mireille
JF-Expert Member
- Mar 4, 2020
- 523
- 568
MWANAHERI BINTI WA KIJAKAZI 1
MTUNZI SMILE SHINE
WHATSAPP:0688156169
MWANAHERI Ni binti alielelewa na mzazi wake mmoja ambae Ni mama yake baada ya baba yake mzazi kufariki miaka mitano iloyopita, maisha ya mama mwanaheri na mwanae yalikuwa Ni maisha ya shida Sana, mama mwanaheri aliamua kufanya kazi kwenye majumba ya watu Kama kufua na kufanya usafi ilimladi wapate kuishi na mwanae.
Japo walikuwa na Hali ngumu na kipato duni mama mwanaheri alijitahidi Sana kumsomesha binti yake mpaka akamalizia kidato Cha nne , mwanaheri alifaulu vizuri lakini mama yake alishindwa kabisa kumsomesha ikabidi mwanaheri akae nyumbani kumsaidia mama yake kazi ndogo ndogo Kama vile kuuza vitumbua na maandazi . Kutokana na ucheshi na kuongea Sana pia kauli nzuri ilifanya biashara kwenda vizuri.
" Haya haya mama zamda toka nje uje ununue andazi lililokandwa kwa Nazi bila kusahau hiriki andazi Lina lika kwa kinywaji chochote ukija Sasa hapo kwenye kitumbua kimechambuka sio ugali Kama Cha mwafulani njooni kwa wingi jamani nikishapita ndio imetoka hiyo. Watu walikuwa wanamiminika kuwahi kununua
" Huyo ndio mwanaheri anavyojua kupiga debe Sasa.
" Sio kupiga debe tu bidhaa zangu zinajitangaza wewe unatafananisha vitumbua vyangu na vile vya Bibi Pili mishavu.
" Basi utasikuwa we mtoto utuletee balaa hapa
" Kumbe na nyie mnaogopa kuchambwa .
Badae ya kuishi maisha ya kubangaiza mama mwanaheri alibahatika kupata kazi kwenye jumba moja la kifahari alilipwa mshahara mzuri kidogo maisha yao yalibadilika , hatimae siku zilienda na maisha yakaendelea
Siku moja usiku mama mwanaheri alipata homa ya ghafla akamwambia mwanae
" Mwanaheri mwanangu naumwa sijui Kama kesho nitaweza kwenda kazini
" Sasa kazini utaendaje na hiyo hali ona unavyotetemeka utaenda kufanya kazi gani huko?
" Lakini kesho Kuna kazi nyingi mtoto wa boss wetu anamvalisha mchumba wake Pete Sasa sijui Kama nitaeleweka.
" Kwanini asikuelewe Sasa kwani wao hawajawahi kuumwa au ndio kwasababu masikini hatuna pesa tunafanya kazi Kama punda.
" Sio hivyo mwanangu nilifikiria Kama itawezekana ungeenda kwaajili yangu
" Khaaa mama Sasa naanzaje kwenda wakati na Mimi Nina Mambo yangu
" Hayo Mambo yako hayana faida kesho tutaenda pamoja nitakukabidhi kwa mfanyakazi mwenzangu ili msaidiane alafu Mimi nitaenda hospital.
" Sawa Ila Mimi Mambo yakurudi jioni sitaki Mambo ya mtaani yatanipita
" Mwanangu huo umbea wa mtaani unakusaidia Nini kutwa kucha Ni kusutana unajua sipendi hiyo tabia Basi tu hujui .
" Basi tusifike huko unaumwa pumzika hapo kesho nitaenda kwenye hiyo kazi yako .
Usiku ule walilala kulipokucha mama yake alimuamsha
" Mwanaheri amka kumekucha mwanaheri aliamka kivivu huku akijinyoosha
" Ndio uamke uache uvivu wako
" Nimeshaamka mama wewe nenda kajiandae. Mama mwanaheri alipotoka chumbani mwanaheri alirudi kulala aliporudi akakuta ndio kwanza mwanaheri anavuta shuka
" Jamani mtoto mvivu wewe hebu amka haraka . Aliongea mama yake huku akimpiga kibao mwanaheri aliamka na kujishika alipopigwa
"Mamaa Sasa ndio nini kunipiga asubuhi subuhi kwani hujui vibao vya asubuhi vinavyouma
" Nimekwambia amka haraka muone unachojua wewe Ni umbea tu nyooo. Mwanaheri aliamka akiwa kanuna akaenda kujiandaa alipomaliza waliondoka na mama yake mpaka kwenye Hilo jumba la kifahari
" Kumbe hapa ndipo unapofanyia kazi ? Aliuliza mwanaheri huku akiangaza macho kuangalia mazingira yakuvutia ya Ile nyumba kabla mama yake hajajibu alitokea mama mwenye nyumba na kuwasalimia
" Habari za asubuhi ! Mama mwanaheri akaitikia
" Salama mmeamkaje?
