Msimamo wa UKAWA mi wa wananchi 17,000.
We kweli bado sana, sijui kama hata huwa unatafakari kile unachoandika. Hii sensa ilifanywa lini na wapi? Na ilifanywa na idara gani ya Serikali!?
Na msimamo wa CCM ni wa wananchi wangapi?
Nafikiri sasa ifike muda tummsahau huyu mtu maana nashangaa kila siku zito,halafu habari yenyewe ni ya kawaida tu,kwa UKAWA ilipofika sasa si lazima zito atuunge mkono ndio ionekane UKAWA wana hoja za msingi hata bila zito UKAWA tunasonga mbele.Viva UKAWA.
Hahahahaha lol!!!! Anajaribu kupima upepo unaelekea kipande ipi naye aunge tela.... Chezeya usaliti weye!!!!
Katiba ya nchi haiwezi kuandikwa bila maridhiano ya makundi yote. Sitakwenda Dodoma licha ya ushauri mbalimbali kwamba nikasemee ndani. Nitakwenda kwenye Bunge la Katiba pale tu nitakaporidhika kuwa kuna maridhiano baina ya makundi na wadau. Ushauri wangu ni kusitisha Bunge Maalumu na kukubaliana maeneo kadhaa ya kurekebisha katika Katiba ya sasa kisha tupate muda wenye utulivu baada ya uchaguzi mkuu mwaka 2015 ili kuandika Katiba Bora. Umoja wa Katiba Bora yenye ridhaa ya wananchi ndio kupona kwa nchi yetu dhidi ya machafuko. Wenye kudhani Katiba ni sawa na ushabiki wa Simba na Yanga wasubiri Ligi Kuu ianze waende Uwanjani kushabikia.
Tatizo lake haaminiki....!
Kama alichosema kimetoka moyoni mwake, basi fahamu zake zimerudi nyumbani.
At least Zitto kaonyesha ukomavu kidogo kwenye hili
kwa kauli kama hii anaweza kupimika kweli? hivi kwani msimamo wa ACT kwenye katiba mpya ni upi?
UKAWA wangekuwa sahihi kama wangefuata Sheria! Ila ni mabingwa wa kulaumu kuwa wengine hawafuati Sheria wakati wao ni wakiuka Sheria wakubwa!
Zitto ni kichwa ndio maana huwa hasukumwi kufanya jambo na mtu,huwa anaamini na kukisimamia ipasavyo kile anachokiona ni sahihi.Hakuna kioongozi makin kama zzk
Ameanza kuweweseka,mara sina uhakika na UKAWA kama utadumu