Mtaalam wa kupinga (betting)

MAMENGAZI

JF-Expert Member
Dec 31, 2010
780
128
Bibi mmoja alikua ana deposit pesa nyingi benki kiasi kwamba meneja wa benki aliamua kwenda kumtembelea maana alikua ni mmoja kati ya wateja waliokuwa na deposits kubwa, alipofika nyumbani kwa bibi akamweleza kuwa alikuja kumtembelea kwa sababu ni mteja wao mzuri na pia angependa kujua bibi anafanya biashara gani zinazomuingizia pesa nyingi hivyo. Bibi akamwambia yeye hua anapinga (bet) na watu na mara nyingi huwa anashinda.

Meneja alishindwa kuamini na akamwambia huwa unapinga na watu kuhusu nini? bibi akamwambia kama unataka tupinge na wewe halafu utaona, meneja akamwambia kama nini? bibi kasema tupinge kama kesho asubuhi utaamka ukiwa na nyeti zako. meneja kusikia vile akasema haiwezekani, basi wakapinga kuwa akiamka asubuhi akakuta hana nyeti atampa bibi milioni 20 na akiamka akikuta anazo bibi atampa milioni 20. bibi akamwambia atakwenda ofisini kwa meneja kesho yake ili akamuneshe.

Meneja alivyoondoka tu bibi akaenda kwa baba mmoja akapinga nae kua kesho atakwenda ofisini kwa meneja wa benki na atamwambia meneja amuoneshe nyeti zake na atakubali, na wakakubaliana kuwa meneja akikubali bibi atapata milioni 40 na akikataa bibi atalipa kiasi hicho cha fedha.

Meneja hakulala usiku mzima anaangalia kwenye kioo kama nyeti zipo au la mpaka asubuhi akawahi kazini.

Ilipofika saa nne bibi akaingia ofisini kwa meneja na akamwambia amekuja na shahidi asije akamdhulumu, meneja akakubali. bibi akamwambia yule baba aingie na kumuamuru yule meneja avue nguo amuoneshe nyeti zake. Kwasababu meneja alikua anauhakika kuwa nyeti zipo akavua haraka na bibi akamgeukia yule baba akamwambia umeona haya nipe hela yangu. akalipwa 40m akampa meneja 20m akaenda kudeposit balance.
 
Hii mbona ya mwaka juzi?!!....poor translation though! hahahhaaa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom