Msomi ni nani

Msomi ni nani

Msomi ni mtu yeyote aliyefikia kiwango fulani che elimu lakini akiwa na upeo mpana wa masuala mbalimbali. Mfano Mtu kasomea Udaktari lakini ana upeo/Uelewa wa mambo ya nchi yanavyokwenda/Elimu ya uraia, anaelewa hoja za mambo ya biashara, uchumi, mazingira N.K kwa kiwango fulani na sio ubobezi. Ukimuona mtu anajua mambo ya kada aliyosomea tu uyo tunamuita mwana taaluma. Mtu aliyobebea kwenye Fani yake tu na kada nyingine akiwa mtupu hana tofauti na mtu asiyekwenda shule maana hata mtu ambaye hajakwenda anakuwa amembobea kwenye shughuli anayoifanya lakini kungine anakuwa mtupu.Ndio maana mitaala ya Olevel-Alevel na baadhi ya vyuo hasa vya serikali vina lazimisha baadhi ya masomo kama vile Hesabu, Kingereza, Uraia/Development studies ili uongeze uwezo wa kufikiri katika nyanja zinginezo. Nafikiri utakuwa umepata mwanga fulani.
 
  • Thanks
Reactions: JMF
Habar wapendwa,
nimekuwa nikijiuliza sana ni ipi tofauti ya msomi na mtu mwenye elimu maana unakuja kuta mtu amesoma ila elimu hana na mwengine ana elimu lakini hajasoma

je utofauti uko wapi? ???????
 
Mawakili ndo wasomi wengine wana elimu hata uwe profesa wa elimu, hatukuiti msomi lakini wakili ni msomi.
Hivi unajua ni bora kuelimika (kuwa na elimu) kuliko kuwa msomi kwa Tz??
Ebu angalia sasa mawakili wasomi hawajui hata kutafsiri taratibu za kumpatia mtu dhamana wanaishia kulalama wakati ufinyu wao wao wa akili??!!
 
Hivi unajua ni bora kuelimika (kuwa na elimu) kuliko kuwa msomi kwa Tz??
Ebu angalia sasa mawakili wasomi hawajui hata kutafsiri taratibu za kumpatia mtu dhamana wanaishia kulalama wakati ufinyu wao wao wa akili??!!
Ishu ya dhamana
Wao ndo wasomi, kupata dhamana ni haki yako lakin pia ni utaratibu wa kisheria unabidi uwe mpole kila kitu kilishapangwa na kipo kwenye sheria soma sheria ya mwenendo ya makosa ya jinai namba 20 iliyofanyiwa marejeo mwaka 2002, kifungu kuanzia 64--69 utaelewa namna ya kupata dhamana
 
Msomi anauwezo wa kuchanganua mambo kwa kina hata kama ameishia form 4 but mwenye elimu anaweza akawa amefika level ya juu but hawezi kureason
Umeongea kinyume chake. Elimu ni taaluma au maarifa yanayoendana na vitendo. Mtu mwenye elimu ataonekana kwa kufanya vitendo ambavyo ndani yake kuna maarifa na mara nyingi vinakuwa na matokeo chanya ila msomi linatokana na neno kusoma yaani aliyekariri maandishi fulani. Na kuna level tofauti tofauti za usomi na wala haziendani na vitendo. Tanzania tuna wasomi wengi ila hawana elimu
 
1. Msomi ni yule alaienda shule mfano sekondary mpaka chuo kikuu...
2. Mwenye elimu huyu ni mtu mwenye uelewa na kitu fulan anaweza kua msomi au asiwe msomi ila akawa na ufahamu na maswala fulan mfano mtu ambae hajasoma lakini ana yajau mambo ya dunia mfano elimu dunia
 
Back
Top Bottom