Msongo wa mawazo na madhara yake!

Msongo wa mawazo na madhara yake!

Mbu

JF-Expert Member
Joined
Jan 11, 2007
Posts
12,752
Reaction score
7,876
tumblr_mnzlelAUqK1sordgyo1_500.jpg tumblr_mnzlelAUqK1sordgyo1_500.jpg &[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];...


Hebu leo tujadiliane Usongo wa Mawazo katika MMU. Tangu zamani pamekuwepo na matukio ya Mauaji ya kimapenzi, ama kusikia Mwanaume au Mwanamke amejiua kutokana na "wivu" wa kimapenzi.

Watu hawa ni sawa na mimi na wewe katika maisha ya kila siku, mpaka linapotokea tukio ndipo unapopatwa na akili "dahhh;.!" kumbe jamaa hakuwa wa kawaida!

Hebu jiangalie unajielewa vipi kukabiliana Usongo wa mawazo kukuepusha na madhara makubwa kwako, kwa mwenza wako na jamii inayokuzunguka.

Kama ushawahi jiambia, "sioni faida ya maisha!" "sina thamani tenasitapata mwingine tena Nishaonekana sina maana somo hili linakuhusu sana.

Chukulia umegombana na Mpenzi wako, au hata mzazi wako, au ndugu yako kipenzi,Unakabiliana vipi na maumivu hayo?

Je, hujifungia chumbani peke yako na kutafakari?
Je, hujiamulia kutoka nje kufunga upepo peke yako?
Je, huwatafuta Marafiki mwende nao sehemu ukajiliwaze?
Je, Kuna mtu (mpango wa pembeni) ambaye humtumia kujiliwaza nae?
Au, wewe ni katika wale wanaochukulia hizi ni changamoto za kawaida&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];.litapita tu?

Kumbuka!

Pombe, sigara, ngono, etc&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];. kwa wengi ni "short term solutions" kwa matatizo yanayosababisha Usongo wa Mawazo.

Karibuni tujadiliane

Cc; Eiyer Dark City BAK King'asti MwanajamiiOne Rock City Mentor, Nyamayao The Boss sakapal TIMING AshaDii Tuko EMT Fixed Point afrodenzi BelindaJacob, na wengineo wote mnaohusika katika "mada nzito"
 
Ingawa watu tunatofautiana but kuna some points tunafanana. Binafsi sio rahisi kuvurugwa kimawazo na mtu kutokana na kuwa naamini kila mtu ana weaknesses zake including me. Yote uliyoyataja hapo juu napractice kulingana na situation but linalofanya kazi ni muda. Kujipa mda kabla ya kureact na sometimes nalazimika kupanga hata safari ili kupitisha mda kabla sijaamua...
 
Sometimes ni bora kujitenga na mtu anayekusababishia msongo wa mawazo, vingivyo you will be dragged down. Sumu ya kwanza ukiwa na mawazo ni kukaa alone, unaanza kuona mauza uza na watu wenye mapembe.

Njia rahisi, kaa na watu, chagua watu unaowaamini uwashirikishe shida yako.

Kumbe hujanimensheni?
 
Ingawa watu tunatofautiana but kuna some points tunafanana. Binafsi sio rahisi kuvurugwa kimawazo na mtu kutokana na kuwa naamini kila mtu ana weaknesses zake including me. Yote uliyoyataja hapo juu napractice kulingana na situation but linalofanya kazi ni muda. Kujipa mda kabla ya kureact na sometimes nalazimika kupanga hata safari ili kupitisha mda kabla sijaamua...

safi sana,….!

Maana inakubalika, "You can't Control what you feel, But you can control what you think!"
kwa kitendo cha kujipa muda ina maana umeweza jijengea 'Delaying' tactics za maana…
sawa na wale wanaosema 'fikiri kabla ya kutenda' badala ya 'kutenda kabla ya kufikiri'

Naamini kwa wanaotaka kujifunza zaidi toka kwako, watataka kujua umewezaje mpaka
ukafanikiwa kui train [Tame!] akili yako mpaka wewe ukawa unaiongoza akili yako 'badala akili kukuongoza.'

