Eeeh Mungu! wenye nia njema na wanione ili wanistiri na mimi!!!!
Napenda kwanza kutoa salaam kwenu nyote.
Jamani nimekuja hapa mbele yenu kwa lengo la kutafuta mwenza ili tustiriane. Najua huwa ni ya kushangaza kwa wengi pale mwanamke anapojitokeza na kuamua kutafuta mume maana haiendani na tamaduni zetu, naomba mtambue kwamba yamenifika shingoni na naona naumia moyoni kwa kusubiri hilo litokee, kwani muda unaenda na natamani hasa kuwa na mwenzangu katika dunia ya mahusiano. Naamini Mungu atanisaidia katika hili. Basi naomba kwa atakae kuwa na nia njema ajitokeze ili nami niweze kufarijika. Sifa zangu ni kama zifuatavyo;
Jinsia: KIKE
Umri:33
Elim: Degree
Kipato: Muajiriwa
Rangi:Mng'avu ila sio mweupe
Umbo: Mwembamba
Kimo: ~160cm
Dini: Islam
Sifa za mwenza
Umri:35-45
Elim: Yeyote tu ila angalau form six
Kipato: Sio lazima muajiriwa ila ni uhakika tu wa kusaidiana kutunza familia
Rangi:yeyote
Umbo: Awe wa kawaida ile sio mnene sana
Kimo: chochote tu
Dini: Islam
Kwa mawasiliano tafadhali naomba tutumie Private message (PM) au email:
gcmrcm2011@gmail.com.
Natanguliza shukran zangu za dhati na nipo tayari kwa maswali yenu.
Karibuni waungwana.