" Salama
" Mama Taliq huyu Ni binti yangu anaitwa mwanaheri. Mwanaheri alimsalimia mama Taliq
" marahaba jamani kumbe una binti mrembo hivi, karibu Sana mwanaheri
" Asante nimekaribia Leo nipo hapa mpaka jioni .mama Taliq aliachia tabasamu
" sawa Tena imekuwa vizuri leo tunasherehe ya Taliq anamvalisha Pete mchumba wake.
" Sawa Sasa mama si uombe hiyo ruhusa uwahi hospital Mimi ndio nimeshafika
" Kumbe mama mwana unaumwa Sasa si ungepumzika
" Nimekuja kuomba ruhusa alafu kwakuwa kutakuwa na kazi nyingi nimemleta mwanaheri aje asaidie saidie kidogo.
" Umefanya vizuri Basi mwanaheri nenda kule utakuta wenzio watakuelekeza Nini Cha kufanya
" Sawa. mwanaheri alienda alipoelekezwa akawaacha mama yake na boss wakiongea mama Tariq alitoa kiasi Cha pesa na kumpa
" Chukua hii kwaajili ya matibabu. Mama mwanaheri alisita kupokea
"Usiogope chukua . Alipokea na kumshukuru Kisha akaondoka .
Mwanaheri alipoingia ndani alianza kushangaa alisogelea kwenye kabati la kioo lililokuwa pale sebleni
" Jamani matajiri siwawezi kumbe wao hawana shida yakununua samaki wanafuga wenyewe ona walivyokuwa wazuri . Mwanaheri alifurahishwa na wale samaki waliokuwa wakizunguka ndani ya yale maji
" Mbona hii inavutia kuangalia ona wamepanda mpaka majani . Alitaka kuingiza mkono Mara akasikia anaambiwa
" Oya unafanya Nini hapo? Mwanaheri alishituka akageuka kumuangalia aliyemuongelesha
MTUNZI SMILE SHINE
WHATSAPP:0688156169
MWANAHERI Ni binti alielelewa na mzazi wake mmoja ambae Ni mama yake baada ya baba yake mzazi kufariki miaka mitano iloyopita, maisha ya mama mwanaheri na mwanae yalikuwa Ni maisha ya shida Sana, mama mwanaheri aliamua kufanya kazi kwenye majumba ya watu Kama kufua na kufanya usafi ilimladi wapate kuishi na mwanae.
Japo walikuwa na Hali ngumu na kipato duni mama mwanaheri alijitahidi Sana kumsomesha binti yake mpaka akamalizia kidato Cha nne , mwanaheri alifaulu vizuri lakini mama yake alishindwa kabisa kumsomesha ikabidi mwanaheri akae nyumbani kumsaidia mama yake kazi ndogo ndogo Kama vile kuuza vitumbua na maandazi . Kutokana na ucheshi na kuongea Sana pia kauli nzuri ilifanya biashara kwenda vizuri.
" Haya haya mama zamda toka nje uje ununue andazi lililokandwa kwa Nazi bila kusahau hiriki andazi Lina lika kwa kinywaji chochote ukija Sasa hapo kwenye kitumbua kimechambuka sio ugali Kama Cha mwafulani njooni kwa wingi jamani nikishapita ndio imetoka hiyo. Watu walikuwa wanamiminika kuwahi kununua
" Huyo ndio mwanaheri anavyojua kupiga debe Sasa.
" Sio kupiga debe tu bidhaa zangu zinajitangaza wewe unatafananisha vitumbua vyangu na vile vya Bibi Pili mishavu.
" Basi utasikuwa we mtoto utuletee balaa hapa
" Kumbe na nyie mnaogopa kuchambwa .
Badae ya kuishi maisha ya kubangaiza mama mwanaheri alibahatika kupata kazi kwenye jumba moja la kifahari alilipwa mshahara mzuri kidogo maisha yao yalibadilika , hatimae siku zilienda na maisha yakaendelea
Siku moja usiku mama mwanaheri alipata homa ya ghafla akamwambia mwanae
" Mwanaheri mwanangu naumwa sijui Kama kesho nitaweza kwenda kazini
" Sasa kazini utaendaje na hiyo hali ona unavyotetemeka utaenda kufanya kazi gani huko?
