaunti yoyote bali walitumia mtindo wa forged cookie ambapo wadukuzi hao walipata uwezo wa kuingia kwenye akaunti ya mtu bila hata kuhitaji password.

Tovuti hizo zinaendelea kuandika kuwa wadukuzi hao waliweza kuiba programu maalum kutoka kwa kampuni ya yahoo ambapo baadae waliweza kubadilisha programu hiyo na kuitumia kutengeneza forged cookie ambapo baadae ndizo zilizotumika kudukua mtandao huo maarufu. Hii ni mara ya tatu kwa mtandao huo kudukuliwa baada ya mtandao huo kudukuliwa na akaunti bilioni moja kuathirika, pamoja na shambulizi lingine lililofanyika miaka ya nyuma. Mtandao wa yahoo unaonekana kukubwa na matatizo mengi sana kipindi hichi wakati kampuni ya Verizon ikataka kununua mtandao huo. Ni vyema kuchukua hatua mapema kama unatumia Email ya Mtandao huo.
 
Huwenda maana jana nimeingia upande wa data recovery method just in case nimesahau password nimekutana na email ambayo sikuiweka mimi na ipo pale kama njia moja wapo ambayo kama nitasahau password basi itumwe link kupitia email hiyo.

Nashauri wenzangu wenye kutumia yahoo mchunguze kuhusu hilo
 
Hivi hata sie makapuku kina kajamba nani tunatakiwa tuhofie udukuzi wa Yahoo kwa kipi cha kuhofia kuibiwa?
mambo ya kimtandao yapo complicated. Leo unaweza kusema no body who cares

Lakini naku assure kuwa kuna mtu mahala fulani anataka kujua wewe ni nani na unafanya nini

Kisa tu kaona unatumia jina lisilo kuwa la kwako hapa JF.
 
Back
Top Bottom