Big Up Bro.

 
Sumu ya kwanza ukiwa na mawazo ni kukaa alone, unaanza kuona mauza uza na watu wenye mapembe.
hii huwa naipenda sana. Inanisaidia kujitafakari....
Huwa kitu cha kwanza kukifanya ni kujifungia na kulia sana, yaani nalia mpaka nione nimetosheka......
Ninapomaliza hapo huwa naanza kutafakari kilichotokea, naweka issue kwenye angle zooteee. najaribu kujiweka kwenye shoes za aliyenitenda, kama ningekuwa mimi ningefanya hivyo? namuhukumu na kumtetea mimi mwenyewe. Nikijiridhisha naanza kusali, kwenye process nampa msamaha (ndani ya moyo wangu). Nikishamsamehe nakutana naye kumtaarifu nimemsamehe na kujadili the way forward (kuendelea au kummwaga).
 
Sometimes ni bora kujitenga na mtu anayekusababishia msongo wa mawazo, vingivyo you will be dragged down. Sumu ya kwanza ukiwa na mawazo ni kukaa alone, unaanza kuona mauza uza na watu wenye mapembe.

Njia rahisi, kaa na watu, chagua watu unaowaamini uwashirikishe shida yako.

Kumbe hujanimensheni?


……hahahaha, Kongosho jamani, si nimeandika 'na kwa wote wanaohusika na mada nzito!'
Hiyo in a manna Including You, ningewataja wote ninaowaaminia kwa hoja nzito mbona ukurasa ungejaa!

Ulichoandika ni sahihi kabisa,
Hilo la kuchagua watu unaowaamini uwashirikishe shida yako japo,
kwakuanzia ni aheri uchague watu Sahihi, maana si kila unayemwamini atakuwa mtu sahihi
kukupa ushauri sahihi kulingana na matatizo yako.

Kuhusu kujitenga peke yako, ndio tunarudi kwa Bro Tuko na hoja zake, uwezo wa mtu binafsi
kuchanganua baya na zuri, lipi aanze nalo na lipi alisubirishe, nk….
maana kama ulivyoandika, kuna watu wengine LONELINESS ndio tatizo zaidi kuliko akiwa kazungukwa na watu.

Je, unaonaje tactic ya #kumface huyo anayeku drag down badala ya kumkimbia kimbia?
Njia mojawapo ya kupambana na Bully, ni kukabiliana nae….au?
 
Sometimes ni bora kujitenga na mtu anayekusababishia msongo wa mawazo, vingivyo you will be dragged down. Sumu ya kwanza ukiwa na mawazo ni kukaa alone, unaanza kuona mauza uza na watu wenye mapembe.

Njia rahisi, kaa na watu, chagua watu unaowaamini uwashirikishe shida yako.

Kumbe hujanimensheni?

Japokuwa hajakumensheni lakini umeandika mapwenti ya nguvu. #team_Zombie
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Nina miaka mingi sijalia, kweli ukiona yatima ana ndevu basi moyo una mvi.


Maumivu yanayosababisha msongo wa mawazo mara nyingi huwa ni mauzmivu ya muda mrefu, wakati mwingine ni kitu kinachotokea kwa mchakato wa taratubu hata inakuwa ngumu kugundua kuwa kinakuletea msongo.

Sasa sijui utajitengaje na watu ili upate wasaa wa kulia. Unapokuwa natatizo lazima kuna muda ule wa mwenyewe kutafakari na kuumia kabla hujakata shauri la kushirikisha watu au kufanya maamuzi.