" Lakini kesho Kuna kazi nyingi mtoto wa boss wetu anamvalisha mchumba wake Pete Sasa sijui Kama nitaeleweka.
" Kwanini asikuelewe Sasa kwani wao hawajawahi kuumwa au ndio kwasababu masikini hatuna pesa tunafanya kazi Kama punda.
" Sio hivyo mwanangu nilifikiria Kama itawezekana ungeenda kwaajili yangu
" Khaaa mama Sasa naanzaje kwenda wakati na Mimi Nina Mambo yangu
" Hayo Mambo yako hayana faida kesho tutaenda pamoja nitakukabidhi kwa mfanyakazi mwenzangu ili msaidiane alafu Mimi nitaenda hospital.
" Sawa Ila Mimi Mambo yakurudi jioni sitaki Mambo ya mtaani yatanipita
" Mwanangu huo umbea wa mtaani unakusaidia Nini kutwa kucha Ni kusutana unajua sipendi hiyo tabia Basi tu hujui .
" Basi tusifike huko unaumwa pumzika hapo kesho nitaenda kwenye hiyo kazi yako .
Usiku ule walilala kulipokucha mama yake alimuamsha
" Mwanaheri amka kumekucha mwanaheri aliamka kivivu huku akijinyoosha
" Ndio uamke uache uvivu wako
" Nimeshaamka mama wewe nenda kajiandae. Mama mwanaheri alipotoka chumbani mwanaheri alirudi kulala aliporudi akakuta ndio kwanza mwanaheri anavuta shuka
" Jamani mtoto mvivu wewe hebu amka haraka . Aliongea mama yake huku akimpiga kibao mwanaheri aliamka na kujishika alipopigwa
"Mamaa Sasa ndio nini kunipiga asubuhi subuhi kwani hujui vibao vya asubuhi vinavyouma
" Nimekwambia amka haraka muone unachojua wewe Ni umbea tu nyooo. Mwanaheri aliamka akiwa kanuna akaenda kujiandaa alipomaliza waliondoka na mama yake mpaka kwenye Hilo jumba la kifahari
" Kumbe hapa ndipo unapofanyia kazi ? Aliuliza mwanaheri huku akiangaza macho kuangalia mazingira yakuvutia ya Ile nyumba kabla mama yake hajajibu alitokea mama mwenye nyumba na kuwasalimia
" Habari za asubuhi ! Mama mwanaheri akaitikia
" Salama mmeamkaje?
" Salama
" Mama Taliq huyu Ni binti yangu anaitwa mwanaheri. Mwanaheri alimsalimia mama Taliq
" marahaba jamani kumbe una binti mrembo hivi, karibu Sana mwanaheri
" Asante nimekaribia Leo nipo hapa mpaka jioni .mama Taliq aliachia tabasamu
" sawa Tena imekuwa vizuri leo tunasherehe ya Taliq anamvalisha Pete mchumba wake.
" Sawa Sasa mama si uombe hiyo ruhusa uwahi hospital Mimi ndio nimeshafika
" Kumbe mama mwana unaumwa Sasa si ungepumzika
" Nimekuja kuomba ruhusa alafu kwakuwa kutakuwa na kazi nyingi nimemleta mwanaheri aje asaidie saidie kidogo.
" Umefanya vizuri Basi mwanaheri nenda kule utakuta wenzio watakuelekeza Nini Cha kufanya
" Sawa. mwanaheri alienda alipoelekezwa akawaacha mama yake na boss wakiongea mama Tariq alitoa kiasi Cha pesa na kumpa
" Chukua hii kwaajili ya matibabu. Mama mwanaheri alisita kupokea
"Usiogope chukua . Alipokea na kumshukuru Kisha akaondoka .
Mwanaheri alipoingia ndani alianza kushangaa alisogelea kwenye kabati la kioo lililokuwa pale sebleni
" Jamani matajiri siwawezi kumbe wao hawana shida yakununua samaki wanafuga wenyewe ona walivyokuwa wazuri . Mwanaheri alifurahishwa na wale samaki waliokuwa wakizunguka ndani ya yale maji
" Mbona hii inavutia kuangalia ona wamepanda mpaka majani . Alitaka kuingiza mkono Mara akasikia anaambiwa
" Oya unafanya Nini hapo? Mwanaheri alishituka akageuka kumuangalia aliyemuongelesha
Smile shine | HUSNA 1___20
www.tupohapa.com