Kweli wengi wanazani Simba itaathirika kama wanavyo fikria kitu ambacho sicho.Huyo ole Mushi kawa mjinga shabiki wa kweli hawi influenced na muomgeaji wa team, wengine tumeanza ushabiki wa team Simba tangu utoto, huyo manara hata hakuwepo. Ushabiki hunoga team ikifanya vizuri and not otherwise
Nimekuelewa sana mkuu sina pingamizi na wewe.Simba wapo Moroco pre season wanajifua vilivyo ili wafanye vizuri.Yanga kama timu wakifanya vizuri uwanjani hata hamasa za Haji zitakua na tija.
uwezi kufanya kazi na mtu anaejiona yeye ni mkubwa kuliko club wakati perfomance ya timu ndo imempa huo ukubwa anaojivunia,kama maneno mengi ni kigezo cha timu kufanya vema basi Ruvu shooting ya Masau Bwire ingekuwa angalau nafasi ya tatu iliyoshikwa na Azam wasio na msemaji mwenye maneno na blabla nyingi.
Simba ndo imewainua wachezaji na watendaji wote wa timu akiwemo na Haji kwa ubora wa kikosi chake misimu iliyopita.
Kwenye pitch kutaamua kati ya maneno na ubora wa timu kipi ni sahihi.
Kweli kabisa hapo nimekuelewa.Ole mushi amekua mjinga, kwenye yanga day mwaka uliopita walijaza uwanja kwani manara alikua kwao?.TIMU nyingi za nje zinajaza uwanja kwani wao wana manara?...
Yanga hawamuhitaji manara kwa lolote lile, ila GSM ndio anamuhitaji manara kwa ajili ya issue zake kupiga Pesa..
Tunaenda kuchukua ubingwa, tunawabonda kwenye ngao ya jamii ndio mtajua manara anacheza namba ngapi.
Au Mtibwa Sugar sababu ya Thobias Kifaru?Kwahiyo na ruvu shooting huwa inajaza mashabiki uwanjani kwa sababu ya maneno ya Masau Bwire
Kuna watu akili zao Ni Mungu tu ndio anajua wanawaza nini.Au Mtibwa Sugar sababu ya Thobias Kifaru?
Naunga mkono hoja Yanga ina viongozi wenye akili kama za kuku! Hakukua na sababu yotote ile ya kumchukua huyo Mbwatukaji. Angebakia zake tu kuwa Balozi wa hayo Makampuni anayo fanya nayo kazi.Akina Mwakalebela wamefanya ujinga wa kijinga.
Hisa za Bongo hata kama simba na yanga wangekuwa registered DSE zisingeathirika na Haji Manara.MSIMCHUKULIE POA MANARA
.
Ameandika @Thadei Ole Mushi.
1.Kama Hisa za Simba zingekuwa sokoni kwa sasa lazima zingeshuka Sana huku za Yanga zikipanda kwa kitendo Cha Manara kuhamia Yanga.
2. Kibiashara Simba kapoteza, hamasa ya Haji kwenye Mpira si ya kuhoji. Kwanza Jersey za Simba hazitatoka Sana kama mwanzo kutokana na kejeli za Manara, lakini pia Simba haiwezi kujaza Uwanja Kwa kiwango Cha Manara alipokuwa akiwapa Hamasa. Hili halitajificha soon tutaliona.
3. Kuna watu wanasema Maneno kwenye Mpira si kitu hivyo Manara Hana athari zozote. Kikubwa wanachosahau watu wa namna hii ni Kuwa soka letu la ndani Ladha yake ni maneno haya ya kina Manara.
Hakuna Timu inaendeshwa ki- professional kama Azam wanachokikosa Azam ni Ladha hii ya kina Manara. Ndio maana Masau Bwire anaweza kukufanya ukaifuatilia Ruvu shooting bila kujua Mchezaji hata mmoja wa Ruvu Shooting. Hii ndio Ladha halisi ya Mpira wetu.
4. Wanaolalamika Manara kwenda Yanga waambie walitaka afanyeje? Abaki nyumbani? Au arudi kule Simba? Yaani Manara asikilize Mtu aliyepo huko Tandahimba kashiba mihogo yake kuwa usiende Yanga halafu utamjazia mafuta ya gari wewe? Utamlisha? Utahudumia familia yake? Yaani aache Dili la GSM kisa aliwahi kuwa Simba?
Mnaombeza Manara hamjui mlifanyalo, Simba kapoteza na kama Fred Vunjabei angelijua haya yangetokea asingekubali kuweka ule mzigo wake Kwenye jersey ya Simba. Lazima mauzo yashuke kutokana na kitendo hiki.
Tusubiri tuone.
NB: Mimi nimewasilisha kwako wala sijaandika mimi haya yameandikwa na Ole Mushi hivyo msinipige vijembe binafsi si shabiki wa YANGA Mimi ni SIMBA