Watu wengi wanajiua huwa wanakuwa na dalili za kujitenga, ndio maana unapokuwa na msongo wa mawaza unashauriwa kukaa na watu. Ni hatari kuwa na msongo mkali afu ukakaa peke yako.

hii huwa naipenda sana. Inanisaidia kujitafakari....
Huwa kitu cha kwanza kukifanya ni kujifungia na kulia sana, yaani nalia mpaka nione nimetosheka......
Ninapomaliza hapo huwa naanza kutafakari kilichotokea, naweka issue kwenye angle zooteee. najaribu kujiweka kwenye shoes za aliyenitenda, kama ningekuwa mimi ningefanya hivyo? namuhukumu na kumtetea mimi mwenyewe. Nikijiridhisha naanza kusali, kwenye process nampa msamaha (ndani ya moyo wangu). Nikishamsamehe nakutana naye kumtaarifu nimemsamehe na kujadili the way forward (kuendelea au kummwaga).
 
hii huwa naipenda sana. Inanisaidia kujitafakari....
Huwa kitu cha kwanza kukifanya ni kujifungia na kulia sana, yaani nalia mpaka nione nimetosheka......
Ninapomaliza hapo huwa naanza kutafakari kilichotokea, naweka issue kwenye angle zooteee. najaribu kujiweka kwenye shoes za aliyenitenda, kama ningekuwa mimi ningefanya hivyo? namuhukumu na kumtetea mimi mwenyewe. Nikijiridhisha naanza kusali, kwenye process nampa msamaha (ndani ya moyo wangu). Nikishamsamehe nakutana naye kumtaarifu nimemsamehe na kujadili the way forward (kuendelea au kummwaga).

…..mnh?

Nahisi kama Tuko na Kongosho wana mtizamo tofauti juu ya hili,
maana hata mimi kuna jambo nahisi halipo sawa hapa….

Kwanini wewe pekee ndiwe uwe unalizwa na kusamehe?
Why do you deserve that?

Wasiwasi wangu, mtu wa aina yako siku utayoamua kusema enough is enough ndio
itayokuwa siku ya Carnage...

Sikuhukumu, tunajadiliana njia mbali mbali za kui-tame akili kupambana na Usongo wa Mawazo
kutokana na 'dharura' na majanga mbali mbali yanayoweza tokea.
 
Last edited by a moderator:
Mambo yanayohusu mapenzi kwangu hayawezi kuniletea msongo wa mawazo hata siku moja. Msongo unaweza kunipata pale nitakapoona maisha yangu yako matatani kama vile kuwaza namna ya kuendesha maisha yangu mwenyewe na familia yangu; hapo ndo nawaza kwa undani zaidi.
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
hii huwa naipenda sana. Inanisaidia kujitafakari....
Huwa kitu cha kwanza kukifanya ni kujifungia na kulia sana, yaani nalia mpaka nione nimetosheka......
Ninapomaliza hapo huwa naanza kutafakari kilichotokea, naweka issue kwenye angle zooteee. najaribu kujiweka kwenye shoes za aliyenitenda, kama ningekuwa mimi ningefanya hivyo? namuhukumu na kumtetea mimi mwenyewe. Nikijiridhisha naanza kusali, kwenye process nampa msamaha (ndani ya moyo wangu). Nikishamsamehe nakutana naye kumtaarifu nimemsamehe na kujadili the way forward (kuendelea au kummwaga).
Unalia umekuwa mtoto?
 
Ok, maelezo ya kutomensheniwa accepted.

Nakubaliana na wewe, wakati mingine tunaowaamini aidha wanakuwa na conflict of interest na ushauri unaofaa au hawana maarifa ya kutushauri. Kitu sahihi ni kubalansi nadhani, kati ya mtu sahihi na unayemwamini kutoa ushauri. Kuna mada zingine ziko too personala hata kuziongelea tu, achilia mbali ziwe zinakuhusu wewe na unataka kupata ushauri. Imagine mwanamme aliyefanyiwa kinyume, hili si suala la kumweleza tu mtu sahihi, bali pia hata uaminifu wa kutunza shida hiyo uwepo. A mambo ya afya, mtu una vvu vinakuleleta msongo, kunamwingine ukimwambia tu, hata kama ni mtu sahihi mtaa mzima utajua na amani yako ya moyo itatoweka zaidi.

