Msomi ni nani

Msomi ni nani

Msomi ni yule aliye yamudu mazingira yanayo mzunguka.. .mengine ni mbwembwe na sifa za kipuuzi tu.
Na kuyafanya hayo mazingira yawe na tija kwake na kwa jamii
 
Msomi ni mtu aliyefikia ngazi ya chuo kikuu na kuspecialise kwenye taaluma fulani. Mfano: O'level alisoma kemia, A'level alisoma kemia, bachelor degrer alisoma kemia, master's degree alisoma kemia na PhD alisoma kemia. Huyu ndio unaweza kumuita msomi! Achana na na hao wanaosema msomi ni mtu anayeweza kuyamudu mazingira na kutatua changamoto. Kuna watu wapo vijijini wameyamudu mazingira ya kijijini na wanaweza kutatua changamoto zinazowakabili kulingana na mazingira wanayoishi vijijini hawajaenda shule hata darasa moja. Je, hao utawaita wasomi? Msomi ni mtu aliyesoma vitu vya darasani na kubobea kwenye kitu kimoja huyo ndo msomi.
 
Mbobezi wa swala furani kitaaluma hizo zingine ni fitna za Mjini Mjini tuyy
 
Nimejiuliza sana ili mtu awe ni msomi anapaswa awe na sifa zipi kadhalika tutaupimaje USOMI wake bado sijapata jawabu.Katika imani yangu sifa kuu ya kuwa mkristo ni kubatizwa lakini kipimo kikuu cha ukristo ni MATENDO MEMA.Sasa ukiwapima wakristo utagundua wengi ni wakristo kwa majina tu lakini kiroho ni wapagani.Hii inanipa shaka na uhusiano wa elimu au vyeti na utendaji wa brain ya mhusika.Naomba majibu waungwana
 
wasomi Ni wanasheria Tu, kwa sababu they always keep on learning (msije mkaelewa vibaya)
 
msomi ni mtu yeyeto aliyeweza kugundua kitu chake mwenyewe,waliobakia wote wanakariri tu!
 
wasomi Ni wanasheria Tu, kwa sababu they always keep on learning (msije mkaelewa vibaya)
Programmers, it securities na wao kila kukicha they keep on learning ,hata hackers pia ni wasomi kila kukicha wanabuni virus,Trojans,loopholes na njia za kupita

Kwahy unavyosema wanasheria tu unakosea..batilisha msemo wako
 
Zamani wakati Mwakyembe alipowatibua waandishi wa habari wa gazeti la Rai
walikuwa wanamwitwa 'Mwanakisomo' wakiepuka kumuita 'msomi'

so kuna 'wanakisomo' na kuna 'wasomi'
 
msomi ni mwenye hela, kama wewe ni msomi halafu huna hata mia unajidanganya,, tumia usomi wako upate pesa
 
Msomi ni mtu anaye weza ishi jijini bila kazi maalum na mambo yanasonga.
 
Definition ya msomi ni m2 yte anaetumia maarifa alyoyapta kuleta utofauti chanya ktk jamii yke jamiiii inanufaika direct au indirect kutokna na uwepo wa usomi wke
 
Msomi ni mtu ambaye hana aibu. Mfano unatafuna michango ya waathirika kama ya tetemeko la ardhi bila kuwa na aibu.
 
Wabongo hata hoja serious mnazifanyia masihara halafu ndio mnataka kuendesha viwanda, mtasubiri sana
 
Nimejiuliza sana ili mtu awe ni msomi anapaswa awe na sifa zipi kadhalika tutaupimaje USOMI wake bado sijapata jawabu.Katika imani yangu sifa kuu ya kuwa mkristo ni kubatizwa lakini kipimo kikuu cha ukristo ni MATENDO MEMA.Sasa ukiwapima wakristo utagundua wengi ni wakristo kwa majina tu lakini kiroho ni wapagani.Hii inanipa shaka na uhusiano wa elimu au vyeti na utendaji wa brain ya mhusika.Naomba majibu waungwana
Msomi au wasomi ni watu wanaopoteza muda wao kusoma MAWAZO ya watu wengine kwenye vitabu nk....huo ndio uelewa wangu.
 
msomi ni mtu yeyeto aliyeweza kugundua kitu chake mwenyewe,waliobakia wote wanakariri tu!
Mtu anayegundua kitu chake ni MGUNDUZI, kisha anaandika kwenye vitabu kile alichogundua hapo ndipo wanatokea WASOMI kuja kuyasoma yale yaliyoandikwa.
 
Back
Top Bottom