Kuhus kumface mtu anayeku-drag down inategemea na sihu yenyewe ni ipi. Kuna mambo unweza mfae mtu na mkaongea na kuelewana na kila mtu akatoka na amani. Sasa fikiria iwe ni mwenza asiye mwaminifu, unamface vipi? Hapa Suprise anahusika. Mwenza ameshakiri anachit sababu shetani anmzidia, na umeshamshika zaidi ya mara kadhaa, si bora kuondoka ama kutafuta njia mbadala(the nasty ones:A S-confused1:-kuchit pia) ili msongo huo upungue?

Kuna wengine misongo inasababishwa na ndugu wa karibu walioamua kuharibu maisha yao kwa makusudi labda ulevi and the like. Mtu wa aina hiyo unamsaidiaje zaidi ya ushauri tu? Kama hashauriki si bora kusepa tu?


……hahahaha, Kongosho jamani, si nimeandika 'na kwa wote wanaohusika na mada nzito!'
Hiyo in a manna Including You, ningewataja wote ninaowaaminia kwa hoja nzito mbona ukurasa ungejaa!

Ulichoandika ni sahihi kabisa,
Hilo la kuchagua watu unaowaamini uwashirikishe shida yako japo,
kwakuanzia ni aheri uchague watu Sahihi, maana si kila unayemwamini atakuwa mtu sahihi
kukupa ushauri sahihi kulingana na matatizo yako.

Kuhusu kujitenga peke yako, ndio tunarudi kwa Bro Tuko na hoja zake, uwezo wa mtu binafsi
kuchanganua baya na zuri, lipi aanze nalo na lipi alisubirishe, nk….
maana kama ulivyoandika, kuna watu wengine LONELINESS ndio tatizo zaidi kuliko akiwa kazungukwa na watu.

Je, unaonaje tactic ya #kumface huyo anayeku drag down badala ya kumkimbia kimbia?
Njia mojawapo ya kupambana na Bully, ni kukabiliana nae….au?
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: Mbu

Sikuhukumu, tunajadiliana njia mbali mbali za kui-tame akili kupambana na Usongo wa Mawazo
kutokana na 'dharura' na majanga mbali mbali yanayoweza tokea.
kila mtu ana namna yake ya kukabiliana na msongo wa mawazo, siyo sababu mimi kukaa mwenyewe inanisaidia basi na wengine pia watumie hiyo.
Unaweza kuamua kukutana na watu, ikatokea wasiwe sahihi au wasikupe ushauri wa kukufariji na ukaishia pabaya zaidi.
Binadamu tumepewa uwezo wa kutafuta solution za matatizo yetu kwa kutumia njia mbalimbali, na mara nyingi watu wanachagua njia ambayo anaiona ni rahisi sana kwake au anayoiweza.
By the way, sijasema kama mimi pekee ndo naumizwa.... Pia nilishasema mara nyingi sana kwa upande wangu kusamehe is not an option, ni lazima. Ili kitu kitoke kwenye mawazo yangu ni lazima nisamehe. Kusamehe hapa haimaanishi kuendelea na mahusiano, kusamehe kwa kitu ulichonifanyia
 
Nina miaka mingi sijalia, kweli ukiona yatima ana ndevu basi moyo una mvi.


Maumivu yanayosababisha msongo wa mawazo mara nyingi huwa ni mauzmivu ya muda mrefu, wakati mwingine ni kitu kinachotokea kwa mchakato wa taratubu hata inakuwa ngumu kugundua kuwa kinakuletea msongo.

Sasa sijui utajitengaje na watu ili upate wasaa wa kulia. Unapokuwa natatizo lazima kuna muda ule wa mwenyewe kutafakari na kuumia kabla hujakata shauri la kushirikisha watu au kufanya maamuzi.


Watu wengi wanajiua huwa wanakuwa na dalili za kujitenga, ndio maana unapokuwa na msongo wa mawaza unashauriwa kukaa na watu. Ni hatari kuwa na msongo mkali afu ukakaa peke yako.
ukiona bado hujalipuka ujue maumivu hayajafika sehemu yake.... yanaweza yakaja taratibu ukayapuuzia huku ukiyaweka kichwani lakini siku yakilipuka ndo utakapoona kila rangi.... huo ndo muda ninaoutumia hasa kuwa mwenyewe. na inanisaidia.
Unapoamua kujitenga ni vizuri ukawa unajua hasa nia yako ya kujitenga. Unaweza kujitenga kwa muda na ukapata solution nzuri sana kwa msongo wako kuliko kusikiliza huyu na yule wanasema nini. kuna ambao wanajiua pia kwa kusikiliza maneno ya watu, kila mtu anakuambia lake mpaka unajiona kama huna maana tena unaona ni bora uishie.
 
Mbu,

Msongo wa mawazo ni rahisi sana kumpata mtu bila kujitambua.

As for me, I had a chance to work with such people at some point in my life na ilinifundisha jambo muhimu kuhusu msongo wa mawazo.

Take life easy...!!!

BTW, nina malalamiko na mimi sikutajwa!!! Ama mimi huwa sichangii mada nzito <beef>
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: Mbu
katika kukabiliana na hali hiyo wengi wananjia tofauti. Kunamwingne hataki kuliona hata jua, mwingne likitokea jambo atacheka na kuendelea na maisha, mwingne atatafuta watu awaelezee kisa kizima hata wakimcheka kwa upande wake atakuwa keshatua mzigo..kila jambo linafaida na hasara zake. Kwa wanaopenda kukaa wenyewe kujiua ama kufanya lolote baya yaweza chukua muda mfupi sana kwani hana mtu wa kutuliza hisia zake zinapofikia juu. Anaependa kuyasema nae anaweza ishia kuua ama kutenda ovu lolote kwani si kila unaemwambia atakutuliza, wengne wataingza emotions zao kwenye jambo lako....
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Nilishapatwa na hii kitu, na ilikuwa ngumu. Niliondoka nyumbani, nikaenda kwa dada na nikawa mtu wa kukaa ndani tu. Nilikuwa nasoma kila kitabu, jarida au kitu chochote kilicho mbele yangu kama njia ya kujidistruct.
Ilibaki nusura niolewe na mtu just for the sake of it, namshukuri dada aliniokoa tena na hilo.

Recently yakipandana sana kichwani, naishia kusali tu (kufunga, novena etc). Anyway, mimi sio mtu sana wa kuyatoa kwa mtu mwingine yale yanayonisumbua hasa, nikishare ni ya juu juu tu na mostly kwa ajili ya kumfanya mtu aone namtegemea. So l think nikiacha kusali, au nisingekuwa na mtoto ninayempenda sana, huenda nami ningekuwa candidate wa suicide.
 
Nilishapatwa na hii kitu, na ilikuwa ngumu. Niliondoka nyumbani, nikaenda kwa dada na nikawa mtu wa kukaa ndani tu. Nilikuwa nasoma kila kitabu, jarida au kitu chochote kilicho mbele yangu kama njia ya kujidistruct.
Ilibaki nusura niolewe na mtu just for the sake of it, namshukuri dada aliniokoa tena na hilo.

Recently yakipandana sana kichwani, naishia kusali tu (kufunga, novena etc). Anyway, mimi sio mtu sana wa kuyatoa kwa mtu mwingine yale yanayonisumbua hasa, nikishare ni ya juu juu tu na mostly kwa ajili ya kumfanya mtu aone namtegemea. So l think nikiacha kusali, au nisingekuwa na mtoto ninayempenda sana, huenda nami ningekuwa candidate wa suicide.
rafiki, believe me usingejiua.....
wangapi wanajiua na wana watoto na vitu vingine vingi tu ambavyo wanavipenda.
wewe hiyo ndo style yako ya ku-deal na msongo wa mawazo. kama hapo juu nilivyosema, kila mtu ana style yake, na inamsaidia. Mimi pia natumia sana hiyo ya kujifungia, kusali na kujitafakari, na hata siku moja sijawahi jiwa na wazo la suicide.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Omba yote bali sio uombe kukosa amani kazini! Naapa bado muda mfupi sana nitaanzisha mambo yangu. Nina msongo wa mawazo sana ambao ni kidudu mtu mmoja tu ndio ananisababishia haya.....
 
Back
Top Bottom